lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
banner
Mengineyo
»Matamko mengine
»Habari Mpya
»Makala mbalimbali
»Midahalo
»Blogu za wanachama
»Picha za matukio
»Maoni Yenu
b.part
Barua Pepe
jina la mtumiaji:
neno-siri
rt.bt.spc
bt.part2

TAMKO LA BARAZA KUU LA CHADEMA KUHUSU UCHAGUZI MKUU 2005

Sisi, wajumbe wa Baraza Kuu la Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA tuliokutana leo Mei Mosi mwaka 2006 katika Ukumbi wa Haidery Plaza, tumepokea ripoti ya uchaguzi mkuu 2005 ambayo inajumuisha taarifa za uchaguzi toka kwa ngazi mbalimbali za chama kote nchini, tumetathmini na kujadili kwa kina uchaguzi husika na kwa pamoja tumeazimia kutoa tamko hili linaolotoa msimamo wa CHADEMA kuhusu mapungufu, mafanikio, mapendekezo na mwelekeo kuhusu uchaguzi mkuu 2005. Tunaamini tamko hili litakuwa changamoto kwa wanaCHADEMA, mamlaka zinazohusika, wadau mbalimbali na Watanzania kwa ujumla kuboresha mchakato wa demokrasia nchini hususan katika chaguzi zinazofuata. Aidha tunawashukuru watanzania wote waliotuunga mkono kwa hali na mali na tunawapongeza walioukuwa wagombea wetu wote katika uchaguzi mkuu pamoja na viongozi wa CHADEMA ngazi mbalimbali kwa jitihada walizozifanya katika uchaguzi mkuu 2005.


MAPUNGUFU

Uchaguzi Mkuu 2005 HAUKUWA HURU NA HAKI kutokana na mapungufu yafuatayo ya msingi:


  1. Ahtari za Uchaguzi wa ngazi za Mtaa na Vijiji wa Mwaka 2004: Mfumo wa utawala wa nchi yetu katika maeneo mengi unaanzia katika vijiji na mitaa ambayo ina mamlaka kadhaa ya kiutendaji na kimaamuzi. Uchaguzi wa ngazi hii hufanyika mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu hivyo hutumika kama msingi wa vyama vya siasa katika uchaguzi mkuu na kuandaa mfumo wa chama kutawala kuanzia ngazi za chini. Uchaguzi huu kwa mwaka 2004 haukuwa huru na haki kwa mapungufu mengi mathalani upigaji kura kutokuwa wa siri, fujo katika vituo, matayarisho hafifu, kuingiliwa na maafisa watendaji wa kata na vijiji ambao walifikia hata hatua ya kuwatisha wananchi na kutotoa taarifa za muhimu za uchaguzi, kukosekana kwa daftari la wapiga kura na uchaguzi kusimamiwa na chombo kisicho huru cha kiserikali moja kwa moja (Wizara ya TAMISEMI). Kutokana na mapungufu haya CCM ilishinda kwa asilimia 96 na kupata mtaji haramu wa kisiasa ambao ilianza nao kama hujuma katika uchaguzi mkuu 2005 na kufanya uwanja wa ushindani wa kisiasa usiwe sawa.

  2. Mapungufu katika Uandikishaji: Vituo vya kujiandikisha vilikuwa mbali na hivyo baadhi ya watu kushindwa kuandikishwa. Pia wananchi wa maeneo mapana waliandikishwa katika eneo moja na hivyo kufanya utaratibu wa kugawa vituo na wananchi kufahamu vituo vyao kuwa mgumu. Ushiriki wa vyama vya siasa katika kuhakikisha kuwa mawakala wa vyama wanakuwepo siku zote za uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura (DKWK) ulikuwa mdogo. Pia vifaa vilikosekana katika baadhi ya maeneo kabla ya siku ya mwisho ya uandikishaji na hivyo wengine kukosa fursa ya kuandikishwa. Zoezi la kuhakiki daftari nalo lilikuwa duni. Vyama vilipewa DKWK yenye orodha ya watu milioni 16 siku chache kabla ya kwenda kupiga kura na taratibu hazikutoa fursa ya wapinzani kuhakiki. Hivyo watu mbalimbali wengi wao wakiwa wanachama wa upinzani walinyimwa kuandikishwa na wengine waliofamika kuwa ni wana CCM hata wasio na sifa waliandikishwa hasa Zanzibar.

  3. Wananchi hususan Wanachama wa Upinzani kunyimwa ama kuogopeshwa kwenda kupiga kura: Palikuwa na utaratibu wa majina kubandikwa nje ya vituo ambapo katika maeneo mbalimbali baadhi ya wananchi wengi wao wakiwa ni wanachama wa vyama vya upinzani walizuiwa kupiga kura pamoja na kuwa na vitambulisho vya kujiandikisha kwenye DKWK - ama kwa kukosa majina yao nje ya vituo au taarifa zao kuwa na mapungufu au kutokuwepo kabisa katika daftari. Ishara zinaonyesha kuwa huu ulikuwa ni mkakati rasmi kwa kuwa siku kadhaa kabla ya uchaguzi watendaji wa chama tawala hususan wajumbe wa nyumba kumi walipita na kuandikisha namba za wapiga kura katika maeneo yao. Kwa kuwa wananchi wengi walikuwa na elimu finyu ya uraia na kwamba katika baadhi ya maeneo wajumbe hawa wanasikilizwa sana na/au hata kuogopwa, wapiga kura wengi waliorodheshwa na hata wengine kutishwa kuwa kura zao zitajulikana na hivyo wasipoipigia kura CCM watashughulikiwa. Vitisho hivi vilipata nguvu kutokana na utaratibu wa kuchukuliwa namba za shahada za wapiga kura na wasimamizi wa vituo wakati wa kupiga kura. Hii ilifanya uchaguzi usiwe huru.
    endelea...

lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl