lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
banner
Maelezo ya Tume
»Sifa za Mbunge
»Sifa za Diwani
»Uteuzi Wagombea
»Mapingamizi
»Kufanya Kampeni
»Upigaji Kura
»Kuhesabu Kura
»Kujumlisha Kura
»Viti Maalum
b.part
Habari za Uchaguzi
»Jiandae kwa 2010
»Jiandae kwa 2009
»Ilani ya 2005
»Utekelezaji wa Ilani
»Ripoti ya Uchaguzi
»Gharama za 2005
»Matokeo kura Urais
»Matokeo Ubunge
»Matokeo kimkoa
»Kura za Awali
b.part

Pingamizi dhidi ya Uteuzi wa Mgombea Ubunge

Wanaoruhusiwa kutoa pingamizi

  1. Mgombea yeyote wa Jimbo la Mgombea anayepingwa
  2. Mkurugenzi wa Uchaguzi
  3. Msimamizi wa Uchaguzi


  4. Mtu mwingine yeyote haruhusiwi

Muda wa kutoa pingamizi

Baada ya saa kumi (10.00) jioni ya siku ya uteuzi, mpaka saa kumi (10.00) jioni ya siku inayofuata

Sababu za pingamizi

Sababu ya pingamizi inaweza kuwa yoyote kati ya zifuatazo:

  1. Maelezo yaliyopo katika fomu ya uteuzi hayatoshi kumtambulisha mgombea;
  2. Fomu ya uteuzi haitimizi au haikuwasilishwa kwa mujibu wa masharti yaliyowekwa na Sheria;
  3. Kutokana na maelezo yaliyoandikwa katika Fomu ya uteuzi ni dhahiri kwamba Mgombea Uchaguzi hana sifa zinazotakiwa;
  4. Uthibitisho wa Msimamizi wa Uchaguzi unaopaswa kutolewa haukutolewa;
  5. Mgombea hana sifa zote zinazohitajika;
  6. Hakuna picha ya mgombea;
  7. Hakuna uthibitisho kuwa mgombea amelipa dhamana ya shilingi Elfu hamsini (50,000/=)


Utaratibu wa Msimamizi wa Uchaguzi Kutoa Pingamizi

Kwa mujibu wa kifungu cha 40(5) cha Sheria ya Uchaguzi namba 1/85 endapo Msimamizi wa Uchaguzi atakuwa na pingamizi dhidi ya mgombea, ataweka pingamizi na kumwarifu Mgombea kwa maandishi kabla ya kutoa uamuzi wake. Kama mgombea ana maelezo atayawasilisha kwa Msimamizi wa Uchaguzi. Baada ya Msimamizi wa Uchaguzi kutoa uamuzi atawasilisha uamuzi wake Tume ya Taifa ya Uchaguzi akiambatisha maelezo ya mgombea.

Uamuzi wa Msimamizi wa Uchaguzi

Kabla ya kutoa uamuzi juu ya pingamizi, Msimamizi wa Uchaguzi atamjulisha mgombea nayepingwa ili aweze kuitolea maelezo kama atakuwa nayo. Baada ya kupata taarifa za pande zote, Msimamizi wa Uchaguzi anaweza kuendelea kutoa uamuzi wake. Hata kama anayepingwa hatatoa majibu, Msimamizi wa Uchaguzi anaweza kutoa uamuzi wake.

Rufaa dhidi ya pingamizi

  1. Msimamizi wa Uchaguzi atamweleza aliyetoa pingamizi, kukata rufaa kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi endapo hakuridhika na uamuzi wa Msimamimzi wa Uchaguzi katika muda wa saa 48 tangu kutolewa kwa uamuzi wa Msimamizi wa Uchaguzi. Rufaa itawasilishwa kwa kutumia Fomu namba 12.


  2. Msimamizi wa uchaguzi atapokea rufani hizo na kuziwasilisha Tume pamoja na maelezo yake.

Kipindi cha Kampeni       Soma Zaidi...


lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl