lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
banner
Mengineyo
»Matamko mengine
»Habari Mpya
»Makala mbalimbali
»Midahalo
»Blogu za wanachama
»Picha za matukio
»Maoni Yenu
b.part
Barua Pepe
jina la mtumiaji:
neno-siri
rt.bt.spc
bt.part2

Waziri Magufuli ingilia kati hatma ya wakazi Kibamba

  1. Utekelezaji wa mradi wa Miundo Mbinu ya ngazi ya wilaya eneo la Luguruni na Kibamba Hospitali kukiuka sheria za ardhi za Tanzania na haki za makazi
  2. Maofisa wanaotuhumiwa kujihusisha na rushwa na kuvunja haki za binadamu katika utekelezaji wa mradi wachukuliwe hatua
  3. Mchakato wa mradi uwekwe wazi kwa Umma

Kwa tamko hili naungana na wakazi wenzangu wa Jimbo La Ubungo wanaokaa katika Kata ya Kibamba kupinga kitendo cha kutaka kuwahamisha Kimabavu kutoka katika ardhi na makazi yao ambavyo wamemiliki kihalali kwa mujibu wa sheria za nchi ya Tanzania kwa kushirikisha ngazi zote za Serikali ya Muungano wa Tanzania zikiwemo Serikali za Vijiji, Mitaa, Kata, Manispaa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi.  Kuwahamisha Kimabavu ni ukiukwaji mkubwa wa Sheria za Ardhi pamoja na Haki za Makazi kama zilivyoainishwa katika Tamko la Kimataifa ya Haki za Binadamu, ambayo Tanzania imesaini. 

Kwa hakika, vitendo vya watumishi wa Wizara yako, Halmashauri ya Jiji na Manispaa ya Kinondoni waliokabidhiwa jukumu la kutekeleza mradi huu vimepelekea utekelezaji wa mradi huu kuchukua sura ya kuhamisha watu kimabavu kutokana na kukiuka kabisa mwongozo wa uhamishaji watu kama ulivyoainishwa katika Sheria ya Kimataifa ya Haki za Binadamu na Haki za Makazi; mikataba ambayo Tanzania imeridhia. Na baada ya kuridhia Serikali ya Tanzania iliwajibika kuuingiza mwongozo huo katika Sheria za Ardhi zinazoongoza watu kuhamishwa kutoka katika Ardhi na Makazi yao.

Hivyo basi namuomba Mhe John Magufuli- Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi kuingilia kati suala la wananchi wa Jimbo la Ubungo Kata ya Kibamba kuhamishwa kimabavu katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundo mbinu eneo la Luguruni na Kibamba Hospitali na kufanya yafuatayo:-

  1. Wizara yako isitishe notisi ya siku 30 iliyotolewa kwa waathrika kuwa wamehama.
  2. Wizara yako isitishe vitendo vya kuvunja mkataba kati yake na wananchi wa Luguruni na Kibamba Hospitali uliofikiwa mwezi Febrauari 2007 kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ngazi ya wilaya eneo la Luguruni na Kibamba Hospitali kwa kutumia ardhi ya wananchi waliopo.
  3. Wizara yako ifanyie uchunguzi wa kina malalamiko ya ukiukwaji taratibu zilizomo ndani ya Sheria ya Ardhi na Sheria ya Kimataifa ya Haki za Binadamu na Haki za Makazi.
  4. Wizara yako isitishe zoezi zima la utekelezaji wa mradi huu hadi hapo tathmini itakayo washirikisha waathrika kuhusu kuepukika au kutoepukika kwa uhamishwaji watu katika utekelezaji wa mradi huu. Mchakato wa mradi mzima uwekwe wazi kwa umma ikiwemo bajeti ya mradi na mchakato wa utekelezaji. Kama Serikali (Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi, JIJI na Manispaa ya Kinondoni) hazitaki kuwashirikisha waathrika katika kupendekeza mbinu mbadala badala ya watu kuhamishwa,  ziwajibike kuhakikisha inapata ridhaa wote itakaowahamisha badala ya kufanya hivyo kwa mabavu.
  5. Endapo baada ya tathmini shirikishi, baadhi ya kaya zitalazimika kuhamishwa, mpango kabambe ambao utakaokuwa shirikishi uandaliwe kuhusu hatma ya kaya zitakazolazimika kuhamishwa. Mpango huo uandae kwa uwazi  raslimali za kutosha kuwalipa fidia itakazowezesha kaya husika kurejea katika kiwango cha maisha walioyokuwa nayo kabla ya kuhamishwa.
  6. Endapo baada ya tathmini shirikishi, baadhi ya kaya zitalazimika kuhamishwa tathmini ya thamani ya mali ifanyike upya ikiwashirikisha independent valuers kwa nia ya kuepuka vitendo vya wananchi kudaiwa rushwa.
  7.  Wizara yako isimamie majadiliano ya pamoja kati ya watekelezaji wa mradi na waathrika kutathmini endapo zipo mbinu zinzoweza kutumika kuepuka watu wasihamishwe kutoka katika ardhi na makazi yao k.m waathrika wakaelekezwa kuwekeza katika miradi mchanganyiko na makzi kama inavyofanyika eneo la Kariakoo.
  8. Wizara yako, JIJI na Manispaa ya Kinondoni viyafanyie uchunguzi wa kina madai yote ya rushwa, ufisadi na ukiukwaji wa haki za binadamu vinavyodaiwa kutendwa na maafisa waliopewa jukumu la kutekeleza mradi huu kwa nia ya kuwabaini watumishi wasio waaminifu ili waondolewe wasiiendelee kuipaka Serkali matope mbele ya wananchi. (kama ilivyoelezewa katika barua ya wazi ya wananchi kwa mamlaka zinazohusika ya tarehe 03 Januari 2008.)

Imetolewa 16 Januari 2008 na:

John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana Taifa(CHADEMA) na Mkazi wa Jimbo la Ubungo

lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl