lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
banner
Mengineyo
»Matamko mengine
»Habari Mpya
»Makala mbalimbali
»Midahalo
»Blogu za wanachama
»Picha za matukio
»Maoni Yenu
b.part
Barua Pepe
jina la mtumiaji:
neno-siri
rt.bt.spc
bt.part2

Tamko la Vijana wa CHADEMA lililoazimiwa Oktoba 21,2006 na kusambazwa Novemba 14,2006 lilitamka pamoja na mambo mengine nanukuu, "Vijana wa CHADEMA tunatoa mwito kwa vijana wote ambao kwa namna mmoja au nyingine walitapeliwa na serikali kuwasilisha malalamiko yao CHADEMA kwa ajili ya kuanza ufuatiliaji“.

Kadhalika imeandikwa kwenye gazeti la Mwananchi Novemba 23,2006 kwamba "CHADEMA kimewataka wanafunzi walioandikishwa na serikali ili wapewe mikopo ya kujiunga na elimu ya juu na baadaye kurejeshwa nyumbani kwa kunyimwa mikopo hiyo, wafike katika ofisi za chama hicho ili kiwasaidie kupata haki yao".

Tunapenda kutoa ufafanuzi na maelekezo yafuatayo:

Yapo makundi mawili makubwa ya walalamikaji:

mbowe

  1. Mosi, wapo ambao wako katika daraja la kwanza wanaume na daraja la kwanza na la pili wanawake ambao pamoja na kwamba serikali imetangaza kwamba wanastahili kupewa mikopo kuna ambao hawapati mikopo husika. Na sehemu kubwa ya watu katika kundi hili ni wale ambao serikali iliwaelekeza wajaze kama watajidhamini binafsi ili wapewe mikopo. Baada ya kujaza fomu hizi serikali iliwapatia mikopo awamu ya kwanza wakaanza masomo na baadaye kidogo serikali ikawajulisha kuwa haitaendelea tena kuwadhamini. Hawa wako wachache hususani katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) suala lao ni la haraka wanapaswa kusaidiwa mapema ili wasishindwe kufanya mitihani yao. Kurugenzi ya Vijana itafuatilia suala lao katika mwezi Disemba.

  2. Kundi la pili ni la wale wa madaraja mengine ambao mwanzoni walikidhi vigezo vyote vya kujiunga na vyuo na kupata mikopo lakini baada ya serikali kubadilisha utaratibu wameshindwa kujidhamini na kuendelea na masomo. Kundi hili ni kubwa na linajumuisha wanafunzi katika vyuo mbalimbali bara na visiwani. Kwa mujibu wa tamko la vijana wa CHADEMA suluhisho la msingi ni kwa CHADEMA na wadau wengine kuishinikiza serikali ili iongeze bajeti ya mikopo ya elimu ya juu kwa upande mmoja na kubadili vigezo vya utoaji mikopo na kurudhisha vigezo ya awali kwa upande mwingine. Kurugenzi ya Vijana wa CHADEMA itaanza kufuatilia suala hili kuanzia Mwezi Januari 2007 ili kuhakikisha bajeti ijayo ya serikali inawezesha wanafunzi hawa kupata mikopo kwa ajili ya masomo. Hivyo, kutokana na uwingi wa walalamikaji kurugenzi ya vijana ya CHADEMA inawaomba katika mwezi huu wa Disemba 2006 wote walioathirika na maamuzi hayo ya serikali wawasilishe malalamiko yao ili yatumike kama msingi wa kujenga ama ‚nguvu ya umma’ au ya kisheria ya kushughulikia tatizo hilo.

Kwa mantiki hiyo wanafunzi waliokosa mikopo kutokana na uamuzi huo wa serikali waliombwa na tunatumia fursa hii kuwaomba tena kuwasilisha malalamiko yao makao makuu ya chama katika kurugenzi ya vijana, wanaweza kuwasilisha malalamiko kwa gharama zao kwa kati ya njia zifuatazo:

  1. Kwa kufika ofisini (Kinondoni Manyanya, Mtaa wa Ufipa)
  2. Kwa njia ya simu (022-2668866, 0754-694553, 0754-471751)
  3. Anauni pepe (vijana@chadema.net)
  4. Tovuti (www.chadema.net)
  5. Ama kutuma barua kwa posta (S.L.P 31191, Dar es salaam)

Aidha tunachukua fursa hii kuwapongeza wanavyuo ambao wameitikia mwito huu mpaka sasa, tukumbuke wosia wa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwamba haki hailetwi kwenye kisahani, inatafutwa.

CHADEMA: Mabadiliko ya Kweli!, Uhuru wa Kweli!

Imetolewa: 23/11/2006

John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana


lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl