lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
banner
Ijue CHADEMA
»Utangulizi
»Falsafa ya Chama
»Itikadi ya Chama
»Uanachama
»Viongozi wetu
»Historia ya CHADEMA
»Jiunge CHADEMA
b.part
Mengineyo
»Habari Mpya
»Makala mbalimbali
»Midahalo
»Blogu za wanachama
»Picha za matukio
»Maoni Yenu
b.part
Barua Pepe
jina la mtumiaji:
neno-siri
rt.bt.spc
bt.part2

Uanachama katika CHADEMA

Mtu yeyote anaweza kuwa mwanachama wa CHADEMA iwapo atakidhi sifa kama ilivyoainishwa katika katiba: sifa za kuwa mwanachama ni kama ifuatavyo:
  1. Awe raia wa Tanzania.
  2. Awe na umri usiopungua miaka 18.
  3. Awe na akili timamu.
  4. Awe anakubaliana na sera, katiba, kanuni na maadili ya chama.
  5. Awe anakubaliana na itikadi na falsafa ya chama.
  6. Asiwe mwanachama wa chama kingine cha siasa baada ya kujiunga na CHADEMA.
  7. Vijana wenye umri kati ya miaka 12 hadi 17 ambao wana mapenzi na chama watapewa kadi maalum kutoka katika baraza la vijana.
  8. Kuwa ndani ya chama kunampa mtu uwezo pia wa kujiunga na mabaraza ya chama (baraza la vijana, wazee na wanawake).

Majukumu, wajibu na haki za wanachama wa CHADEMA.

Kila mwanachama ana haki ya:
  1. Kuchagua viongozi wa chama wa ngazi anayohusika kwa mujibu wa katiba.
  2. Kuchaguliwa kuongoza na kuwakilisha chama katika ngazi yoyote kwa kuzingatia masharti yaliyowekwa ya sifa za uongozi.
  3. Kushiriki vikao vya chama vinavyomhusu na kutoa mawazo yake kwa uhuru kwa kuzingatia taratibu za vikao.
  4. Kujitetea, kusikilizwa na kuKata rufaa anaposhitakiwa ama kuchukuliwa hatua za kinidhamu kichama.

Kila mwanachama ana wajibu wa:
  1. Kushiriki kikamilifu katika vikao vinavyomhusu na katika shughuli nyingine za chama kadri atakavyotakiwa.
  2. Kuchangia gharama za uendeshaji chama kwa njia ya ada ya Uanachama ya kila mwaka na kwa michango mingineyo inayoamriwa na vikao vya chama.
  3. Kutetea na kueneza Itikadi, falsafa na madhumuni ya chama ndani ya jamii anamoishi.
  4. Kushirikiana na wanachama na viongozi wengine wote katika kutekeleza sera na mipango ya chama.
  5. Kuwa tayari kupambana na namna yoyote ya uonevu, ukandamizaji, udhalilishaji na ubaguzi.
  6. Kuwa chachu ya maendeleo popote pale alipo.

dokezo:

Unaweza kujaza fomu hapa kisha ukapata kadi ya Uanachama!
Usisubiri, kuwa Mwanachama leo!
lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl