lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
Seza Zingine
Sera ya Afya
Sera ya Ajira
Sera ya Ardhi
Sera ya Biashara
Sera ya Demokrasia
Sera ya Elimu
Sera ya Kilimo
Sera ya Madini
Sera ya Maji
Sera ya Mazingira
Sera ya Michezo
Sera ya Mifugo
Sera ya Miundombinu
Sera ya Rasilimali
Sera ya Uchumi
Sera ya Ulinzi
Sera ya Utamaduni
Sera ya Utawala
Sera ya Utawala Bora
Sera ya Vijana
Sera ya Viwanda
b.part
Barua Pepe
jina la mtumiaji:
neno-siri
rt.bt.spc
bt.part2
Sera ya Uchumi

lf.bevel rt.bevel
Sekta ya Kodi
Kodi ni nyingi na za kificho. Serikali ya CHADEMA itafanyaje kuboresha mfumo wetu wa kodi?
lf.bevel rt.bevel

Uchumi wa Takwimu, Umasikini kibao, kwa nini?

  1. Uchumi umekuwa kwa matajiri na wageni. Kwa Watanzania walio wengi uchumi unazidi kudorora.
  2. Bei za bidhaa zinapanda kifalaki kila mwaka-Petroli ilikuwa shilingi 450 mwaka 1995, mwaka 2005 imefikia shilingi 1,100 na inazidi kupanda.
  3. Pesa imepotea mifukoni mwa wananchi wakati maisha yanazidi kuwa ghali.
  4. Sekta zinazokuwa kwa kasi ni madini, utalii na utoaji huduma ambazo zinamilikiwa kwa kiasi kikubwa na wageni - ugenishaji
  5. Umaskini umezidi kuongezeka - asilimia 60 ya Watanzania wote maisha yao ya kiuchumi ni duni kuliko 1992.
  6. Kati ya Watanzania mia moja ni arobaini na nne tu wana uhakika wa mlo MMOJA kwa siku.
  7. Tofauti kati ya wenye kipato na wasicho nacho inazidi kuwa kubwa.
  8. Tumegeuzwa soko (dampo) la bidhaa hafifu za nje.
  9. Gharama ya kulipia mikopo holela kutoka nje inazidi kuwa kubwa – mikopo ya miradi isiyotekelezeka na miradi hewa iliyotafunwa na wajanja.
  10. Serikali ya awamu ya tatu imesambaratisha thamani ya shilingi ya Tanzania - Shilingi 575 iliweza kununua dola moja mwaka 1995, mwaka huu utahitaji takriban shilingi 1,200.
  11. Uchumi wa nchi unashikiliwa na wanaume wachache na wanawake kuwekwa pembezoni kabisa katika umiliki wa uchumi. Walio masikini zaidi katika Tanzania ni wanawake na hasa wa vijijini.
  12. Mchango wa wanawake wa Tanzania katika kukuza uchumi hauthaminishwi, mfano mchango wa kukaa nyumbani na kulea watoto na kutunza nyumba haupewi thamani ya kifedha katika kukokotoa pato la Taifa.
  13. Uchumi unakua mjini ilhali vijijini unazidi kuzorota. Umasikini wa Tanzania una sura ya Kijiji.
  14. Masharti ya mikopo ya mabenki kwa wanawake ni magumu sana.
  15. Serikali imepuuza kilimo ilihali kinachangia asilimia 44% ya pato la Taifa na 80% ya ajira.
  16. Bajeti zinapendelea walionacho - mfano kufutiwa kodi mafuta ya ndege

CHADEMA itafanyaje WATANZANIA WOTE wafaidi matunda ya kukua kwa uchumi?

  1. Tutatunga na kutekeleza sera za uchumi zinazojali watu maskini (pro-poor economic policies).
  2. Tutahakikisha kuwa tunatoa kipaumbele kwa sekta zinazotengeneza ajira kwa watu wengi mfano kilimo.
  3. Tutatunga na kutekeleza sera ambazo zitaweka mazingira bora kwa Watanzania kufanya biashara na hasa biashara ya kimataifa ili kuongeza ajira na kukuza pato la mtu binafsi na pato la Taifa.
  4. Tutaweka mazingira ya Watanzania kumiliki uchumi wao wenyewe na kuwezesha wanawake kushiriki katika kumiliki uchumi wa nchi yao kwa kuwapa fursa zaidi na mafunzo bora na ya kisasa zaidi.
  5. Tutafuta misamaha ya kodi kwa wawekezaji wageni isipokuwa kwenye sekta ya kilimo na mifugo tu.
  6. Tutaimarisha benki ya rasilimali (Tanzania Investment Bank) ili itoe mikopo kwa Watanzania kwa masharti na gharama nafuu na hasa kuzingatia umuhimu wa mikopo kwa wanawake ili masharti yalingane na uwezo wa wanawake na vijana katika kulipa.
  7. Tutajenga miundo mbinu ya barabara ili kurahisisha kukua kwa uchumi kwa mikoa ya pembezoni. Barabara za kuunganisha mikoa ya Rukwa, Mbeya, Tabora, Shinyanga na Kigoma zitajengwa ili kuunganisha mikoa hii na nchi nzima.
  8. Tutaelekeza halmashauri za wilaya kuanzisha benki za jumuiya pamoja vikundi vya kuweka na kukopa.
  9. Mikopo ya nje itakuwa ni kwa ruhusa ya Bunge ili kuthibiti ukopaji usio wa lazima.
  10. Kuanzisha mfumo utakaomwezesha kila Mtanzania kumiliki mali bila mizengwe- ikiwamo mali za vipaji.
  11. Sheria zote za umiliki wa mali ikiwemo ardhi zitapitiwa kwa lengo la kuhakikisha haki ya kumiliki mali hasa kwa wanawake na vijana inalindwa kisheria na kufuta sheria au kanuni zote za ubaguzi katika kumiliki mali.
  12. Tutathamini mchango wa Wanawake katika kukuza uchumi kwa kutoa vipaumbele kwa wanawake katika elimu na nafasi za kazi kama ujira wa kazi wasiolipwa ya kulea Taifa.
lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl