lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
banner
Seza Zingine
Sera ya Afya
Sera ya Ajira
Sera ya Ardhi
Sera ya Biashara
Sera ya Demokrasia
Sera ya Elimu
Sera ya Kilimo
Sera ya Madini
Sera ya Maji
Sera ya Mazingira
Sera ya Michezo
Sera ya Mifugo
Sera ya Miundombinu
Sera ya Rasilimali
Sera ya Uchumi
Sera ya Ulinzi
Sera ya Utamaduni
Sera ya Utawala
Sera ya Utawala Bora
Sera ya Vijana
Sera ya Viwanda
b.part
Mengineyo
»Habari Mpya
»Makala mbalimbali
»Midahalo
»Blogu za wanachama
»Picha za matukio
»Maoni Yenu
b.part

Sera ya Michezo

Hali ikoje?

  1. Kuna ukosefu wa viwanja vya michezo - Viwanja vya michezo vimetelekezwa na viko katika hali mbaya.
  2. Viwango vya michezo ni duni na wenye vipaji hawaendelezwi.
  3. Tanzania tumepotea katika ramani michezo duniani - Hakuna mchezo wowote kama nchi tunaojivunia kufanya vizuri.
  4. Michezo mingi imeachwa chini ya viongozi matapeli – wananchi wamebakia kuwa washabiki.
  5. Mashindano ya mashule yamefutwa na michezo imeondolewa katika ratiba za kawaida za shule.

Serikali ya CHADEMA itafanyaje?

  1. Tutaziagiza halmashauri kuweka mazingira ya kujengwa vituo vya michezo vyenye viwanja katika kila wilaya.
  2. Tuboresha muundo wa Baraza la Michezo (BMT) nchini ili kuwa na uwakilishi mpaka katika ngazi ya wilaya.
  3. Tutarejesha viwanja vilivyotaifishwa na kuviweka chini uangalizi wa BMT kwa kusudio la kuweza kuviendeleza.
  4. Vilabu vya mpira wa mguu vitatakiwa kuendeshwa kibiashara.
  5. Itahamasisha uwekezaji katika vituo vya vijana (yoso) wenye vipaji, hususan kandanda na riadha ili kuwaendeleza mpaka kufikia kiwango cha kuliwakilisha taifa letu kimaatifa.
  6. Tutarejesha na kuhimiza michezo katika mashule na vyuo – michezo itaingizwa katika ratiba na mitaala, mashindano ya shule na vyuo yatarejeshwa na kupewa mkazo.
  7. Itaanzisha siku ya michezo nchini itakayofanyika kitaifa na katika ngazi ya wilaya.
lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl