lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
banner
Seza Zingine
Sera ya Afya
Sera ya Ajira
Sera ya Ardhi
Sera ya Biashara
Sera ya Demokrasia
Sera ya Elimu
Sera ya Kilimo
Sera ya Madini
Sera ya Maji
Sera ya Mazingira
Sera ya Michezo
Sera ya Mifugo
Sera ya Miundombinu
Sera ya Rasilimali
Sera ya Uchumi
Sera ya Ulinzi
Sera ya Utamaduni
Sera ya Utawala
Sera ya Utawala Bora
Sera ya Vijana
Sera ya Viwanda
b.part
Mengineyo
»Habari Mpya
»Makala mbalimbali
»Midahalo
»Blogu za wanachama
»Picha za matukio
»Maoni Yenu
b.part

WATANZANIA TUKUBALI KUWA KUNAHITAJIKA KUWEPO MABADILIKO KATIKA MFUMO NA MUUNDO WA TAWALA ZA MIKOA!

TUONDOKANE NA
“MAZOEA TU”

lf.bevel rt.bevel
Mheshimiwa Sylvester K. Masinde anafafanua Sera ya Utawala wa Majimbo na kutoa mtazamo wake juu ya Sera hii baada ya kufuatilia kwa makini malengo ya Chama na maoni ya Watanzania.
lf.bevel rt.bevel

Miaka 44 sasa baada ya nchi yetu kuwa huru, hatuna haja wala ulazima wa kuendelea kukumbatia mfumo na muundo wa Tawala za Mikoa tuliorithi kutoka kwa wakoloni. Ni muundo wa kuwa na mamlaka (Rulership) juu ya watu kama ilivyokuwa wakati wa Tanganyika ya Ukoloni. Utawala wetu sasa unatakiwa kuwa wa kuongoza watu (Leadership).

Nyakati za mfumo wa siasa za Chama Kimoja na Dhana ya Chama kushika hatamu za utawala wa nchi, muundo wa tawala za mikoa uliendelezwa kwa maslahi ya kiitikiadi. Wakati huu wa zama na udikiteta wa kisiasa, muundo huu ulitumika kuunganisha mamlaka na madaraka ya utawala na shughuli za chama. Kwa ajili hii chama kiliweza kudhibiti Nguvu ya Umma kwa kuwanyima watu fursa ya kupata na kujua maoni na mitazamo tofauti ya kisiasa. Chama kilichukua nafasi ya kuwa kiunganishi cha jamii ya Watanzania badala ya serikali. Serikali ilifanywa chombo cha kutumiwa na chama badala ya kuwa chombo cha watu, raia huru wa nchi.

Leo CCM na Serikali zake vinatetea na kuukumbatia mfumo na muundo huu kwa maslahi ya kisiasa tu na siyo kwa sababu ya ufanisi wa kuwaendeleza wananchi kimaisha. Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya kama watu binafsi hawawezi kuwaendeleza watu zaidi ya kuwatawala.

Serikali za Mitaa na siyo Tawala za Mikoa ndilo jibu sahihi katika kuleta ufanisi wa kuwaendeleza Watanzania. Wakuu wa Mkoa na Wakuu wa Wilaya wako na wanajishughulisha zaidi na maslahi ya kisiasa ya chama chao na ndio maana uteuzi wao ni wa kiitikadi zaidi ya taaluma, ujuzi na uzoefu wa maswala ya utawala. Ni vema ikumbukwe kuwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya ndiyo nguzo za kuwezesha CCM kushinda uchaguzi. CCM na Serikali zake hawako tayari kuzifanya nyadhifa hizi kuwa za kitendaji katika utumishi Serikalini. Hii ni kwa sababu wanaogopa kupoteza nguvu hii kubwa ya kisiasa.
  Maneno 'JIMBO' na 'MKOA'...

Toa Maoni yako hapa   

lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl