|
|
|
|
|
|
Sera ya Maji
Hali ikoje?
- Tanzania ni nchi ya maji – imezungukwa na maziwa makuu, bahari, mito, chemchem na maji ya mvua.
- Asilimia 95% ya wananchi hawapati maji safi, salama na kwa uhakika.
- Wananchi hawa, hususan wanawake, hutumia nguvu na muda wao mwingi kuyatafuta maji
- Kumekuwa na ahadi hewa za upatikanaji wa maji – Kwa miaka zaidi ya 30 wananchi wote wameahidiwa maji bila mafanikio!
Serikali ya CHADEMA itafanya nini?
- Itawekeza katika uvunaji wa maji ya mito, maziwa, chemchem na mvua.
- Mamlaka ya Usambazaji ya maji itakuwa chini ya halmashauri za manispaa, miji na wilaya
- Itawezesha vijiji kutunza vyanzo vya maji ili visiharibiwe.
- Upatikanaji wa Maji kwa Wananchi itakuwa ni kipaumbele muhimu cha serikali ya CHADEMA.
- Itaingiza kwenye mitaala kuanzia shule ya msingi hadi sekondari dhana ya utumiaji na utunzaji wa maji.
- Tutaboresha na kukarabati miundombinu ya maji iliyopo ili kuzuia upoteaji wa maji.
- Tutahakikisha kila Mtanzania anapata maji safi na salama katika kipindi kifupi iwezekanavyo.
- Hatutabinafsisha sekta ya Maji na makampuni yote yaliyobinafsishwa yatarejeshwa chini ya mamlaka za Maji katika Halmashauri za Wilaya. CHADEMA haitaweka MAJI chini ya mikono ya Makampuni ya kigeni, ni hatari kwa usalama wa Nchi.
|
|
 |
 |
|
 |
 |
|