lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
Seza Zingine
Sera ya Afya
Sera ya Ajira
Sera ya Ardhi
Sera ya Biashara
Sera ya Demokrasia
Sera ya Elimu
Sera ya Kilimo
Sera ya Madini
Sera ya Maji
Sera ya Mazingira
Sera ya Michezo
Sera ya Mifugo
Sera ya Miundombinu
Sera ya Rasilimali
Sera ya Uchumi
Sera ya Ulinzi
Sera ya Utamaduni
Sera ya Utawala
Sera ya Utawala Bora
Sera ya Vijana
Sera ya Viwanda
b.part
Mengineyo
»Habari Mpya
»Makala mbalimbali
»Midahalo
»Blogu za wanachama
»Picha za matukio
»Maoni Yenu
b.part

Sera ya Madini

Hali ikoje katika utajiri wetu wa madini?

  1. Tanzania imebarikiwa kuwa na madini ya aina mbalimbali.
  2. Katika kila shilingi mia inayopatikana kwenye madini Tanzania inapata shilingi tatu tu!
  3. Mapato yanoyopatikana kutokana na madini bado hayamfikii wala kumnufaisha Mtanzania
  4. Mikataba ya uchimbaji wa madini imetawaliwa na usiri mkubwa na inanuka rushwa.
  5. Vijana wa Kitanzania wafanyao kazi kwenye migodi ya wageni ni sawa na manamba na watumwa ndani ya nchi yao.
  6. Wachimbaji wadogowadogo wanafukuzwa na kunyimwa fursa ya kumiliki migodi.

Serikali ya CHADEMA itafanya nini Tanzania ifaidi utajiri wa Madini?

  1. Si chini ya asilimia thelathini ya mapato yatokanayo na madini yatabaki nchini.
  2. Mikataba yote ya uchimbaji itapitiwa upya na kuwekwa wazi kwa wananchi.
  3. Kuwekwa sheria na utaratibu zitakazowalinda Watanzania wanaojishughulisha na uchimbaji wa madini hususan wachimbaji wadogowadogo.
  4. Kugawa maeneo ya uchimbaji kulingana na mahitaji halisi ya wananchi ili kuzuia migogoro iliyopo hivi sasa.
  5. Kutoa mikopo na ushauri wa kitaalamu kwa wachimbaji wadogo na kujihusisha na utafutaji wa teknolojia ya kisasa ya uchimbaji.
  6. Wanawake wafanyao biashara za madini watajengewa uwezo zaidi ili kulinda biashara zao dhidi ya utapeli na pia kuwawezesha kujiendeleza zaidi na kupata masoko ya biashara zao.
  7. Wachimbaji wadogo wadogo wa Kitanzania watawezeshwa kumiliki maeneo ya uchimbaji kama mbinu ya kuzalisha ajira kutokana na sekta ya madini.
  8. Mamlaka za serikali za Mitaa ambayo migodi ya madini au visima vya mafuta vipo zitashiriki kwa kiasi kikubwa katika kuandaa mikataba ya uchimbaji wa madini na mafuta.
  9. Mapato yanayotokana na madini yatatumika katika kuwekeza katika elimu kwa vijana wa Kitanzania.
  10. Usafishaji wa madini angalau kwa hatua za awali ni lazima ufanyike Tanzania ili kutoa ajira na pia kuchangia ukuaji wa uchumi na pato la wananchi.
  11. Tenda zote za ugavi kwa makampuni ya madini kwa bidhaa zinazoweza kupatikana Tanzania zitatolewa kwa Watanzania tu. Makampuni ya kigeni hayataruhusiwa kufanya ugamvi wa vitu kama vyakula, kwa mfano!
lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl