|
|
|
|
|
|
Sera ya Uchumi - Sekta ya Kodi
Kodi nyingi na za kificho, hali gani hii?
- Kodi nyingi ni za kificho au kinyemela – mfano sukari yaweza kuwa na bei ndogo sana iwapo kodi kadhaa katika bidhaa zitaondolewa au kupunguzwa.
- Viwango vya Kodi anazotozwa mwananchi ni kubwa mno.
- Mfumo mbovu wa kodi unaosababisha mianya mingi ya ukwepaji kodi.
- Wageni wanapewa misamaha ya kodi kiholela na kiupendeleo.
- Kiwango cha VAT kipo juu sana na mzigo kwa wananchi wengi hasa VAT katika vifaa muhimu vya afya na hasa kwa akina mama.
Serikali ya CHADEMA itafanya yafuatayo kuboresha mfumo wetu wa kodi.
- Itaweka wazi kodi zote zinazotozwa – mwananchi lazima ajue kodi anayotozwa.
- Tutapunguza VAT ili iendana na viwango vya nchi nyingine za Afrika Mashariki.
- Tutaziba mianya ya ukwepaji kodi na kutoa misamaha pale tu itakapobidi na lazima iidhinishwe na bunge.
- Tutapanua wigo wa kukusanya kodi.
- Tutafuta kodi katika bidhaa zote muhimu kwa akina mama wajawazito na watoto wao na pia vifaa vya elimu na vyakula vinavyozalishwa ndani ya nchi.
|
|
 |
 |
|
 |
 |
|