|
|
|
|
|
|
Sera ya Utawala Bora
Hali ikoje?
- Rushwa na upendeleo vimekithiri katika nyanja zote - Rushwa sasa imekuwa utamaduni.
- Shughuli za vyama vya siasa zinafanywa na vyombo vya dola.
- Matumizi ya anasa ya viongozi ilhali wananchi wamezamishwa kwenye umaskini uliokithiri.
- Viongozi kutowajibika mbele ya wananchi.
- Wizi wa mali ya umma, ubinafsishaji holela na ufisadi.
- Uuzaji wa nyumba za Serikali kwa viongozi kiupendeleo.
- Mamlaka ya Umma imeporwa na tabaka la watu wachache.
- Ukosefu wa maadili ya Taifa.
- Viongozi wabovu wasiokuwa na dira.
- Viongozi wanakula njama na wageni kuhujumu rasilimali zetu.
- Hakuna morali.
- Ubinafsi umetawala.
- Uzembe umekithiri.
- Viongozi wasiojali nchi na watu wake.
- Mwizi ni yule anayekamatwa, asiyekamatwa ruksa.
Serikali ya CHADEMA itafanyaje?
- Itafuta PCB na kuunda upya idara ya kupambana na rushwa chini ya idara ya Mkurugenzi wa makosa ya jinai.
- Idara ya Usalama wa Taifa itafanyiwa marekebisho makubwa ili ilinde maslahi ya nchi na sio ya wakubwa wachache.
- Tutaita Mkutano wa Katiba ndani ya mwaka mmoja wa utawala wa CHADEMA.
- Katiba kuwa na kipengele kitakacho ruhusu wananchi kuwawajibisha madiwani, wabunge na wawakilishi “recalling clause”.
- Itapiga marufuku uuzaji wa nyumba za Serikali na kurejesha zilizokwisha uzwa kiupendeleo.
- Matumizi yote ya gharama kubwa bila stahili kusimamishwa mara moja.
- Tutakomesha rushwa na atakayetoa au kupokea rushwa atahukumiwa adhabu kali.
- Upendeleo utapigwa vita.
- Viongozi wa CHADEMA watajali nchi na watu wake.
- Tutahamasisha maadili ya Taifa.
|
|
 |
 |
|
 |
 |
|