lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
banner
Seza Zingine
Sera ya Afya
Sera ya Ajira
Sera ya Ardhi
Sera ya Biashara
Sera ya Demokrasia
Sera ya Elimu
Sera ya Kilimo
Sera ya Madini
Sera ya Maji
Sera ya Mazingira
Sera ya Michezo
Sera ya Mifugo
Sera ya Miundombinu
Sera ya Rasilimali
Sera ya Uchumi
Sera ya Ulinzi
Sera ya Utamaduni
Sera ya Utawala
Sera ya Utawala Bora
Sera ya Vijana
Sera ya Viwanda
b.part
Mengineyo
»Habari Mpya
»Makala mbalimbali
»Midahalo
»Blogu za wanachama
»Picha za matukio
»Maoni Yenu
b.part
Barua Pepe
jina la mtumiaji:
neno-siri
rt.bt.spc
bt.part2

Sera ya Ardhi

Hali katika sekta ya ardhi ikoje?

  1. Watanzania wote ni wapangaji katika ardhi yao – sheria za ardhi hazitoi mamlaka ya kumiliki ardhi kama mtu binafsi ama vikundi.
  2. Sheria hizi zinampa mgeni mamlaka makubwa juu ya ardhi kuliko mwananchi.
  3. Mfumo dume umetawala katika kumiliki ardhi – wanawake na vijana hawajapata fursa ya kumiliki au ‘kukodisha’ ardhi.
  4. Wageni wanauziwa ardhi kama khanga.
  5. Mfumo mbaya wa ugawaji na umiliki wa ardhi pamoja na rushwa imesababisha utitiri wa migogoro ya ardhi.
  6. Wananchi wanaporwa ardhi zao kwa visingizio vya kuendeleza maslahi ya Taifa.
  7. Utaratibu uliyopo wa milki ya ardhi hautoi uhakika kwa wanyonge na maskini kumiliki ardhi yao.
  8. Kuna urasimu mkubwa unaoshawishi rushwa katika kutoa haki za kumiliki ardhi.

Serikali ya CHADEMA itafanya nini ili kumilikisha Ardhi kwa Watanzania?

  1. Tutarejesha mamlaka ya asili ya wananchi kumiliki ardhi.
  2. Hatima ya ardhi ya kijiji itaachwa mikononi wa mamlaka ya Serikali ya kijiji.
  3. Rais hatokuwa na mamlaka ya kuhamisha ardhi kutoka kundi moja hadi jingine.
  4. Wageni watapatiwa ardhi kwa masharti yafuatayo - kutoimiliki, kutoiuza, kutoipora rasilimali na kutoitumia kwa namna itakayoharibu mazingira.
  5. Umilikaji wa ardhi kwa wanawake haitakuwa suala la mjadala tena. Mfumo dume wa kumiliki ardhi utatokomezwa na kufanywa historia.
  6. Utawekwa utaratibu wa kisheria utakaowawezesha wanawake kumiliki ardhi bila bughudha wala hofu ya kuporwa.
  7. Itaimarisha mabaraza ya ardhi ya vijiji na wilaya na kuhakikisha yanatoa haki kwa wananchi.
  8. Utawekwa utaratibu wa serikali kuwawekea mawakili wananchi wasio na uwezo katika mashauri ya ardhi katika ngazi ya mahakama kuu na mahakama ya rufaa.
  9. Tutatunga na kusimamia sheria zitakazo shughulikia uvamizi na ujenzi holela.
  10. Itatoa maelekezo kwa halmashauri kuendesha mipango ya ujenzi wa nyumba za bei nafuu za wananchi.
  11. Itarejesha nyumba zote za serikali zilizouzwa kwa upendeleo.
  12. Tutaunda baraza la Taifa la ardhi litakalowajibika kwa Bunge.
  13. Mahitaji ya ardhi kwa jamii za vijijini yatapewa kipaumbele kuliko mahitaji ya wengine.
  14. Tutalinda ardhi za vijiji dhini ya umegaji mkubwa ili kuepuka matatizo ya kijamii.
  15. Itahakikisha vijiji vinakuwa ni vitengo vinavyojiendesha na kujitawala vyenyewe na tutawezesha wanavijiji kushiriki kikamilifu kuendesha masuala yote ya ardhi kupitia vikao vya mkutano mkuu wa kijiji.
  16. Tutahakikisha wanyonge na maskini wanamiliki ardhi ya nchi yao bila ubaguzi wa jinsi wala umri.
  17. Madaraka ya kutoa haki za kumiliki ardhi yatakuwa chini ya mikoa (majimbo).
lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl