lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
banner
Seza Zingine
Sera ya Afya
Sera ya Ajira
Sera ya Ardhi
Sera ya Biashara
Sera ya Demokrasia
Sera ya Elimu
Sera ya Kilimo
Sera ya Madini
Sera ya Maji
Sera ya Mazingira
Sera ya Michezo
Sera ya Mifugo
Sera ya Miundombinu
Sera ya Rasilimali
Sera ya Uchumi
Sera ya Ulinzi
Sera ya Utamaduni
Sera ya Utawala
Sera ya Utawala Bora
Sera ya Vijana
Sera ya Viwanda
b.part
Mengineyo
»Habari Mpya
»Makala mbalimbali
»Midahalo
»Blogu za wanachama
»Picha za matukio
»Maoni Yenu
b.part

Sera ya Ajira

Hakuna Ajira, Watanzania tukale wapi?

  1. Watanzania wengi wanaishi kwa kubahatisha – Asilimia 28 ya vijana wanaoishi mjini hawana ajira.
  2. Wafanyakazi wanakandamizwa – mifumo ya ajira ya soko holela inawaminya.
  3. Wafanyakazi wanazidi kupunguzwa bila maslahi yao kuzingatiwa.
  4. Wafanyakazi wa Kitanzania wanalipwa mishahara midogo kuliko wa kigeni kwa kazi ileile.
  5. Mishahara na mazingira ya kazi bado ni duni.
  6. Hakuna juhudi mahususi za kutengeneza ajira kwa Watanzania.
  7. Hakuna takwimu sahihi za masuala ya ajira.
  8. Wawekezaji wanaajiri wageni hata kwa kazi ambazo kuna Watanzania wengi wanaweza kuzifanya.

Serikali ya CHADEMA itatengezena ajiri nyingi na hasa kwa vijana, kivipi?

  1. Tutaweka kipaumbele kuweka mazingira ya kuongezeka fursa za ajira
  2. Tutatengeneza ajira milioni moja ndani ya mwaka mmoja wa utawala wa CHADEMA kwa kuimarisha sekta za ujenzi, madini, kilimo, utalii na huduma za jamii (walimu, madaktari na manesi)
  3. Tutakomesha ubaguzi wa ajira kwa watu wenye ulemavu na tutatoa motisha kwa mashirika yatakayoajiri watu wenye ulemavu na kuwaendeleza kitaaluma.
  4. Tutaweka sheria kali kulinda haki za ajira kwa wanawake na mashirika na makampuni yatakayo ajiri wanawake zaidi yatapewa motisha katika kodi na hata zabuni za serikali.
  5. Tutaweka mifumo yenye kulinda haki na maslahi ya wafanyakazi.
  6. Vyama vya wafanyakazi vitalindwa kisheria na kupewa nafasi kubwa katika kulinda maslahi ya wafanyakazi.
  7. Vyama vya wafanyakazi vitakuwa huru kweli kweli na itakuwa ni marufuku kwa serikali kuingilia utendaji wa vyama vya wafanya kazi.
  8. Tutasimamia wazawa na wageni wenye ujuzi unaolingana kulipwa sawasawa.
  9. Tutatunga sheria itakayohakikisha kuwa Wageni wataajiriwa pale tu hakuna mtanzania anayemudu kazi husika na kwamba Wawekezaji watafanya juhudi kufundisha Watanzania kumudu kazi hizo siku za mbeleni.
  10. Tutatoa msamaha wa kodi wa kiasi kwa kila atakaye ajiri mhitimu wa chuo mara baada ya masomo.
  11. Tutaweka kipaumbele umuhimu wa kurekebisha ajira na maslahi ya wafanyakazi.
lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl