|
|
|
|
|
|
Sera ya Ajira
Hakuna Ajira, Watanzania tukale wapi?
- Watanzania wengi wanaishi kwa kubahatisha – Asilimia 28 ya vijana wanaoishi mjini hawana ajira.
- Wafanyakazi wanakandamizwa – mifumo ya ajira ya soko holela inawaminya.
- Wafanyakazi wanazidi kupunguzwa bila maslahi yao kuzingatiwa.
- Wafanyakazi wa Kitanzania wanalipwa mishahara midogo kuliko wa kigeni kwa kazi ileile.
- Mishahara na mazingira ya kazi bado ni duni.
- Hakuna juhudi mahususi za kutengeneza ajira kwa Watanzania.
- Hakuna takwimu sahihi za masuala ya ajira.
- Wawekezaji wanaajiri wageni hata kwa kazi ambazo kuna Watanzania wengi wanaweza kuzifanya.
Serikali ya CHADEMA itatengezena ajiri nyingi na hasa kwa vijana, kivipi?
- Tutaweka kipaumbele kuweka mazingira ya kuongezeka fursa za ajira
- Tutatengeneza ajira milioni moja ndani ya mwaka mmoja wa utawala wa CHADEMA kwa kuimarisha sekta za ujenzi, madini, kilimo, utalii na huduma za jamii (walimu, madaktari na manesi)
- Tutakomesha ubaguzi wa ajira kwa watu wenye ulemavu na tutatoa motisha kwa mashirika yatakayoajiri watu wenye ulemavu na kuwaendeleza kitaaluma.
- Tutaweka sheria kali kulinda haki za ajira kwa wanawake na mashirika na makampuni yatakayo ajiri wanawake zaidi yatapewa motisha katika kodi na hata zabuni za serikali.
- Tutaweka mifumo yenye kulinda haki na maslahi ya wafanyakazi.
- Vyama vya wafanyakazi vitalindwa kisheria na kupewa nafasi kubwa katika kulinda maslahi ya wafanyakazi.
- Vyama vya wafanyakazi vitakuwa huru kweli kweli na itakuwa ni marufuku kwa serikali kuingilia utendaji wa vyama vya wafanya kazi.
- Tutasimamia wazawa na wageni wenye ujuzi unaolingana kulipwa sawasawa.
- Tutatunga sheria itakayohakikisha kuwa Wageni wataajiriwa pale tu hakuna mtanzania anayemudu kazi husika na kwamba Wawekezaji watafanya juhudi kufundisha Watanzania kumudu kazi hizo siku za mbeleni.
- Tutatoa msamaha wa kodi wa kiasi kwa kila atakaye ajiri mhitimu wa chuo mara baada ya masomo.
- Tutaweka kipaumbele umuhimu wa kurekebisha ajira na maslahi ya wafanyakazi.
|
|
 |
 |
|
 |
 |
|