Kujenga uwezo wa wabunge na madiwani wa CHADEMA na kuwashirikisha kujenga taswira ya chama kwa michango yao bungeni, katika halmashauri za wilaya na kuboresha utumishi wao kwa wananchi.
- Pia kutawekwa mfumo wa wabunge kuchangia raslimali na muda kwa ajili ya shughuli za chama.
- Idara mpya ya mambo ya bunge na halmashauri itaanzishwa kuwasaidia wabunge na madiwani kutekeleza wajibu wao kwa wananchi na chama.
- Kanuni za kusimamia shughuli,mwenendo na maadili ya wabunge, madiwani na wenyeviti wa mitaa wa CHADEMA na halmashauri zinazoongozwa na CHADEMA zitaandaliwa ambazo pamoja na mambo mengine zitaelekeza nidhamu na wajibu wa pande zote.