lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
banner
Jihusishe
»Jiandae kwa 2009
»Jiandae kwa 2010
»Ilani ya 2005
»Utekelezaji wa Ilani
»Ripoti ya Uchaguzi
»Gharama za 2005
»Matokeo kura Urais
»Matokeo Ubunge
»Matokeo kimkoa
»Kura za Awali
»Gombea Ubunge
»Gombea Udiwani
b.part
Mengineyo
»Habari Mpya
»Matamko ya Chama
»Makala mbalimbali
»Midahalo
»Blogu za wanachama
»Picha za matukio
»Maoni Yenu
»Katuni
b.part


Mapendekezo ya Muungano wa Vyama

Mitazamo kadhaa ya Vyama vya Upinzani Kushirikiana

Pendekezo la Pili:

KUSHIRIKIANA KABLA YA UCHAGUZI

  1. Katika utaratibu huu vyama vyenye nia ya kushirikiana ili kuingia katika uchaguzi dhidi ya chama kinachotawala vinakubaliana kuweka mgombea mmoja kuwakilisha vyama vyote katika ngazi ama zote au kadhaa.
  2. Vyama vyaweza kushirikiana kwa kuweka mgombea mmoja katika ngazi ya urais na kugawana majimbo ya ubunge na kata za udiwani. Hapa chama kimojawapo kinatoa mgombea Urais na mgombea mwenza na pia majimbo na kata zinagawiwa miongoni mwa vyama vinavyoshirikiana.
  3. Vyama vyaweza kushirikiana katika ngazi ya majimbo na kata tu na kila chama kuweka mgombea wake wa urais. Hii inawezekana kwa kugawa nchi kwa mujibu wa halmashauri za wilaya/Miji/Manispaa/Jiji na kisha majimbo na kugawana miongoni mwao Wilaya hizo. Lengo la njia hii ni kuhakikisha kutawala Halmashauri na kushinda jimbo au majimbo yaliyopo katika Halmashauri husika.

Hatua za kuchukua:

  1. Viongozi wa vyama vyenye nia ya kushirikiana kukutana na kuunda kamati ya ufundi itakayoshauri njia mwafaka na taratibu za kushirikiana. Kamati ya ufundi itaandaa mkataba wa kisheria wa ushirikiano utakaoweka bayana muundo wa ushirikiano ikiwemo vikao vya kisheria vya kutatua migogoro itakayotokana na ushirikiano.


  2. Mkataba wa ushirikiano uridhiwe na vikao halali vya vyama husika.


  3. Mkataba uunde bodi ya uchaguzi ya vyama vinavyoshirikiana itakayokuwa na wajumbe sawa kutoka kila chama. Bodi hii iwe ni ya kitaifa na pia kila wilaya iwe na bodi hii.


  4. Kama ushirikiano unahusu wagombea wa nafasi za ubunge na udiwani, vikao vya utetuzi vya vyama vinavyoshirikiana vikae sambamba ili uteuzi ufanyike wakati mmoja. Hii itasaidia sana kuondoa migogoro miongoni mwa vyama.


  5. Mkataba uoneshe makubaliano ya majimbo na kuruhusu bodi za uchaguzi za wilaya kukubaliana kuachiana kata.


  6. Bodi iwe na nguvu kubwa ya kuamua wagombea na kupendekeza kwa vikao vya vyama ili kuhakikisha hakuna jimbo linalopita bila kupingwa.

Faida za Pendekezo la Pili

  1. Vyama vitapata uwakilishi mkubwa katika vyombo vya maamuzi - Mabaraza ya madiwani na Bungeni. Hili litatokea kwa sababu kura za wananchi hazitakuwa zimegawanyika kwa vyama tofauti.

  2. Kila kura ya Mtanzania itakuwa na heshima kwani itachangia sana kwa ushindi badala ya kupotea.

  3. Itasaidia vyama vidogo kupata uwakilishi bungeni na hatimae kupata ruzuku za kujiendesha.

  4. Iwapo mgombea mmojawapo wa upinzani atakuwa ameshinda kiti cha Urais ataweza kuunda serikali bila tatizo na kuteua Waziri Mkuu kutokana na wabunge wa upinzani waliopo ndani ya Bunge na pia kuteua mawaziri [Katiba ya Jamhuri ya Muungano ibara 51(1)(2) na 55(4)].

  5. Iwapo Rais atatoka katika chama kinachotawala, lakini wabunge wengi wanatoka vyama vya upinzani ushirikiano utaweza kuhalalisha serikali ya mseto (rejea ibara za katiba hapo juu).

  6. Inakwepa hasara zote za Pendekezo la kwanza

Hasara za Pendekezo la Pili

  1. Vyama kugeuka vya kikabila na kikanda na hivyo kuigawa nchi na kuhatarisha umoja na mshikamano wa nchi.

  2. Vyama vikubwa kutokukua kufuatia kufungiwa katika eneo moja la nchi.

  3. Kudumaa kwa demokrasia kwa kuminya wigo wa chaguo kwa wananchi.

  4. Uwezekano wa migogoro katika kuachiana majimbo. Wagombea kutoka vyama vilivyo katika ushirikiano kutokubaliana nani agombee kwa chama kipi.

  5. Kupoteza faida za pendekezo la kwanza na hasa ile ya kuunda chama kimoja cha upinzani chenye nguvu.

CHADEMA INASEMAJE?

Kwa kuzingatia uchambuzi wetu hapo juu tunapendekeza kama ifuatavyo:

  1. Kwa lengo la muda mrefu la kuimarisha demokrasia nchini Tanzania, vyama vikubaliane kuungana na kuwa chama kimoja kikubwa chenye nguvu. Hata hivyo, muda huu sio mwafaka kwani ni muda wa uchaguzi. Badala ya kutumia muda mwingi kuweka mikakati ya kuungana na kushiriki vikao vya kuungana ambavyo ni virefu sana, muda utumike kuweka mikakati ya ushindi katika uchaguzi Mkuu 2005. Hivyo mazungumzo ya kuunganisha vyama yafanyike mara baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2005.


  2. Kwa lengo la muda mfupi ambalo pia litapelekea vyama kuungana baada ya uchaguzi mkuu 2005, tunapendekeza vyama kushirikiana katika maeneo yafuatayo:


  1. Kugawana wilaya za uchaguzi ili kushinda na kuongoza halmashauri ya wilaya/Miji/Manispaa/Jiji. Huu ni ushirikiano katika ngazi za udiwani
  2. Kushirikiana katika kuachiana majimbo ili vyama vinavyoshirikiana kuweka mgombea mmoja dhidi ya mgombea wa chama tawala.
  3. Kila chama kiwe huru katika kuamua chenyewe juu ya nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
  1. Kwa kuwa muda umekwisha na uchaguzi Mkuu umekaribia tunapendekeza vikao vya ushirikiano vianze mara moja na viongozi wa vyama waunde vyombo muhimu vitatu:
  1. Kikao cha viongozi wa vyama (Summit of party leaders)
  2. Kamati ya ufundi ya ushirikiano (Technical Team of Parties)
  3. Bodi ya uchaguzi wa vyama vinavyoshirikiana (Parties' Electoral Board)
  1. Kamati ya ufundi ianze kutafuta fedha za kuwezesha mazungumzo na shughuli za ushirikiano.



Waasisi wa CHADEMA waliamini kwamba ni lazima nguvu za upinzani ziunganishwe ili kuwa na umoja wenye nguvu utakaoweza kupambana na CCM. Katika uchaguzi wa 1995 CHADEMA kilishirikiana na NCCR-Mageuzi baada ya vyama vingine kujiengua kwenye muungano wa wapinzani katika dakika za mwisho. Hata hivyo kambi hii iliweza kushika nafasi ya pili katika uchaguzi huo. Mwaka 2000 CHADEMA tena kilishirikiana na CUF baada ya vyama vingine kususia muungano. Vilevile kambi hii ilishika nafasi ya pili katika uchaguzi huo.

Watanzania wanataka vyama kuungana. Kuna ugumu sana kwa vyama kuungana na hata kushirikiana lakini uzoefu wetu unaonyesha kwamba hili linawezekana kama nia thabiti ipo. CHADEMA inasisitiza kwamba wananchi wapewe kile wanachokitaka. Tushirikiane ili kukidhoofisha chama tawala. Tutafaidika zaidi katika kushirikiana kuliko kutoshirikiana.

lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl