Oktoba 21, 2006 CHADEMA kilizindua mchakato wa kukusanya maoni ya vijana na wadau mbalimbali kuhusu Sera ya vijana ya CHADEMA ili kuifanya sera hii iendane na mahitaji ya sasa. Pia baadhi ya mambo yaliyopo katika sera ya sasa na kutoa maoni yako kwa lengo la kuboresha sera hii ya vijana. Mwisho wa kutoa maoni yako ni Januari 30 mwaka 2007:
- Tunaamini kwa vitendo kuwa kijana ni Taifa la Leo.
- Tutatoa fursa na kuwezesha kizazi kipya kuwa mstari wa mbele katika siasa, uchumi na sekta nyingine.
- Tutaweka mazingira ya kuundwa kwa Baraza Huru la Vijana Tanzania.
- Tutawezesha vijana wa kike na wa kiume kumiliki ardhi na rasilimali nyingine kwa kutenga maeneo kadhaa ya biashara kwa vijana tu.
- Tutaweka kipaumbele katika kukuza ajira kwa vijana kupitia vipaji vyao katika nyanja mbalimbali – tutazielekeza halmashauri kuanzisha mifuko ya ukuzaji vipaji vya Vijana.
- Tutaweka mazingira ya kuboreshwa kwa malezi ya Vijana katika familia na mashuleni ili kukabiliana na UKIMWI na madawa ya kulevya.
- Tutatoa leseni za bure na likizo ya kodi kwa Vijana wafanyabiashara ndogondogo na Vijana wanayojishughulisha na uzalishaji mali.
- Muziki wa kizazi kipya utapewa kipaumbele ili soko la muziki huu litakuzwa nje ya Tanzania.
Asante kwa kupitia maeneo ya sera ya vijana ya CHADEMA inayohitaji kuboreshwa. Tafadhali tuma maoni yako kwenye anuani pepe
vijana@chadema.net ama sanduku la posta 31191, Dar es salaam.Vijana: ”Nguvu ya mabadiliko”