CHADEMA ndicho chama pekee kikubwa cha upinzani ambacho kimekua na kinaendelea kukua kisiasa.
Aidha CHADEMA ndicho chama cha upinzani chenye nguvu kuliko vyote Tanzania bara. Ingawa CHADEMA ni chama cha upinzani lakini pia ni chama tawala wilaya za Karatu na Kigoma Ujiji. Wengi wanaamini CHADEMA ndicho chama mbadala kinachotegemewa kukiondoa CCM madarakani. Hivyo basi uamuzi wako wa kujiunga na chama ni uamuzi wa kina, sahihi na wenye busara.
Kama wewe ni Mtanzania mwenye umri usiopungua miaka 18, mwenye akili timamu na uliyesoma na kukubaliana na Sera, Falsafa,
Itikadi na Katiba yetu basi unazo sifa zote za kuwa mwanaCHADEMA.
Aidha hutatakiwa kuwa mwanachama wa chama kingine cha siasa unapojiunga nasi.
Ada ya kujiunga na chama ni shilingi mia tano na ya Uanachama kwa mwaka ni shilingi elfu moja. Hata hivyo mnakaribishwa na mnahimizwa kuchangia zaidi ya hicho kiwango kama uwezo unao. Tutawasiliana nawe kwa barua-pepe kukueleza utaratibu wa kulipia ada.
Fuata maelekezo yafuatayo hapo chini ili nawe uweze kujivunia kuwa mwanaCHADEMA leo!
Hatua ya Kwanza
Jaza fomu ya uanachama kwa uangalifu na kisha tutumie. Hakikisha unajaza sehemu zote zenye alama ya nyota nyekundu.
Fomu ya Uanachama