lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
banner
Ilani ya Chama
»Utangulizi
»Utekelezaji wa ilani
»Tanzania tuitakayo
»Mfumo wa Utawala
»Elimu Bora
»Afya kwa Wote
»Kilimo cha Kisasa
»Uchumi wenye Ajira
»Michezo
b.part
Habari za Uchaguzi
»Jiandae kwa 2010
»Jiandae kwa 2009
»Ilani ya 2005
»Ripoti ya Uchaguzi
»Gharama za 2005
»Matokeo kura Urais
»Matokeo Ubunge
»Matokeo kimkoa
»Kura za Awali
»Kampeni
b.part

Michezo imesahaulika

  1. CHADEMA inaamini kuwa michezo ni muhimu sana kwa afya lakini pia inaleta sifa kwa Taifa. Kwa mfano Tanzania ilifahamika sana mwaka 1976 wakati Filbert Bayi alipotwaa medali ya dhahabu; Klabu ya Simba ilipofikia fainali za klabu bingwa ya Afrika. CHADEMA tunajiuliza mafanikio hayo yameenda wapi? Kuna tatizo gani?


  2. Michezo itawapatia vijana ajira. CHADEMA itawaandaa watoto na vijana wadogo (yoso chini ya miaka 15) wenye vipaji vya kucheza kandanda na riadha kwa ajili ya kuunda kikosi cha taifa kwa kipindi cha zaidi ya miaka mitano. Vijana hawa watapangiwa vituo maalum, mafunzo maalum na chakula maalum. Pia kutakuwapo na chombo cha kandanda ambacho kitakuwa na mtandao nchi nzima na kushirikisha wanamichezo kuanzia ngazi ya vijiji na kujumuisha taasisi mbalimbali kama vile shule na makundi mbalimbali ya kijamii.

lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl