|
Hali ya Mkulima wa Tanzania Ikoje?
Hali Halisi ya Elimu Ikoje Tanzania?
-
Kilimo kimedorora. Licha ya Kilimo kuchangia asilima 44% ya pato la taifa Wananchi bado wanategemea jembe
la mkono na mvua zisizotabirika. Barabara hazifiki vijijini na hivyo mazao kuoza kabla ya kufika sokoni.
-
Soko linalonyonya wakulima. Wachuuzi wanadhulumu wakulima kwa kununua mazao kwa bei ya kutupa. Sera potofu
za soko holela zimeua kabisa motisha wa wakulima.
-
Tunauza mazao ghafi. Hakuna viwanda vidogo vya kuhifadhi na kusindika mazao ya kilimo.
Serikali ya CHADEMA itafanya nini?
- CHADEMA inatambua umuhimu wa kilimo katika maisha ya Mtanzania. Asilimia 80 ya Watanzania wanategemea kilimo.
Tanzania ilikuwa ni nchi pekee katika Afrika iliyokuwa na kiwango kikubwa cha uzalishaji wa mazao ya chakula katika miaka ya sitini
na sabini. Hivi sasa Tanzania inategemea misaada ya vyakula kutoka nje na uigizaji wa vyakula umekuwa ukiongozeka kila siku. Hii ni
aibu kwa nchi yetu iliyo na vyanzo vingi vya maji kama vile mito na maziwa. Kilimo cha umwagiliaji hakipo tena. Kwa CHADEMA, sekta
ya kilimo itaboreshwa na kilimo cha umwagiliaji kitapewa kipaumbele.
- Itafuta kodi. Kodi zote za pembejeo za kilimo ikiwemo VAT zitaondolewa. Itatoa ruzuku kwa wakulima wetu.
Itanzisha kilimo kikubwa cha umwagiliaji maji.
- Soko la mazao. Soko holela litadhibitiwa. Itaweka kipaumbele kujenga miundo mbinu ya barabara ziendazo
vijijini. Itatoa motisha na ushauri kwa wakulima kuzalisha mazao mbadala ya biashara kama maua, viungo na mboga.
- Usindikaji. Itatoa ruzuku na motisha kwa uzalishaji wa chakula na usindikaji wa mazao ya kilimo. Itahamasisha
wakulima kuuza bidhaa zilizoongezwa thamani.
|