|
Elimu Bora
Hali Halisi ya Elimu Ikoje Tanzania?
Ubora wa elimu Tanzania umeporomoka. Wanafunzi wanarundikana madarasani na wengine hata kusomea chini ya miti.
Mitaala haiendani na hali halisi, vipaji haviendelezwi. Mazingira ya shule hayana mtazamo wa kijinsia na hayawajali watoto
wenye ulemavu. Mfumo wa elimu ya msingi haumwandai mwanafunzi kuwa raia wa kujitegemea anapohitimu.
-
Bajeti ya Elimu finyu. Waalimu ni wachache, wamefukarishwa na hawaendelezwi kitaaluma. Shule na vyuo hazina
vifaa vya kuweza kutosheleza ongezeko la wanafunzi.
- Gharama za elimu bado ni mzigo mkubwa kwa familia masikini. Wazazi wengi wameshindwa kupeleka watoto wao katika
shule za sekondari na vyuo vya elimu ya juu ilhali walionacho wachache wanasomesha watoto wao katika shule za gharama kubwa. Matokeo
yake mfumo wa elimu unajenga matabaka ya matajiri walioelimika na maskini mbumbumbu.
Serikali ya CHADEMA itafanya nini?
- CHADEMA inaamini kwamba elimu ndio chimbuko la maendeleo ya binadamu yeyote yule. Tunatambua kwamba mataifa
yaliyoendelea mengine yakiwa ni machanga kama Tanzania yamezingatia kuwekeza katika elimu. Kwa CHADEMA elimu ndio sekta ongozi
katika kuchochea maendeleo, mabadiliko na uhuru wa kweli. Kwa lengo hili basi, CHADEMA itaboresha elimu kwa kuipa kipaumbele.
- Itabadili mitaala ya elimu. Mitaala italenga mahitaji na maslahi ya taifa, na kuchochea fikra, udadisi,
ugunduzi na kuendeleza vipaji. Masomo ya biashara na kilimo yatarejeshwa katika mitaala. Mashindano ya Umiseta na Umitashumta
yatarejeshwa. Elimu ya awali mpaka kidato cha pili itakuwa ya lazima na bure kwa kila Mtanzania.
- Bajeti ya elimu kupanda kutoka 18% mpaka 35%.
Itajali waalimu kwa kuboresha kipato, makazi na mafunzo yao.
Shule na vyuo vitapatiwa vifaa vya kiada na ziada vya kutosha.
- Itapunguza mzigo wa gharama za elimu kwa Watanzania maskini. Itatoa ruzuku kwa shule za sekondari na vyuo
vya elimu ya juu. Itabadili shule za serikali kuwa ni vituo vya ubora wa elimu ili kuondoa matabaka.
|