lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
banner
Ilani ya Chama
»Utangulizi
»Utekelezaji wa ilani
»Tanzania tuitakayo
»Mfumo wa Utawala
»Elimu Bora
»Afya kwa Wote
»Kilimo cha Kisasa
»Uchumi wenye Ajira
»Michezo
b.part
Habari za Uchaguzi
»Jiandae kwa 2010
»Jiandae kwa 2009
»Ilani ya 2005
»Ripoti ya Uchaguzi
»Gharama za 2005
»Matokeo kura Urais
»Matokeo Ubunge
»Matokeo kimkoa
»Kura za Awali
»Kampeni
b.part
Barua Pepe
jina la mtumiaji:
neno-siri
rt.bt.spc
bt.part2

Afya kwa Wote

Hali Halisi ya Afya Ikoje Tanzania?

  1. Mazingira duni ya wahudumu wa afya. Madaktari na manesi wanapata maslahi duni, vitendea kazi haba na chakavu na hospitali ni chafu. Hali hii imewajengea wahudumu wa afya mazingira ya rushwa.



  2. Gharama za afya ni mzigo kwa wananchi. Serikali imekwepa jukumu la kutoa huduma za afya kwa wananchi. Huduma za afya zimekuwa za kibiashara.

  3. Huduma ya afya haziridhishi. Licha ya kuchangia gharama huduma ni mbaya na zinatolewa kwa misingi ya rushwa. Wakati wananchi wanapoteza maisha yao kwa magonjwa yanayotibika kama malaria viongozi wanafuja fedha nyingi za umma kutibiwa nje ya nchi. Wagonjwa zaidi ya mmoja kulala kitanda kimoja limekuwa jambo la kawaida. Inasikitisha zaidi kuona kina mama wajawazito wakilazimishwa kwenda kujifungua bila vifaa kama vile pamba, gloves na hata nyembe! Hii imefanya kina mama waendelee kujifungulia majumbani au hata kwa wakunga wa jadi kwa kukosa vifaa husika. Kujifungua ni jambo linalostahili staha na faragha.


Serikali ya CHADEMA itafanya nini?

  1. CHADEMA inaamini kuwa afya bora ndio msingi wa maendeleo. Wananchi wasio na afya bora hawataweza kujishughulisha katika ujenzi wa Taifa lao na katika kujipatia kipato cha kuendesha maisha yao ya kila siku. Tunatambua kuwa mataifa mengi yaliyoendelea yamefanikiwa kwa kuwekeza katika afya. Kwa CHADEMA sekta ya afya itaboreshwa zaidi ili wananchi wote waweze kupata huduma hii muhimu ili waweze kuchangia vyema katika maendeleo ya nchi yao.

  2. Gharama nafuu za huduma ya afya. Itapanua mpango wa bima ya afya kwa kumshirikisha kila Mtanzania. Huduma zote zinazohusu afya ya mama na mtoto zitaondolewa kodi na kutengewa fedha za kutosha. Itatoa tiba ya malaria bure.


  3. Huduma kwa wanaoishi na VVU. Serikali za mitaa zitawahudumia watu wanaoishi na VVU kwa kuwapatia dawa za kurefusha maisha na matunzo ikiwemo lishe bora.


  4. Bajeti ya afya kuongezwa. Maslahi na vitendea kazi vya madaktari na manesi kuboreshwa. Itatoa motisha kwa hospitali safi.
  Tunaahidi nini kwenye Kilimo?


lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl