lf.bevel
MWANZO CHAMA SERA KATIBA TUUNGE MKONO UCHAGUZI TUWASILIANE
banner
Uzinduzi wa Chama
»Utangulizi
»Tumaini Jipya!
»Hotuba ya Uzinduzi
»Mpango Mkakati
»Marekebisho Katiba
»Bendera Mpya
»Wimbo wa Chama
b.part
Mengineyo
»Habari Mpya
»Makala mbalimbali
»Midahalo
»Blogu za wanachama
»Picha za matukio
»Maoni Yenu
b.part
Barua Pepe
jina la mtumiaji:
neno-siri
rt.bt.spc
bt.part2

KADI MPYA ZA WANACHADEMA


kadi

Uzinduzi mpya wa chama hapo Agosti 13 2006 uliambatana na uzinduzi wa kadi mpya za uanachama wa CHADEMA.

Tumeamua kuleta imani, matumaini na mwelekeo zaidi katika uanachama na sasa tutaanza kuandikisha wanachama upya. Tumeamua kusitisha utamaduni wa kutoa kadi bure ingawa kadi za CHADEMA bado zitaendelea kuuzwa kwa bei ndogo ili kila Mtanzania aweze kugharamia.

Lengo ni kuhakikisha kila anayechukua kadi ya chama anachangia kama ishara ya nia yake ya kuunga mkono chama na harakati za ukombozi wa nchi hii. Tunataka tuwe na wanachama hai chini ya mkakati wa “CHADEMA ni msingi”. Tunataka wanachama wamiliki na kukiendesha chama. Michango hii midogo midogo ikiunganishwa pamoja ni nguvu ya pekee katika kuchochea kujitegemea na kuendesha chama kwa nguvu ya wanachama. Kama ambavyo bahari ni muunganiko wa matone madogo madogo ya maji ndivyo ambavyo michango hii inaweza kukijenga chama. Tunataka uanachama uwe chachu ya imani, matumaini na mwelekeo wa CHADEMA.


dokezo:

Unaweza kujaza fomu hapa kisha ukapata kadi ya Uanachama!
Usisubiri, kuwa Mwanachama leo!


lf.curl lf.curl2 rt.curl2 rt.curl