<?xml version='1.0' encoding='UTF-8'?><rss xmlns:atom='http://www.w3.org/2005/Atom' xmlns:openSearch='http://a9.com/-/spec/opensearchrss/1.0/' version='2.0'><channel><atom:id>tag:blogger.com,1999:blog-13876107</atom:id><lastBuildDate>Tue, 22 Apr 2008 20:12:27 +0000</lastBuildDate><title>Blogu ya J.J. Mnyika</title><description/><link>http://www.chadema.net/blogu/mnyika/</link><managingEditor>UDI</managingEditor><generator>Blogger</generator><openSearch:totalResults>25</openSearch:totalResults><openSearch:startIndex>1</openSearch:startIndex><openSearch:itemsPerPage>25</openSearch:itemsPerPage><item><guid isPermaLink='false'>tag:blogger.com,1999:blog-13876107.post-8399857045552001604</guid><pubDate>Tue, 22 Apr 2008 20:12:00 +0000</pubDate><atom:updated>2008-04-22T23:12:28.160+03:00</atom:updated><title></title><description>Bado nalijaribu jamvi jipya</description><link>http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2008/04/bado-nalijaribu-jamvi-jipya.html</link><author>UDI</author></item><item><guid isPermaLink='false'>tag:blogger.com,1999:blog-13876107.post-7480841724861753642</guid><pubDate>Mon, 03 Mar 2008 09:58:00 +0000</pubDate><atom:updated>2008-03-03T13:01:52.585+03:00</atom:updated><title></title><description>Kingunge alijivunjia mwenyewe heshima&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hebu nikukumbushe kauli zake kidoooooooooogo---&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;TAMKO KUHUSU KAULI ZA KINGUNGESisi, viongozi wa vyama vya CHADEMA, CUF, NCCR Mageuzina TLP tuliokutana Equator Hotel tarehe 20 Septemba2007 hapa Arusha tumeitafakari “Orodha yaMafisadi”(List of Shame) na tumejadili kauli za Waziriwa Nchi, Ofisi ya Rais, Siasa na Uhusiano waJamii-Mheshimiwa Kingunge Ngombale-Mwiru alizozitoa 18Septemba 2007 na kunukuliwa na vyombo mbalimbali vyahabari Jumatano 19 Septemba 2007 na kwa pamojatumeazimia kutoa tamko lifuatalo:Kingunge anapotosha umma, apuuzwe; wapinzani wanateteataifaTunaunga mkono uamuzi wa viongozi wetu wa kitaifakuanika wazi kwa umma orodha ya mafisadi; hii ni kwasababu rasilimali zinazofujwa ni za wananchiwatanzania, wanaoathirika kutokana na ufisadi ni ummawa watanzania na wenye uamuzi wa mwisho wakuwawajibisha viongozi mafisadi ni umma wa watanzania.Kwa kuzunguka nchini kueleza yaliyotokea bungeni(hususani kusimamishwa kwa Mbunge Zitto Kabwe nakupigwa danadana kwa hoja ya kashfa ya ufisadi ndaniya Benki Kuu iliyokuwa iwasilishwe na Dr WilbroadSlaa) wakati wa Mkutano wa Bunge la Bajetiuliomalizika hivi karibuni, wabunge wa upinzaniwanatimiza wajibu wao kama wawakilishi wa kweli wawananchi. Kwa kuzunguka nchini kueleza kuhusu ufisadiunaendelea nchini, viongozi wa upinzani wanatekelezawajibu wao wa kisiasa wa kuwazungumzia wananchi wotewa Tanzania wanaoguswa na ufisadi bila kujali itikadiama uanachama; ikumbukwe kuwa vyama vya siasa siovyombo vya uchaguzi tu bali ni taasisi muhimu katikajamii katika kuchochea uwajibikaji na maendeleo. Kwamantiki hiyo basi Waziri Kingunge anaupotosha ummaanaposema kwamba ziara za viongozi wa upinzanizinatokana na ‘hasira ya kushindwa uchaguzi mkuu 2005,kambi ya upinzani kushindwa kumtetea Zitto bungeni,wivu wa kuona CCM inatekeleza ilani yake vizuri, nakwamba wanautumia vibaya mfumo wa vyama vingi’.Tunapenda kusisitiza kuwa Viongozi wa umma wanaokiukana/au kuvunja masharti ya katiba ya Jamhuri yaMuungano na Sheria za Maadili ya Viongozi wa ummalazima waanikwe hadharani na kuwajibishwa na yoyoteanayetoka kauli ya kubeza jitahada hizi ni vyemawatanzania wakampuuza. Kama viongozi wa upinzaniwanavunja sheria kwa kutoa uzushi na kufanya uchochezikama Waziri Kingunge anavyodai kwa nini serikalihaiwakamati na kuwapeleka mahakamani badala ya kutoamatamko ya kulalamika?Kauli za Kingunge ni msimamo wa Serikali?; Ikulu itoetamko!Tumezijadili kauli za Waziri Kingunge na katika hatuaya sasa tusingependa kuamini kama zinawakilishamsimamo wa serikali kwa ujumla wake; hatutaki kuaminikwamba kauli hizo ni msimamo wa pamoja wa Serikalichini ya Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekitiwa Baraza la Mawaziri. Katika hatua ya sasatunazichukulia kauli hizo kuwa ni maoni binafsi yaBwana Kingunge mpaka hapo Ikulu itakapothibitishavinginevyo; hivyo kwa tamko hili tungependa ikulu itoeufafanuzi kuhusu kauli hizo. Lakini tunapenda piakutoa tahadhari kwamba inawezekana kauli hizi za BwanaKingunge amezitoa kwa nia ya kupoteza lengo tuanzekuzijadili kauli zake badala ya kujadili orodha yamafisadi na hatma ya rasilimali za nchi yetu. Hivyotungependa kusisitiza kuwa ikulu ijibu hojazilizotolewa na viongozi wa upinzani ambazo zimemgusamoja kwa moja Rais na serikali.Anayelinda ufisadi ndiye anayekwamisha maendeleo nahuduma za kijamiiTunashangazwa na uamuzi kauli ya Kingunge kwambauamuzi wa Viongozi wa Vyama na Wabunge wa Upinzanikuzunguka nchini ni mkakati wa kisiasa wa kuitoaserikali kwenye mstari wa kushughulikia maji, afya nabarabara. Tunapenda kumbukusha Waziri Kingunge kuwakatika orodha hii ya mafisadi pekee zaidi ya shilingitrilioni 1.3(1,300,000,000,000) ambazo kamazingetumika vizuri ni wazi zingeweza kutumikakuboresha maji, umeme na barabara bila kuendeleakuwakamua zaidi wananchi masikini. Ukweli ni kuwa kwakuendelea kulea ufisadi serikali inajitoa yenyewekwenye mstari wa kutumia vyema kodi za wananchi narasilimali za taifa katika kushughulikia shughuli zamaendeleo na huduma za kijamii ikiwemo maji, afya nabarabara. Ni ukweli pia kwamba kwa kuwawajibishamafisadi viongozi wa upinzani wanatimiza wajibu wao wakuhakikisha rasilimali za taifa zinatumika kwa ustawiwa wananchi walio wengi.Vyombo vya dola tayari vinayo orodha ya mafisadi;vichukue hatuaTunashangazwa na kauli ya Waziri Kingunge ya kuhojisababu za Viongozi wa Upinzani kushindwa kuziwasilishakwenye vyombo vya dola tuhuma walizozitoa dhidi yavigogo hao iwapo kweli wanao ushahidi wakuzithibitisha. Tunashangazwa na kauli hii kwa kuwatunaamini kabisa Waziri Kingunge anafahamu kabisa kuwasehemu kubwa ya tuhuma hizi zipo katika Ripoti zaMkaguzi wa Serikali ikiwemo ile ya mwaka 2005/06 nakwamba vyombo vya dola vinafahamu uwepo wa tuhuma hizilakini kwa zaidi ya miaka miwili vyombo hivyohavijachukua hatua dhidi ya vigogo waliotajwa.Tunaamini kwamba viongozi wa upinzani walichofanya nikuamua kushtaki kwa wenye mali walioibiwa ambao niwananchi wote wa Tanzania ili kwa pamoja tuwezekuvitaka vyombo vya dola viweze kuchukua hatua.Tunashangazwa na kauli hii ya Waziri Kingunge ya‘kuwahukumu’ viongozi wa upinzani kwa kushindwakupeleka ushahidi kwa kuwa kauli hii inapingana nakauli zingine ambazo zimewahi kutolewa na viongozi waserikali kuhusu tuhuma hizo hizo. Tunapendakumkumbusha Waziri Kingunge kwamba tayari Spika WaBunge-Samuel Sitta alishasema kwamba anavipelekapolisi vielelezo vyote vya ushahidi alivyotoa Dr Slaaili vichunguzwe. Pengine Kingunge angetoa hukumu hiyokwa Spika kwa kushindwa kupeleka vielelezo. Piaikumbukwe kwamba ni serikali hiyo hiyo iliyowahi kutoataarifa kwa umma kwamba tuhuma za ufisadi ikiwemo zaBOT zinachunguzwa na TAKUKURU. Kadhalika WaziriMkuu-Edward Lowasa alitoa kauli baadaye kwambaSerikali iliyafahamu madai ya Kashfa ya ufisadi BenkiKuu(BOT) kabla ya upinzani. Kwa upande mwingine, madaiya kutaka kushughulikia rushwa kubwa kubwa ikiwemo zakwenye mikataba yalianza kutolewa na Rais Kikwetewakati akifungua Mkutano wa Kwanza kabisa wa Bungemwaka 2005. Lakini baadaye ni Rais Kikwete alinukuliwana vyombo vya habari akisema kwamba anawafahamu walarushwa na anawapa muda wajirekebishe; tulitarajiaWaziri Kingunge kama mshauri wa Rais wa masuala yasiasa angemshauri apeleke ushahidi katika vyombo vyadola na si kuwahukumu viongozi wa upinzani ambaowametoa orodha ya mafisadi na ushahidi kutoka kwenyetaasisi za serikali yenyewe!. Na ni jukumu la vyombovya dola kuchukua hatua za kufuatilia baada ya orodhaya mafisadi kuwekwa hadharani.TAKUKURU inajipotezea imani yenyewe!Tumeshangazwa pia na kauli ya Waziri Kingunge yakuwalaumu viongozi wa upinzani kwa kutokuwa na imanina TAKUKURU. Kwa misingi ya kauli zao ambazo wamezitoakatika nyakati mbalimbali, viongozi wa upinzaniwamekuwa wakikisisitiza kuwa TAKUKURU inajipotezeayenyewe imani kwa wananchi kutokana na taarifa zake nakwamba wamekuwa wakiipa changamoto TAKUKURU kuchukuahatua. Mathalani TAKURU kuisafisha kampuni yaRICHMOND. “….hakuna ushahidi wowote uliopatikanakuthibitisha vitendo vya rushwa, uzembe na upokeaji wakamisheni watendaji wa serikali….uchunguzi huoumethibitisha udhaifu wa kawaida katika utendaji naambao haukuhusisha rushwa au manufaa ya aina yoyoteile kwa upande wa watendaji na hakuna hasarailiyosababishwa na udhaifu huo”(Mwananchi 12/5/2007).“….baada ya kuona hivyo, Richmond ilionekana kufahamumwenendo wa mambo serikalini…”(Tanzania Daima12/5/2007). Maswali yaliyobaki mpaka hivi sasa ambayosi TAKURU wala TAKUKURU ya sasa hawajayajibu ni pamojana: Ni kwanini Kamati ya Waziri Mkuu iliipa tendaRichmond baada ya Bodi ya Wakurugenzi ya Tanescokuitaka bodi yake ya sabuni kutangaza upya zabuni hiyokwa kutimia zabuni za kimataifa? Richmond kuwezakufahamu mwenendo wa mambo ya ndani serikalini sioishara ya rushwa ya kimadaraka? Ni kweli kama hakunahasara iliyosababishwa na uamuzi huu wakati ambapowatanzania wamekaa bila umeme kwa miezi mingi bilakupata umeme wa dharura waliotarajia wakati wadharura, Rais amekiri kwamba umeme ulichangia kushukakwa kasi ya ukuaji wa uchumi na hata kuongeza mfumukowa bei na mpaka leo bado megawatts 100 hazijatimizwana Richmond/Dowans? Tunapenda kumkumbusha WaziriKingunge kwamba Mkataba wa Richmond/Dowans pekeeumeligharimu taifa zaidi ya Bilioni 200 mpaka sasaambazo zingeweza kuelekezwa kwenye elimu, afya nabarabara. Viongozi wa upinzani wanapohoji utendaji waTAKUKURU wanataka ichukue hatua za harakakushughulikia mafisadi na kuendelea kuwa Taasisi yaKuzuia na Kudhibiti Rushwa na si Taasisi ya Kulinda,Kusafisha ama Kutetea Rushwa !Wasomi na asasi za kijamii wako sahihi; Kingungeamelewa madarakaTumefadhaishwa na kauli ya Waziri Kingunge kwambawasomi nchini wametathimini uamuzi wa Bunge wakumsimamisha Mbunge Zitto Kabwe kwa kutanguliza jazbabadala ya busara na kutilia wasiwasi uelewa wa makundiya kijamii kuhusu mantiki ya uzalendo. Hatutakikuamini katika hatua ya sasa kwamba huu ni msimamo waserikali kwamba wasomi na makundi ya kijamiiwametanguliza jazba na kukosa busara na uelewa katikakuijadili adhabu aliyopewa Mbunge Zitto Kabwe na hojayake ya kutetea Rasilimali za nchi yetu hususanimadini. Tunaamini kwamba kauli hii ni maoni binafsi yaBwana Kingunge ambayo ni ishara ya kulewa madarakakutokana kung’ang’ania serikalini toka wakati nchi hiiinapata uhuru kwani hii si mara ya kwanza kutoa kauliza kubeza-aliwahi kuibeza CHADEMA kwa kumtaja Nyererekwenye kampeni 2005 na hivi karibuni Julai 3, 2007aliripotiwa na vyombo vya habari akitetea msimamo waRais Kikwete wa kutumia nafasi yake kama raiskudhoofisha upinzani kwa kufanya kampeni za CCM katikamikutano ya kiserikali. Tunapenda kumbukusha WaziriKingunge maneno ya Shaban Robert kwamba “ elimuilipokuwa bado kujulikana mvi zilihesabika kuwa alamaya hekima lakini fikra hizo wakati wake umeshapitahaupo na wala hauji tena. Kisichobadilika ni kwambamtu mzima bado anastahili heshima kutoka kwa mdogo” .Ni vyema Waziri Kingunge akafahamu kwamba wasomi kamaProfesa Issa Shivji na makundi ya Kijamii mathalaniMtandano wa Jinsia(TGNP), Chama cha Wanasheria waMazingira(LEAT), Kituo cha Sheria na Haki zaBinadamu(LHRC) walifanya tathmini yao kwa lengo lakulinda maslahi ya taifa bila kujali itikadi.Mafisadi zaidi waendelee kutajwa; serikali ijibu hojaHivyo tunapongeza na tutaendelea kuunga mkono jitahadazote za vyama vya siasa, asasi za kijamii na hata watubinafsi waliowataja na watakaoendelea kuwatajaviongozi na/au maafisa wa umma na/au mawakala na/auwashirika wao katika sekta binafsi ambao kwa namnambali mbali wameshiriki katika kupora utajiri na/aufedha za umma na hivyo kulisababishia taifa na umma waWatanzania ufukara na/au umaskini mkubwa. Kadhalikatunaunga mkono na kutoa mwito kwa vyama vya siasa,asasi za kijamii na hata watu binafsi kuendeleakuwawajibisha viongozi wa umma ambao kwa kutumianyadhifa na/au vyeo vyao katika utumishi wa ummawamefanya maamuzi ambayo yamesababisha taifalimepoteza mapato na/au utajiri na rasilmali zake nakuwaneemesha raia na/au taasisi za kiuchumi na/au zakibiashara za kigeni. Kwa mfano, viongozi wa ummawalioshiriki katika kusaini mikataba mibovu katikasekta za madini na/au nishati na/au maeneo mengineyenye umuhimu mkubwa kwa maisha ya taifa na jamii yaWatanzania. Na katika haya tunataka serikali ijibuhoja na si kupuuzia na kutoa kauli za kejeli kama "haoni wapinzani hawana jingine la kufanya", "wana haki yakutoa maoni yao na huo ndio uzuri wa demokrasia" .Waziri Kingunge na serikali kumbukeni kuwa watuwachache wanaweza kudanganyika katika muda mchachelakini watu wote hawewezi kudanganywa wakati wote.Watanzania wa leo na kesho si watanzania wa jana najuzi.John MnyikaMkurugenzi wa Vijana Taifa (CHADEMA)Na Mwenyekiti wa KikaoGodbless LemaKatibu Mwenezi Mkoa-Arusha(TLP)Na Msemaji wa Ushirikiano wa Vyama vya Upinzani-ArushaMohamed MaabadMwenyekiti wa Wilaya-Arusha Mjini(CUF)Na Mwenyekiti wa Ushirikiano wa Vyama vyaUpinzani-ArushaEned MuroMwakilishi-Arusha(NCCR-Mageuzi)Amos KibandaKatibu Mkoa-Arusha(CHADEMA)Calist LazaroMwenyekiti wa wilaya-Arusha Mjini (TLP)</description><link>http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2008/03/kingunge-alijivunjia-mwenyewe-heshima.html</link><author>UDI</author></item><item><guid isPermaLink='false'>tag:blogger.com,1999:blog-13876107.post-6276351187241246573</guid><pubDate>Wed, 20 Feb 2008 17:29:00 +0000</pubDate><atom:updated>2008-02-20T20:32:27.697+03:00</atom:updated><category domain='http://www.blogger.com/atom/ns#'>Jambo Forum ifunguliwe</category><title></title><description>&lt;div align="justify"&gt;Kwa niaba ya Baraza la Vijana wa CHADEMA(BAVICHA), vijana wa CHADEMA tunaungana na wapenda uhuru, haki na ukweli kote nchini kulaani uamuzi wa Jeshi la Polisi kuwakamata na kuwaweka ndani vijana wa wawili wa kitanzania Maxence Melo na Mike Mushi kwa sababu ya masuala ya mtandao wa Jambo Forum(&lt;a href="http://www.jamboforums.com/"&gt;www.jamboforums.com&lt;/a&gt;).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uamuzi wa kuwakamata na kuwaweka ndani kwa takribani saa 24 na kuwahoji kwa zaidi ya saa 14(usiku na mchana) tunaona ni kinyume cha sheria ambayo inaeleza bayana mtuhumiwa anapaswa kuhojiwa si zaidi ya masaa manne kwa mfululizo na kwa ujumla ni uvunjaji wa haki za binadamu na haki za kikatiba za kupata na kutoa taarifa/habari. Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali katika Jeshi la Polisi, vijana hawa wamekamatwa kwa kutuhumiwa kuendesha mtandao wa Jambo Forum ambao unadaiwa kuwachafua watu mbalimbali ambao vyanzo hivyo vya polisi mpaka sasa havijawataja.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vyanzo mbambali vya polisi vimeeleza kuwa uamuzi wa kuwakamata vijana hawa umetokana na jeshi la polisi kupata mashtaka toka kwa watu wasiotajwa kwamba mtandao huo umekuwa ukiwachafua watu mbalimbali hususani viongozi wa serikali; suala hili nao linakwenda kinyume cha misingi ya kikatiba na kisheria. Sisi tunaamini kwamba kama kuna mtanzania yoyote ambaye anadhani amekashifiwa na mtandao huo ana haki ya kukanusha ama kuchukua hatua za kisheria kwa kwenda mahakamani. Mikakati hii ya kuzuia uhuru wa habari iliwahi kujitokeza siku za usoni pale upinzani ulipotoa ‘orodha ya mafisadi’ na baadhi ya vyombo vya habari kuchapa majina hayo vilipewa vitisho mbalimbali na watuhumiwa hao wa ufisadi ambao walisema wamechafuliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali na vyombo vya dola ni vyema vikafahamu kwamba uhuru wa maoni kupitia katika mitandao unafaida zake na hasara zake, hivyo kuundoa uhuru wote kwa sababu za malalamiko ya watu wachache, masuala binafsi au migogoro ya familia Fulani ni kuukosesha umma faida ambazo zinatokana na mitandao kama Jambo Forum. Pia serikali ifahamu kwamba sheria nyingi za Tanzania zinasimamia masuala ya habari ziko kimya kuhusu masuala ya habari katika mitandao hivyo, mitandao kama Jambo Forum inalindwa kwa kanuni na mikataba ya kimataifa ambapo imesajiliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunarudia tena kukumbusha kuwa mwanahabari ni mjumbe tu wakufikisha ujumbe katika jamii; ambaye anapaswa kulindwa na kuheshimiwa. Tabia inayoanza kuchipua ya kuwanyanyasa wajumbe au chombo kilichofikisha ujumbe tena kwa njia ambazo ni kinyume cha sheria na haki binadamu badala ya kuushughulikia ujumbe wenyewe; ikiachwa ikashamiri inaweza ikatishia ufanisi wa sekta ya habari ambayo inapaswa kudumishwa kama mhimili wa nne wa dola.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha vijana wa CHADEMA tumesikitishwa na kutoweka hewani kwa mtandao wa Jambo Forum ambako kutokana na vyanzo mbalimbali inaelezwa kwamba waratibu wa mtandao huo wameshinikizwa kuufunga kutokana na shinikizo la ‘kigogo’ mmoja wa jeshi la polisi kwa maelekezo toka serikalini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jambo Forum Wanahabari imekuwa mstari wa mbele kwa uwazi bila woga katika mapambano dhidi ya ufisadi na kutetea rasilimali za taifa, na kuwa sehemu ya jukwaa la sauti umma kusikika na habari kusambaa ndani na nje ya Tanzania kutia teknolojia ya habari na mawasiliano(TEKNOHAMA). Jambo Forum imekuwa mstari mbele katika kuandika tuhuma za ufisadi na/au matumizi mabaya ya madaraka zinazowakabili viongozi kadhaa wa serikali, makampuni na taasisi mbalimbali.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mtandao wa Jambo Forums ni moja katika ya vyombo vya habari na majukwaa ya umma yaliyohusika kwa kiasi kikubwa kwa kulifunua na kuliweka wazi sakata la Richmond hasa baada ya kuweka hadharani mkataba wa Richmond na kuchambua mambo mbalimbali yanayohusiana na mkataba huo. Kashfa ya Richmond ndiyo iliyosababisha kujiuzulu kwa Waziri Mkuu Mhe. Edward Lowassa na baadaye kuvunjwa kwa baraza la Mawaziri.  Jambo Forum imewezesha ‘siri’ za ufisadi zinazofichwa na baadhi ya vigogo ikiwemo serikalini kuwekwa wazi kwa umma na watumishi mbalimbali wa serikali na taasisi mbalimbali bila majina yao kujulikana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mtandao wa Jambo Forum umekuwa ni changamoto kwa mitandao mingine ya serikali ikiwemo kitengo cha mawasiliano cha Ikulu kuboresha ufanisi wao katika kutumia TEKNOHAMA katika kuwasiliana kwa umma. Mtandao huo umekuwa ni ukumbi pia wa vyombo vya ulinzi na usalama ikiwemo polisi kupata mawazo mbalimbali ya umma kuhusu masuala ya uhalifu yanayopaswa kufuatiliwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; “Inashangaza badala ya serikali kutoa ushirikiano kwa mitandao kama hii inakuwa mstari wa mbele kuona kwamba inafungwa. Huku ni kukinzana na dhamira ya Rais Kikwete ya kuongeza uhuru wa habari na haki ya Taarifa hapa nchini. Sisi tulitegemea vipaji vya vijana wanaotengeneza mitandao mbalimbali vikuzwe kwa maslahi ya Taifa badala ya kukamatwa”.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vijana wa CHADEMA tunatoa rai kwa umma kutochukulia suala hili kuwa ni tukio dogo linalowahusu vijana wawili waliokamatwa bali litazamwe kama tukio linalohusu maslahi ya taifa, uhuru wa vyombo vya habari na haki za kikatiba za kupata na kutoa taarifa/mawazo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo tunaitaka serikali kutoa tamko la kina lenye kueleza ni kwa sababu zipi zilizopelekea kukamatwa na vijana hawa na walalamikaji ni wakina nani. Pia serikali itoe tamko rasmi kama imeufungia mtandao wa Jambo Forum au la na tunawataka watanzania wanaoratibu mtandao huo kwa mapenzi mema ya nchi yao waurudishe mtandao huo hewani mapema iwezakanavyo wakati tamko la serikali linasubiriwa. Kadhalika tunatoa rai kwa yoyote ambae anadhani hajatendewa haki ama amechafuliwa na Jambo Forum ajitokeze kukanusha au kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mtandao huo badala ya kulitumia jeshi la polisi ama baadhi ya watu kuhujumu haki ya umma ya kupata na kutoa taarifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Katika mataifa mbalimbali duniani, mitandao kama Jambo Forum inachukuliwa kama sehemu ya vyombo vya habari na mahali pa umma kukutana kujadili masuala mbalimbali. Hivyo uamuzi wa kufungia Jambo Forum, ni sawa na uamuzi wa kufungia chombo kingine cha habari kama redio, televisheni na magazeti. Kadhalika, uamuzi wa kufungia Jambo Forum ambapo umma wa watanzania kwa maelfu umekuwa ukikutana kujadili masuala mbalimbali ni sawa na kupiga marufuku kukusanyika huko ambapo ni kinyume cha katiba ya nchi na mikataba ya kimataifa ya haki za binadamu. Mwisho, tunaitaka serikali na vyombo vya dola visidhani Jambo Forum ni Maxence Melo ama Mike Mushi bali mihimili ya Jambo Forums kwani ni umma wa wachangiaji na wasomaji waliosambaa hapa nchini na nchi mbalimbali ambao baadhi yao wanaweza kukamatwa, majukwaa yao kuweza kushambuliwa, lakini mawazo yao ya mabadiliko yataishi milele hata pale ndoto ya maendeleo, uhuru na umoja itakapotimia katika taifa letu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Imetolewa tarehe 20 Februari 2008 na:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika&lt;br /&gt;Mkurugenzi wa Vijana&lt;br /&gt;0754694553&lt;br /&gt; &lt;/div&gt;</description><link>http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2008/02/kwa-niaba-ya-baraza-la-vijana-wa.html</link><author>UDI</author></item><item><guid isPermaLink='false'>tag:blogger.com,1999:blog-13876107.post-161615833032048422</guid><pubDate>Thu, 17 Jan 2008 08:33:00 +0000</pubDate><atom:updated>2008-01-17T11:33:44.923+03:00</atom:updated><title></title><description>TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;WAZIRI MAGUFULI INGILIA KATI HATMA YA WAKAZI KIBAMBA&lt;br /&gt;UTEKELEZAJI WA MRADI WA MIUNDO MBINU YA NGAZI YA WILAYA ENEO LA LUGURUNI NA KIBAMBA HOSPITALI KUKIUKA SHERIA ZA ARDHI ZA TANZANIA NA HAKI ZA MAKAZI&lt;br /&gt;MAOFISA WANAOTUHIMIWA KUJIHUSISHA NA RUSHWA NA KUVUNJA HAKI ZA BINADAMU KATIKA UTEKELEZAJI WA MRADI WACHUKULIWE HATUA.&lt;br /&gt;MCHAKATO WA MRADI UWEKWE WAZI KWA UMMA&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa tamko hili naungana na wakazi wenzangu wa Jimbo La Ubungo wanaokaa katika Kata ya Kibamba kupinga kitendo cha kutaka kuwahamisha Kimabavu kutoka katika ardhi na makazi yao ambavyo wamemiliki kihalali kwa mujibu wa sheria za nchi ya Tanzania kwa kushirikisha ngazi zote za Serikali ya Muungano wa Tanzania zikiwemo Serikali za Vijiji, Mitaa, Kata, Manispaa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi.  Kuwahamisha Kimabavu ni ukiukwaji mkubwa wa Sheria za Ardhi pamoja na Haki za Makazi kama zilivyoainishwa katika Tamko la Kimataifa ya Haki za Binadamu, ambayo Tanzania imesaini. &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hakika, vitendo vya watumishi wa Wizara yako, Halmashauri ya Jiji na Manispaa ya Kinondoni waliokabidhiwa jukumu la kutekeleza mradi huu vimepelekea utekelezaji wa mradi huu kuchukua sura ya kuhamisha watu kimabavu kutokana na kukiuka kabisa mwongozo wa uhamishaji watu kama ulivyoainishwa katika Sheria ya Kimataifa ya Haki za Binadamu na Haki za Makazi; mikataba ambayo Tanzania imeridhia. Na baada ya kuridhia Serikali ya Tanzania iliwajibika kuuingiza mwongozo huo katika Sheria za Ardhi zinazoongoza watu kuhamishwa kutoka katika Ardhi na Makazi yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo basi namuomba Mhe John Magufuli- Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi kuingilia kati suala la wananchi wa Jimbo la Ubungo Kata ya Kibamba kuhamishwa kimabavu katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundo mbinu eneo la Luguruni na Kibamba Hospitali na kufanya yafuatayo:-&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;1)      Wizara yako isitishe notisi ya siku 30 iliyotolewa kwa waathrika kuwa wamehama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;2)      Wizara yako isitishe vitendo vya kuvunja mkataba kati yake na wananchi wa Luguruni na Kibamba Hospitali uliofikiwa mwezi Febrauari 2007 kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ngazi ya wilaya eneo la Luguruni na Kibamba Hospitali kwa kutumia ardhi ya wananchi waliopo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;3)      Wizara yako ifanyie uchunguzi wa kina malalamiko ya ukiukwaji taratibu zilizomo ndani ya Sheria ya Ardhi na Sheria ya Kimataifa ya Haki za Binadamu na Haki za Makazi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;4)      Wizara yako isitishe zoezi zima la utekelezaji wa mradi huu hadi hapo tathmini itakayo washirikisha waathrika kuhusu kuepukika au kutoepukika kwa uhamishwaji watu katika utekelezaji wa mradi huu. Mchakato wa mradi mzima uwekwe wazi kwa umma ikiwemo bajeti ya mradi na mchakato wa utekelezaji. Kama Serikali (Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi, JIJI na Manispaa ya Kinondoni) hazitaki kuwashirikisha waathrika katika kupendekeza mbinu mbadala badala ya watu kuhamishwa,  ziwajibike kuhakikisha inapata ridhaa wote itakaowahamisha badala ya kufanya hivyo kwa mabavu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;5)      Endapo baada ya tathmini shirikishi, baadhi ya kaya zitalazimika kuhamishwa, mpango kabambe ambao utakaokuwa shirikishi uandaliwe kuhusu hatma ya kaya zitakazolazimika kuhamishwa. Mpango huo uandae kwa uwazi  raslimali za kutosha kuwalipa fidia itakazowezesha kaya husika kurejea katika kiwango cha maisha walioyokuwa nayo kabla ya kuhamishwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;6)      Endapo baada ya tathmini shirikishi, baadhi ya kaya zitalazimika kuhamishwa tathmini ya thamani ya mali ifanyike upya ikiwashirikisha independent valuers kwa nia ya kuepuka vitendo vya wananchi kudaiwa rushwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;7)       Wizara yako isimamie majadiliano ya pamoja kati ya watekelezaji wa mradi na waathrika kutathmini endapo zipo mbinu zinzoweza kutumika kuepuka watu wasihamishwe kutoka katika ardhi na makazi yao k.m waathrika wakaelekezwa kuwekeza katika miradi mchanganyiko na makzi kama inavyofanyika eneo la Kariakoo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;8)      Wizara yako, JIJI na Manispaa ya Kinondoni viyafanyie uchunguzi wa kina madai yote ya rushwa, ufisadi na ukiukwaji wa haki za binadamu vinavyodaiwa kutendwa na maafisa waliopewa jukumu la kutekeleza mradi huu kwa nia ya kuwabaini watumishi wasio waaminifu ili waondolewe wasiiendelee kuipaka Serkali matope mbele ya wananchi. (kama ilivyoelezewa katika barua ya wazi ya wananchi kwa mamlaka zinazohusika ya tarehe 03 Januari 2008 ambayo nimeiambatanisha)&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Imetolewa 16 Januari 2008 na:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;John Mnyika&lt;br /&gt;Mkurugenzi wa Vijana Taifa(CHADEMA) na Mkazi wa Jimbo la Ubungo&lt;br /&gt;0754694553</description><link>http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2008/01/taarifa-kwa-vyombo-vya-habari-waziri.html</link><author>UDI</author></item><item><guid isPermaLink='false'>tag:blogger.com,1999:blog-13876107.post-3487890244995569083</guid><pubDate>Mon, 14 Jan 2008 08:57:00 +0000</pubDate><atom:updated>2008-01-14T12:00:11.226+03:00</atom:updated><title></title><description>&lt;div align="justify"&gt; &lt;/div&gt;&lt;div align="justify"&gt; &lt;/div&gt;&lt;div align="justify"&gt; &lt;/div&gt;&lt;div align="justify"&gt;Majibu kuhusu Utamaduni wa Amani&lt;/div&gt;&lt;div align="justify"&gt; &lt;/div&gt;&lt;div align="justify"&gt; &lt;/div&gt;&lt;div align="justify"&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt;Prosper,&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nakubaliana na maoni yako, ndugu zetu wa Kenya hususani na Kibaki na Raila wanapaswa kuweka utaifa wao mbele na kutafuta suluhu ya mgogoro unaoendelea kufukuta huko. Na ni funzo kwetu wa Tanzania kwamba tufanye mabadiliko sasa kuhakikisha mifumo yetu ya uchaguzi na kisiasa inakuwa huru na inasimama mstari wa mbele katika kulinda haki na amani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huu ujumbe ameandika kaka Mwakatobe mwenyewe kwa mkono wake? Sitaki kuamini!Kila uhuru ana haki ya mawazo na fikra, lakini binadamu anapotoa mawazo tofauti na imani yake ambayo imezoeleka na wengi kuna haja ya kujiuliza maswali mengi sana. Nitaendelea kujiuliza. Ukipata wasaa wa kuonana naye naomba umwulize ana kwa ana kama ujumbe huu ameuandika yeye.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sidhani kama mwakatobe ambaye tulikuwa naye NYF miaka mingi nyuma kabla ya kuingia kwenye siasa- wakati huo tukiwa kwenye harakati tu za kawaida za kuhamasisha mabadiliko ya kiraia nchini, sidhani kama alikuwa na mawazo kama haya. Na kwa kweli binafsi nimepata nafasi ya kubadilishana naye mawazo kirafiki kabisa maeneo mbalimbali hapa dsm na hata nje ya mkoa- kuanzia nyumbani kwake mpaka kwenye vikao vya ndani. Ukimweleza hivi najua atakumbuka mengi sana! Kama ujumbe umeandikwa mwenyewe- basi binadamu ni kiumbe cha pekee sana! Nitajaribu kuingia katika kumbukumbu zangu kuona kama nipata maandiko yake ya wakati huo, ikiwemo ile itikadi/falsafa aliyokuwa akiitetea. Je, ni wakati huo ndio alikuwa akiandika alichokuwa akiamini au ni sasa ndicho anachokiamini, Je, ataendelea kuamini hivyo? Nini asili ya uongofu huu? Kwa kweli, nikianza kuandika kwa undani kumbukumbu hizo za zamani, tukio hata tukio, hatua hata hatua- kwa kweli nitajikuta naandika mambo mengine binafsi kabisa! Sitafanya hivyo. Na wala si nia yangu kuandika makala ya gazetini, sitafanya hivyo pia. Kwa kuwa siamini kama makala haya uliyonitumia ni fikra huru za kaka Gwandumi Mwakatobe!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nakubaliana na maandiko haya kwamba AMANI ni tunu ya muhimu sana, na inafaa kulindwa kwa gharama zozote. Nakubaliana pia kwamba Tanzania ina UTAMADUNI WA AMANI. Ila mwandishi alipaswa kujiuliza- Utamaduni nini? Je, utamaduni huweza kuzaliwa na kufa? Nini asili ya utamaduni wa amani katika Tanzania? Na yapi yanaweza kufanya utamaduni huo kutoweka?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Msimamo wa Kaka Gwandumi huko nyuma umekuwa ni kuwa Tanzania pamoja na kuwa tuna amani lakini kuna watanzania wengi hawana amani- na hali hii ya kukosa kwao amani inachangiwa pia na kukosa kwao haki, na wengine ni kutokana na hali mbaya ya maisha iliyozidi mipaka. Katika mazingira hayo msimamo wake wakati wote umekuwa kama ule wa Mwalimu Nyerere ambao pia ni msimamo ulioko kwenye Biblia ambayo Kaka Gwandumi amekuwa akiitumia kwa muda mrefu kwenye maandiko yake. Kwamba AMANI ni TUNDA la HAKI. Ndio maana sitaki kuamini kama msimamo huu mpya ni wa Kaka Gwandumi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nakubaliana na mwandishi katika utangulizi kwake kwamba njia za amani ndizo ambazo ni za kwanza kabisa, na za kistaarabu katika kufikia malengo ya kisiasa. Ila sikubaliani naye kwamba njia zingine ni njia ambazo madhara yake hayawezi kufutika milele. Naandika ujumbe huu leo Januari 12 ambapo Wazanzibar wameadhimisha mapinduzi ya umma yaliyomwaga damu kumng’oa sultani; Je, anataka kusema kwamba mapinduzi yale- yeye kama mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi, anayatangaza kuwa ni haramu na njia mbaya zaidi iliyowahi kutumika katika historia ya Taifa letu ambayo itasababisha visiwa vile visiwe na Amani milele? Afrika Kusini ilitumia muda mwingi mijadala na kujenga hoja huku makuburu wakitumia risasi za moto, ANC baadaye ikaazisha Umkotwo we Sizwe, jeshi lake hili ambalo lilifanya uharamia kwa serikali ya makuburu ikilenga miundo mbinu yao- ni harakati hizi ziliwarudisha makaburu kwenye meza ya majadiliano. Sisemi hivi kuhalalisha mapinduzi ya kijeshi; njia ambayo katika siasa za sasa za ustaraabu ni njia ya mbali kabisa. Nasema hivi kufuta hoja ya mwandishi, na mifano kwa kweli iko mingi sana duniani. Hawa wastaarabu wa demokrasia wa magharibi tunaowazungumzia leo, karibu kila taifa lao limepitia katika ushenzi usiomithilika kufikia katika ustawi walio nao sasa! Sisemi hivi kuhalalisha kwamba sasa tuwe washenzi, nasema hivi ili mwandishi wa makala haya ajaribu kutafakari kidogo- “Hivi kwa nini binadamu wanafikia hatua ya kuwa washenzi?”.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwandishi amejaribu kujenga hoja kwamba AMANI ndiyo kipeo cha yote. Na amani hiyo ndiyo ameiita URITHI MKUU WA UTAMADUNI WETU WA KISIASA. Kama nilivyosema, utamaduni huzaliwa, hukua na huweza hata kufa? Mwandishi ajiulize, ni mambo gani yanatishia kuua huu utamaduni? Niliwahi kuandika hapa baadhi ya mambo ambayo yanaweza kutishia kufa kwa utamaduni wetu wa amani, mambo ambayo baadhi hata Nyerere mwenyewe alishawahi kuyatabiri- bonyeza hapa kusoma andiko langu hilo:Jambo moja utabaini; &lt;/span&gt;&lt;a href="http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_15.html"&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt;http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_15.html&lt;/span&gt;&lt;/a&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt;  HAKI( kwa maana ya JUSTICE ambayo ni zaidi ya RIGHT); ni roho ya AMANI. Bila haki amani iko shakani. Haki ikitoweka, amani haiwezi kuishi hata kwa kuandika makala elfu na maelfu za propaganda kuhusu umuhimu wa amani katika nchi yetu. Namna ya kuendeleza uhai wa amani hiyo ni kuchambua, kukemea na kuondoa mizizi inayotishia haki za wengi. Mwandishi amesema AMANI ni urithi mkuu; lakini mwandishi anajua kuwa urithi ni jambo jema lakini si kila mrithi anauwezo wa kutunza urithi kama mwenye mali mwenye ambaye aliichuma kwa tabu hatua kwa hatua. Kauli ya kwamba huu ni urithi pekee haiwezi kulinda urithi huo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukiona viongozi wa serikali wanazomewa hadharani. Ukioana wananchi wanaanza kujichukulia sheria mikononi wenyewe. Huku viongozi na makada wakiendelea kuiamba AMANI,AMANI, AMANI! Wananchi wakiendelea kuimba HAKI, HAKI, HAKI!. Hizo ni alama za nyakati. Ni wakati wa viongozi na wananchi kukaa na kutafakari na kuzungumza lugha moja.  Si wakati wa viongozi na kikundi cha watu wachache kuwahubiria kile wasioamini. Tembelea maeneo ya migodi, pata hisia za wananchi. Jaribu kaa vijiweni, sikiliza wananchi wanazungumza nini kuhusu ufisadi na watawala wao. Mambo haya yatahitaji mchambuzi kama huyu, aliyeandika kurasa zote hizi kuyafanyia kazi kwa manufaa ya taifa letu. Na ni kwa kuchukua hatua ndipo tutakuwa kweli walinzi wa AMANI. Ni kwa kuamka, na kukemea aina zote za UBAGUZI, zinazoanza kujitokeza katika nchi yetu, ndipo tutadumisha Taifa lenye AMANI.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Umemkweza lakini wakati huo huo umemtweza Kinjeketile; niliwahi kuandika, tunu ya yangu kwa shujaa huyu:    &lt;/span&gt;&lt;a href="http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_13.html"&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt;http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_13.html&lt;/span&gt;&lt;/a&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt;  mwandishi wa uchambuzi huu kama naamini anajua historia ya nchi yetu pamoja na upotofu wote wa kihistoria uliofanyika. Anajua kwamba Kinjekitile ni mtu ambaye anapaswa kujengewa Minara kama ambavyo wakina Nyerere wanabigiwa baragumu! Wajerumani wametumia muda mrefu katika nchi yao mwaka jana kukumbuka vita vya Maji Maji, wanajua ni mapambano ya namna gani yalifanyika. Na mara baada ya Vita hivi utawala wa Kijerumani haukuwa tena katika hali ya awali hapa nchini. Falsafa ya maji, ilikuwa ni falsafa ya mapambano tu; lakini mbele yake waliokuwepo machifu na viongozi wengine wa kiafrika na wapambanaji wao waliokamata silaha. Mataifa ya wenzetu, chimbuko la uzalendo wao- ni harakati za watu kama hao. Lakini sisi tunawabeza! Uzalendo utatoka wapi? Uzalendo huchachushwa kwa moyo za hisia za kutazama mambo makubwa yaliyofanyika katika Taifa!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwandishi anajua kwamba Wajerumani ndio walikokuwa wakoloni halisi, huku waingereza ambao Mwalimu aliwakimbiza kwa Harakati za Ndani na Zile hotuba za umoja wa Mataifa kwa kuwa walikuwa na wadhamini tu. Najua mwandishi anayajua haya yote! Mwandishi anajua kwamba kama waingereza wangekuwa walowezi Tanganyika kama ilivyokuwa kwa Kenya ni wazi baada ya Maji Maji ingezaliwa Mau Mau nyingine hapa kwetu. Mwandishi anajua haya! Anajua kwanini tulipeleka vikosi vyetu vijana wetu wakapoteza damu kuleta ukombozi kusini mwa Afrika- Msumbiji, Angola, Afrika Kusini nk! Anajua haya. Hata Nyerere aliyajua haya, ndio maana hakupeleka njia za Amani na Maelewano huko(Non Violence Method); Nyerere aliyekuwa kiongozi aliyejua falsafa ya mapambano. Alijua adui anayetumia mbinu gani akabiliwe kwa mbinu gani!. Ndio maana hakutaka kukaa meza moja ya majadiliano na maelewano na Iddi Amini Dada! Unadhani Nyerere hakuwa anajua “urithi mkuu na utamaduni wetu wa kisiasa” za AMANI?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwandishi ametumia muda mrefu kujenga hoja kwamba WAPINZANI wanachochea vurugu, uhasama, ugomvi, matusi, kejeli nk na kwamba ndio wanaoelekea kuvunja AMANI nchini. Lakini mwandishi ameshindwa kutaja mifano ya kauli au matukio hayo na yalihusu wapinzani gani! Ujumbe huu, ukisomwa juu juu, waweza kuaminika na kuviza imani ya watanzania kwa watanzania wenzao walioko kwenye upinzani. Lakini tukumbuke, Mandela alipopinga ubaguzi aliitwa mpinzani mwenye kuvunja amani. Nyerere aliitwa na serikali ya mkoloni, mpinzani mwenye kuvunja amani na akashtakiwa kwa uchochezi. Mchambuzi mahiri kama huyu, angetumia muda kuvitaka vyombo vya dola kuchukua hatua kwa wapinzani hao kama kweli wanavunja amani ya nchi!. Mwandishi akumbuke kwamba, kwa mpinzani Dr Slaa alipojitokeza hadharani kusema ufisadi wa Benki Kuu(BOT) aliitwa majina yote ambayo mwandishi huyu ametumia kueleza tabia ya upinzani. Leo hii baada ya Rais Kikwete kuona ukweli wa mambo tena katika sehemu ndogo tu ya ukaguzi wa EPA; wale wote waliosema maneno hayo sijui kama wanajisikia AMANI mioyoni mwao! Ndio maana sitaki kuamini kama ameandika Kaka Mwakatobe ujumbe huu, kwa kuwa najua yeye anajua , na huwa anapenda sana kutumia biblia- na ndani ya kitabu hicho kuna simulizi ya Yesu ambaye naye aliitwa majina kama hayo na watawala wa wakati huo. Lakini leo wakristu wote kote duniani wanamuita jina tofauti kabisa!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Siasa za kistaraabu za kujenga hoja naziunga mkono! Siasa safi, za sera na hoja. Na ndio ambazo upinzani umekuwa ukifanya. Dr Slaa alianzia bungeni, akajaribu kutoa hoja ya awali ikapuuzwa. Akaongeza ukali zaidi wa maneno, hakueleweka. Akaongeza uzito zaidi kwa kuandaa hoja binafsi, akaletewa mizegwe. Na hapo ndipo alipotumia lugha kali zaidi, kwamba ‘hawa ni wezi na mafisadi’. Leo mpaka Kikwete naye ameanza kutumia lugha kali! Lugha ambayo miezi michache nyuma, mawaziri waliikebehi kama ambayo makala hii inakebehi upinzani!. Wote kati yetu, mtu akichukua mali- tutazungumza kwa ‘urithi wa utadamuni wetu wa kisiasa’, “Naomba nirudishie”; asiporudisha lugha gani hufuata?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwandishi ameendelea mbele kuonyesha nia ya maandiko yake pale alianza kujenga hoja kwamba Nyerere alisema ‘kiongozi bora lazima atoke CCM”; mwandishi anasahau ni Mwalimu huyu huyu alisema “CCM sio Mama yangu”. Mwandishi akasome maandiko ya mwisho mwisho ya Mwalimu Nyerere kwenye “Uongozi wetu na hatma ya Tanzania”; hakika hii kansa ya uongozi Nyerere alishaitabiri, na unaweza kubashiri kama angekuweo sasa na ufisadi angefanyaje! Kama kweli Nyerere aliamini kwamba “Kiongozi bora lazima atoke CCM”; Mwandishi anaweza kutuelezaje yaliyotokea kule Musoma baada ya mfumo wa vyama Vingi kuanza ambapo Baba wa taifa alimnadi wazi mgombea wa Upinzani Balozi Ndobho kwa ubora wake na kumuacha wa chama chake CCM? Watanzania tunapaswa kuwa na siasa zilizo juu ya vyama, zinazotazama zaidi maslahi ya Taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwandishi anajenga hoja kwamba dosari kuu ya upinzani ni kutaka wananchi wakichukie Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake! Mwandishi anajua kabisa kwamba wema ni sumu ya uovu. Kama CCM na serikali yake wanatenda mema, unadhani wananchi wanaweza kuchukia hata wapinzani wangesambaza chuki? Lakini kwa kuwa kuna UOVU unajaribu kufichwa ni wazi kwamba yoyote anayesema UKWELI, ataonekana ni mchonganishi na mchochea chuki. Wakina Dr Slaa, Zitto wote wanaitwa waongo, huku wakina Mbowe na wengine wakiitwa wachochezi, Wakina Kubenea wakimwagiwa Tindikali na wakina Ndimara Wakikatwa mapanga. Hiyo ndiyo AMANI! Bahati nzuri, watanzania wanaelewa, na ipo siku KITAELEWEKA!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Eti, kero ya wapinzani ni kuona CCM inazidi kuimarika na kukubalika! Ndio maana siamini kabisa kuwa haya ni maneno ya Kaka Mwakatobe. Mwandishi anasema watanzania hawafanyi utafiti kubaini ukweli huu, anasahau kuwa ni watanzania hawa hawa ndio wametoa maoni yao kwenye tafiti mbalimbali kwamba umaarufu wa CCM umeporomoka. Sio sababu ya chuki ya upinzani, ni kwa chama hicho kushindwa kutekeleza ahadi lukuki ilizotoa. Huu ni ukweli ambao mwanaCCM yoyote makini anaufahamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mchambuzi huyu anarudia kauli ya mara kwa mara ya kwamba wapinzani hawana DIRA- lakini mchambuzi huyu huyu anajua hazina ya sera ambazo CCM imekuwa ikichota kutoka upinzani kuanzia enzi za kufuta kodi za manyanyaso mpaka kipindi hiki cha kupitia mikataba ya madini. Mchambuzi huyu anajua kuwa “Maisha Bora kwa Kila Mtanzania” ni lengo tu la MKUKUTA ambao umeandaliwa na wananchi wote bila kujali itikadi na kuchukuliwa tu kwenye ilani ya Chama tawala. Mchambuzi amesahau kabisa kwa CCM imeshatelekeza falsafa na itikadi yake, na hata Mwalimu Nyerere amekiri hili kwenye kitabu cha Uongozi Wetu na Hatma ya Tanzania. Mwandishi angetueleza- DIRA YA CCM ni ipi? Mchambuzi mahiri kama huyu alipaswa awe anafahamu kabisa Dira na mwelekeo wa vyama vingine nchini. CHADEMA mathalani, mambo haya yamefafanuliwa Kwa CHADEMA falsafa na itikadi yake inapatikana hapa: &lt;/span&gt;&lt;a href="http://www.chadema.net/maoni/kijue.php" target="_blank"&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt;http://www.chadema.net/maoni/kijue.php&lt;/span&gt;&lt;/a&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt; na ilani yake ambayo utangulizi wake ni dira ya “Tanzania tunayoitaka” inapatikana hapa: &lt;/span&gt;&lt;a href="http://www.chadema.net/ilani/tanzania.php" target="_blank"&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt;http://www.chadema.net/ilani/tanzania.php&lt;/span&gt;&lt;/a&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt; na popular manifesto 2005 inapatikana hapa &lt;/span&gt;&lt;a href="http://www.chadema.net/maoni/ilani.php" target="_blank"&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt;http://www.chadema.net/maoni/ilani.php&lt;/span&gt;&lt;/a&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt; . Lakini Ndio maana sitaki kabisa kuamini kwamba aliyeandika ni Kaka Mwakatobe, kwa kuwa najua kabisa yeye alikuwa kwenye jopo la wataalamu waliofanya mapitio ya Sera na Katiba ya CHADEMA mwaka 2003/04. Wakati huo, mimi hata sikuwa mwachama wa CHADEMA. Kwa maneno mingine, najua Kaka Mwakatobe anafahamu vizuri asili ya Falfafa ya “Nguvu ya Umma”. Hivyo, sifikiri kabisa kwamba anaweza kusema upinzania hauna dira! Yeye anafahamu kwamba hata Mwalimu Nyerere aliwahi kusifia Sera za CHADEMA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bahati nzuri nilikuwepo CHADEMA mwaka 2005, na nilikuwa mgombea Ubunge wa Ubungo wakati huo; najua undani wa mambo. Mwandishi amezusha kwamba mwaka 2005 CHADEMA iliponzwa kwa kujipendekeza kwa wafadhili; wafadhili gani, kujipendekeza gani? Hapa mwandishi anataka kusheheneza hisia kwamba CHADEMA ilipewa mapesa kutoka nje na kuyatumia kwenye helikopta na kuwatelekeza wagombea wa ngazi nyingine. Bahati nzuri, ni CHADEMA pekee iliyotangaza wazi matumizi yake ya fedha katika kampeni.  Rejea Tamko la Baraza Kuu la CHADEMA hapa:   &lt;/span&gt;&lt;a href="http://www.chadema.net/uchaguzi/ripoti1.php"&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt;http://www.chadema.net/uchaguzi/ripoti1.php&lt;/span&gt;&lt;/a&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt; CCM mbona mpaka leo haijatangaza? Hapa imeelezwa wazi kiasi gani tulitumia, kiasi gani zilitumika kwenye helikopta. Lakini tulikwenda mbele zaidi kutangaza ni kiasi gani zilipatikana toka nje. Tuliweka wazi, kampeni zetu hajikuchangiwa kwa fedha toka nje- zimegharamiwa kwa ruzuku ya chama ni michango ya wanachama mbalimbali. Kitu pekee tulichopata toka kwa rafiki zetu wa nje ni ruzuku kidogo ya kuendesha warsha ya mafunzo kwa wagombea ubunge, na michango hii ya kiufundi haikutolewa kwa CHADEMA tu katika kipindi cha kuelekea uchaguzi. Mchambuzi huyu, angepaswa aandike uchambuzi wa kutaka CCM itangaze mapato na matumizi yake ya uchaguzi-na angeuliza vile vile, zile tuhuma za fedha za uchaguzi wa CCM kutoka nje ya nchi ambazo walisema wangelishitiki gazeti la nje lililofichua suala hilo zimefikia wapi? Kama mchambuzi huyu hafahamu tuhuma hizo- asome humu atazipata:   &lt;/span&gt;&lt;a href="http://www.chadema.net/habari/misc/misc_10.html"&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt;http://www.chadema.net/habari/misc/misc_10.html&lt;/span&gt;&lt;/a&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt; .Baada ya kuchambua hapa, atajua ni chama kipi cha siasa ‘kinajipendekeza’ kwa wafadhili wake wa wakati wa uchaguzi!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Inasikitisha kwamba mchambuzi kama huyu, anadiriki kudanganya kuwa CHADEMA ilikuwa ikitumia milioni 10 kwa siku kwa ajili ya helikopta! Huu ni uzushi kabisa. CHADEMA haijawahi kutumia milioni 10 kwa siku kwa ajili ya kukodi helikopta. Niliwahi kuchambua gharama za matumizi ya helikopta katika makala yangu iliyotoka katika vyombo vya habari vya nyumbani- makala hiyo inapatikana pia hapa: &lt;/span&gt;&lt;a href="http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2008/01/helikopta-ya-chadema-raha-karaha-au.html"&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt;http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2008/01/helikopta-ya-chadema-raha-karaha-au.html&lt;/span&gt;&lt;/a&gt;&lt;span style="font-family:verdana;"&gt;  .Ni vyema akajiridhisha na kusema ukweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mchambuzi huyu, anataka kujenga picha kwamba upinzani unapokea mabilioni mengi ambayo ingeweza kabisa kujenga zahanati, shule, hospitali nk ili kuonyesha kwa vitendo. Mchambuzi anataka kujenga picha kwamba vyama vya upinzani vinatapanya fedha! Mwandishi anashindwa kujua kwamba ruzuku ya vyama inatolewa kwa kazi maalumu za kisiasa ambazo sheria ya vyama vya siasa imeelekeza. Mwandishi anashindwa kujua kwamba michango mahususi inayotolewa inatolewa kwa kazi mahususi. Mchambuzi anashindwa kujua kabisa kwamba huwezi kupewa mchango wa kuendesha mafunzo wa viongozi ukapeleka kwenye kujenga zahanati pamoja na umuhimu wake. Kubwa kuliko yote, mwandishi anaashindwa kuelewa kazi ya vyama vya siasa- anashindwa kujua kwamba vyama vya siasa vinatoa sera na viongozi ili watumie vizuri rasilimali kuleta barabara, zahanati nk. Mwandishi anashindwa kujua kwamba michango ya wafadhili mbalimbali inapitia serikalini kutoa huduma za kijamii na kutekeleza miradi ya kimaendeleo- kazi ya upinzani ni kuiwajibisha serikali iliyoko madarakani na kutoa mwelekeo mbadala! Mwandishi anashindwa  kujiuliza mbona CCM inapokea ruzuku ya takribani bilioni mbili(milioni 2000) kila mwezi kutokana na fedha za walipa kodi, wakati CHADEMA inapokea milioni 56 tu kwa mwezi lakini CCM haijengi barabara, zahanati kutokana na ruzuku hiyo? Badala yake madarasa, zahanati nk zinajengwa kwa kodi za wananchi kupitia bajeti ya nchi, michango ya wananchi na fedha toka kwa wadau wa maendeleo? Ni kutokujua au kupotosha?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hili la kusaidia miradi ya kuthibiti umaskikini: Linahitaji mjadala zaidi, tujiulize- duniani kote, kazi ya vyama vya siasa ni nini? Imani yangu ni kuwa CHADEMA tumeweza kufanya vizuri katika miradi mbalimbali katika halmashauri ambazo tumeongoza Kigoma Ujiji, Hai na Karatu; na tuendelea katika halmashauri ambazo tumeanza kuongoza baada ya 2005, sasa tunaoongoza pia Halmashauri mpya moja ya Tarime. Sidhani kama upinzani unatakiwa kugawa fedha za miradi ya kuondoa umasikin- kufanya hivyo, kuna vikwazo vifuatavyo: Mosi, tutakuwa tunatoa takrima ya maendeleo kwa wananchi toka mifukoni mwa chama ambayo kimsingi ni rushwa, Pili, tutatoa fursa kwa mafisadi nao kuanza kutoa michango hiyo kupitia vyama vyao- sasa mwenye kisu kikali ndio atakula nyama. Tatu, tutakuwa tumetoka katika malengo ya msingi ya chama cha siasa. Kwa maoni yangu, chama cha siasa ni muunganiko wa watu wenye mawazo yanayoshabihiana kwa lengo la kuchukua dola ili kutekeleza mawazo hayo, na kabla ya kuchukua dola kuiwajibisha dola iliyoko madarakani kwa misingi ya mawazo hayo! Kwa hiyo bidhaa za vyama vya siasa ni 'uongozi', 'sera' na 'oganizesheni'. Kwa hiyo, tunaondoa umasikini kwa kutoa viongozi bora, sera bora na oganizesheni bora. Kwa sasa pamoja na kuwa upinzani tumewatoa wakina Dr Slaa, Zitto nk ambao wanaiwajibisha serikali kwa sera zinazopinga ufisadi na kutetetea rasilimali za taifa, kwa kweli matokeo ya harakati zao ni fedha zetu za kodi kutumika vizuri zaidi katika miradi ya kuondoa umaskini. Naamini kabisa, serikali ya sasa(pamoja na ufisadi unaoendelea) kwa staili hii ya Orodha ya mafisadi kila mmoja yuko tumbo joto- hivyo, sidhani kama watakuwa na ari, nguvu na kasi mpya ya kufuja fedha za miradi ya kuondoa umaskini kama ilivyokuwa wakati wa Mkapa- sasa kama hali ikiwa nzuri kiasi nani atanufaika kama sio mwananchi? Nani amesababisha manufaa hayo kama si upinzani? Na ikifika 2009 na 2010 changamoto kwetu ni kuwafanya watu waelewe kwamba wakituchagua sisi tutaingia wenyewe kutekeleza sera hizo vizuri zaidi tofauti na CCM inayofanya mambo machache tena baada ya shinikizo. Kama ni kutokujua, niliwahi kuandika hapa kazi chama cha siasa- na ni kwa vipi upinzani unasaidia maendeleo nchini: “Huduma za Kijamii zinazotolewa na Vyama Vya Siasa vya Upinzani. Akitaka naweza kumtumia hilo andiko. .Leo upinzani ukiwezesha bilioni 133 zilizofujwa BOT zikapatikana unajua ni madarasa, barabara na zahanati ngapi? Kati ya chama kutumia milioni 56 kufanya harakati za kisiasa za kupambana na ufisadi na kuokoa bilioni 133 na chama kutumia milioni 56 kujenga matundu ya choo nyumbani kwa wananchi wachache kipi bora?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndio maana siamini kama ujumbe huu umeandikwa na kaka Mwakatobe; najua anaujue Ukweli huu, na anajua kuwa UKWELI ni UHURU. Na anajua kwamba utumwa wowote unaosababishwa na jitihada ya kulinda maslahi binafsi na ni suala baya. Lakini anajua zaidi, kujaribu kuambikiza utumwa huo kwa kizazi cha baadaye cha Taifa hili ni DHAMBI. Na Ole wake yule ayakayesababisha mmoja wapo wa watoto hawa kutenda dhambi...................&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;JJ&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ps: Unaweza kuutuma ujumbe huu kwa Kaka Mwakatobe na marafiki zetu wengine, lakini usiupeleke kama makala ya kwenye gazeti kwa kweli. Sijafanya uhariri wowote wala kuweka mpangilio, nimeandika mawazo kwa kadiri yalivyokuwa yakitiririka. Heri ya Mwaka Mpya na wasalimie Kigoma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;/span&gt;&lt;/div&gt;</description><link>http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2008/01/majibu-kuhusu-utamaduni-wa-amani.html</link><author>UDI</author></item><item><guid isPermaLink='false'>tag:blogger.com,1999:blog-13876107.post-7529699523420254531</guid><pubDate>Sat, 12 Jan 2008 17:56:00 +0000</pubDate><atom:updated>2008-01-12T20:59:13.238+03:00</atom:updated><title></title><description>‘HELIKOPTA YA CHADEMA’: RAHA, KARAHA AU ‘SILAHA’?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na John Mnyika&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati wa uchaguzi mkuu 2005 “Helikopta ya CHADEMA” ilizua hamasa na mjadala mkubwa. Wako walioponda na wapo waliosifia. Mapema mwaka huu baraza kuu la CHADEMA lilitangaza kwamba chama kitaendelea kutumia helikopta kama moja ya vitendea kazi wakati wa utekelezaji wa mpango mkakati wa miaka mitano ya chama hiki. Wiki chache zilizopita vyombo kadhaa vya habari viliripoti kwamba CHADEMA inatarajia kutumia helikopta katika ziara yake ya kuwashukuru wananchi na kutekeleza baadhi ya mikakati ya chama huku chombo kimoja cha habari kikisema kwamba “Helikopta hiyo itakodiwa kwa dola 1200 kwa saa hivyo kwa saa 24 itakuwa dola za kimarekani 28,800 kwa siku. Hii ni sawa zaidi ya milioni 35 kwa siku”. Eti, CHADEMA itakodi helikopta kwa shilingi za kitanzania 35,000,000 kwa siku!. Hoja na maswali mbalimbali yametolewa kuhusu helikopta. Lengo la makala hii ni kujibu baadhi ya maswali na kupanua mjadala kuhusu matumizi ya helikopta. Wakati serikali ilipoamua kutumia magari ghali maarufu kama mashangingi, palikuwa na mjadala mkali. Wakati serikali iliponunua ndege ya raisi kwa takribani bilioni 40 mjadala ulikuwa kitu cha muhimu. Wakati serikali iliponunua rada ya kijeshi kwa gharama kubwa hutukuweza kuepuka kujadili kama walipa kodi. Kadhalika CHADEMA kama chama cha siasa kinaposemwa kinataka kutumia milioni 35 kwa siku kukodi chombo cha usafiri tunapaswa kwa kweli kukijadili. Tunawajibu huo kwa kuwa vyama vya siasa ni asasi za wanachama. Lakini pia ni asasi za umma kwa kuwa zinaendeshwa kwa pesa za walipa kodi kwa kiasi fulani. Hii ni kwa sababu ruzuku inayotolewa na serikali kwa vyama vya siasa vyenye wabunge na vilivyofikisha asilimia inayotakiwa ya kura inatokana na kodi za wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Si kweli kwamba gharama za kukodi helikopta ni shilingi milioni 35 kwa siku. Na kwa mtazamo wangu ni kwamba katika kufanya ziara mfulululizo za kisiasa katika nchi kubwa kama Tanzania helikopta ni nafuu kuliko magari na ndege. Najua wengi mtashangaa!. Huu ndio ukweli.  Helikopta nyingi duniani zinakodishwa kati ya dola 1000 na dola 2000 kutegemea aina, mwendo kasi, msimu nk. Uchaguzi 2005 CHADEMA ilikodi helikopta ya dola 1200 kwa saa.  Kwa kampeni zote zilizoratibiwa na makao makuu ya chama, CHADEMA ilitumia jumla ya Tsh milioni 750 na ushee. Kati ya hizo ni sh milioni 223 tu zilitumika kwenye helikopta. Na si bilioni 3 kama baadhi wanavyosema, na pesa hizi zilitoka wanachama na wapenzi wa chama humu humu nchini. Na kwa kweli CHADEMA inapaswa kupongezwa kwa kuwa wazi kusema imetumia shilingi ngapi na kuvitaka vyama vingine navyo viseme. CHADEMA iliviambia vyama vingine navyo viseme toka Mei sasa ni Disemba. Kimya!!!Bado wanaandaa mahesabu toka Disemba  mwaka jana uchaguzi ulipokwisha!.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nirejee kwenye mjadala wa helikopta!. Wasichojua watu ni kuwa helikopta, tofauti na vyombo vingi vya usafiri gharama zake za kukodi zinahesabiwa kwa muda ambao helikopta inakuwa hewani. Helikopta ikiwa chini hailipiwi gharama za kukodi. Wanachofanya tu ni kukupa kiwango cha chini kabisa cha kuruka kwa siku ambacho mara nyingi ni saa moja na kiwango cha chini kabisa cha siku za kukodi ambacho kwa mashirika mengi ni wiki moja. CHADEMA katika uchaguzi uliopita ilikuwa inatumia kati ya saa moja hadi mawili kwa siku!.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa tuchukue kadirio la juu- masaa mawili kwa siku, hii inafanya gharama kuwa dola 2,400 kwa siku. Mafuta ya ndege ni kati ya tsh 900 na 1200 kwa lita. Ila kwa uzoefu wanngu mafuta ya masaa mawili ni takribani asilimia 10 ya gharama za kukodi kwa hiyo ni dola 240. Jumla kwa siku ni takribani dola 2640, tufanye 2700 ili tuweze kufanya mahesabu kwa urahisi. Tukigeuza kwenda fedha za kitanzania hii ni sawa na takribani  2,970,000 kama dola moja ikiwa shilingi 1100 .&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa hiyo gharama ya CHADEMA kukodi helikopta kwa siku ni shilingi hata tukimbandisha kupindukia milioni 3 tu. Ukifanya mikutano 8 kama ambavyo Mbowe alikuwa akifanya kwenye uchaguzi 2005 kwa siku hii ni sawa na wastani wa kadirio la juu wa shilingi laki nne kwa mkutano mmoja. Laki nne kwa mkutano mmoja wa mgombea urais. Hizi ni pesa kidogo. Mkutano uliofura watu ambao wamekuja wenyewe bila kubebwa na FUSO wala mabasi wala kuletwa kulipwa posho wala kuja kwa kupewa fulana na kofia. Wanakuja kwa ridhaa yao. Hii ni kuwa very cost effective(umakini katika gharama)! Iliwahi kusemwa kwamba Naambiwa mkutano mmoja wa kikwete wa Jangwani uligharimu tsh milioni 20. Hii ni sawa na mikutano mingapi ya helikopta? Gharama za kukodi ‘shangingi’ moja kwa siku ni dola 200. Hii ni sawa na 1/6 ya kukodi helikopta kwa gari moja tu!. Kikwete alikuwa na msafara wa mashangingi mangapi katika msafara wake wa kampeni? (watasema aliyanunua- sawa sasa tuyahesabu katika rate ya kukodishwa!). Haishangazi katika maeneo walikuwa wakitumia mashangingi ya serikali. Msafara wa magari mengi unahitaji watendaji kiasi gani? Kama kila mmoja akilipwa posho ya kati ya 20 na 30 jumla ya gharama kwa siku ni kiasi gani? Kikwete na Shein walikuwa wavuki kwa magari pekee  mkoa hadi mkoa. Walikuwa wakitumia ndege ya serikali. Eti walikuwa wanaikodi. Ndege ya serikali kukodi ni bei gani kwa safari? Inatofauti gani na helikopta? Lakini je, ndege inaweza kutua kijijini na kufanya mikutano kama nilivyosema? Haya ndiyo mambo yanayohitaji mjadala!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo wanaotoa hoja kwamba helikopta inafika maeneo machache tu. Ukweli ni kuwa helikopta inafika maeneo mengi hata yale yasiyofikika kirahisi. Katika uchaguzi uliopita CHADEMA ilitumia magari katika awamu ya kwanza ya kampeni. Tukapata uzoefu wa kutumia magari katika kampeni za urais. Kumbuka hii ilikuwa ni mara ya kwanza kusimamisha mgombea urais. Katika awamu ya pili na kuendelea CHADEMA ilitumia helikopta. Mosi, Baada ya kuanza kutumia helikopta CHADEMA ilikuwa na uwezo wa kufanya wastani wa mikutano 8 kwa siku. Hii ilifanya Mbowe awe mgombea aliyefanya mikutano mingi kuliko mgombea mwingine yoyote tena katika maeneo yenye utofauti mkubwa wa umbali. Pili, CCM ni wajanja, siku za kampeni(kabla ya muda kuongezwa ni around 70) wakati ambapo nchi ina wilaya zaidi ya 130 na majimbo zaidi ya 230. Mgombea urais anayetumia magari kufanya mkutano mmoja kila wilaya kwa siku hawezi kumaliza nchi nzima katika kipindi hiki kifupi cha kampeni. CCM  inatumia ‘faida’ ya kuwa na wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa nakadhalika kuziba mapengo na kuwa na ‘nguvu ya ziada ya kushindana’(competitive edge). Njia moja ya kuwazidi kete ni kutumia helikopta kwenda maeneo tofauti kwa haraka. Tatu, CCM imeshindwa katika miaka zaidi ya 45 ya utawala wake imeshindwa kuweka mtandao mzuri wa barabara mpaka vijijini kabisa. Hiki ni kikwazo cha wagombea wa uraisi kufika kila mahali. Yapo maeneo ambayo mpaka sasa wanadhani Nyerere bado ni rais. Hapafikiki kirahisi. Helikopta ilikuwa na makawa na jenerata ndogo. Ipo mikutano ambayo ilifanyika vijijini kabisa ambapo ingekuwa ngumu kufika kwa magari katika wakati mwafaka. Huku ni kuwafikishia ujumbe wa mabadiliko wananchi waliopembezoni kabisa!. Sasa itatumika tena kuchambua mwaka mmoja serikali imefanya nini na imeshindwa kufanya nini na kuwahamasisha uwajibikaji na kusambaza  ‘TUMAINI JIPYA’. Hii ni kwa manufaa kwa Taifa zaidi ya vyama..&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo waliotoa hoja kwamba helikopta imekuwa ikimbeba Mbowe pekee na kwamba inawakosesha fursa viongozi wengine kuhutubia mikutano. Si kweli kwamba helikopta ilimbeba Mbowe pekee. Helikopta inategemea ukubwa. Ile ambayo CHADEMA ilikodi katika uchaguzi 2005 ilikuwa na uwezo wa kubeba abiria 3 na rubani. Kwa hiyo kupanga ni kuchagua, unaamua tu kuchagua ni viongozi wangapi wapande. Kwa hiyo alikuwa akipanda Mbowe, mratibu wa ziara ya helikopta ambaye humsaidia pia rubani kutambua maeneo na nafasi ya kiongozi mmoja. Hapa ilitegemea mahali. Yapo maeneo ambayo alipanda mgombea mwenza, yapo maeneo ambayo mgombea wa eneo husika wa ubunge alipanda na yapo maeneo ambayo kiongozi wa chama wa eneo husika alipanda. Kwa hiyo ilifanyika kutokana na hali na mahali. Binafsi nilipanda helikopta ilipokuja Ubungo- tulitua Kimara, Mbezi, Mabibo, Urafiki na kadhalika. Nilipanda kama mgombea ubunge wa jimbo la Ubungo katika mwaka 2005. Kwa hiyo wagombea wanaosema helikopta ni ya Mbowe pekee ni wazushi. Tatizo ni kuwa ilikuwa ukitaka kupanda helikopta lazima uache jimbo lako uende kuipandia katika jimbo ambalo mkutano wa mwisho unafanyika kabla ya kufika kwako. Kwa hiyo wapo waliamua kubaki jimboni kwao waisubiri ije wampokee mgombea urais. Ilikuwa ni suala la kuchagua tu. Lakini  kupanda helikopta ni nini mpaka watu wagombanie? Kiongozi wa chama wa eneo husika anapaswa kuwa uwanjani akimsubiri mgombea wake wa urais au kiongozi wa kitaifa afike ampokee, hizo ndizo itifaki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo wanaotoa hoja kwamba hizo pesa zilizotumika kwa ajili ya helikopta zingepelekwa katika matumizi mengine. Nyerere aliwahi kusema, kupanga ni kuchagua. Hizo milioni 200 na ushee zilizopelekwa katika helikopta zingepelekwa katika matumizi mengine zisingeleta kishindo kama ambayo imeletwa na helikopta. Kupanga ni kuchagua. Lakini, kama ni kupelekwa maeneo mengine shilingi milioni 500 zilipelekwa katika maeneo mengine  mathalani mabango, vipeperushi, vyombo vya habari, kusaidia wagombea ubunge katika maeneo ambayo chama kilikuwa na uwezekano mkubwa wa kushinda kwa mujibu wa tathmini ya vikao vya huu vya chama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo wanaosema helikopta ni ‘raha mustarehe’ hivyo ni ishara ya Mbowe na CHADEMA kupenda anasa. Ukweli ni kuwa helikopta ni suluba, helikopta ni kazi. Kwa yoyote aliyewahi kupanda helikopta ya polisi ambayo inashabihiana na ile iliyotumiwa na CHADEMA anajua kuwa kupanda helikopta ni kuweka roho rehani kama sio hewani. Helikopta inaleta suluba ya kuongeza idadi ya mikutano, binafsi nampa pole Freeman kwa kuhutubia mikutano mingi namna hiyo kwa siku. Huyu jamaa angekuwa ‘kimeo’ angeanguka siku nyingi sana! Lakini jamaa alikuwa wima siku zote za kampeni. Sijasikia ameanguka jukwaani. Helikopta ni chombo cha kazi. Helikopta tunayotumia haina kiyoyozi kama mashangingi, haina viti vinavyofanana na masofa kama mashangingi. Haina raha kama ndege ya serikali wala haina anasa kama ndege ya rais. Hakuna wahudumu ndani wala ratiba ya kupewa juisi na keki. Karaha ya helikopta ni harufu ya moshi na vumbi la upepo mkali unaposhuka. Ni ishara ya mapambano na harakati!. Ni ‘silaha’ ya vita vya kidemokrasia dhidi ya mfumo mbovu wa utawala unaopenda anasa!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo wanaojenga hoja kwamba Tanzania bado haijafikia ngazi na hadhi ya viongozi wake wa vyama vya siasa kutumia helikopta.Lol, salaale! Huku ni kujidharau. Wakenya jirani zetu hapo wanatumia helikopta mpaka kukagua mashamba. Ile helikopta ambayo CHADEMA ilikodi pamoja na kurudi kufanyiwa matengenezo ilitumiwa pia na watu wa mashindano ya magari. Ni helikopta ilitumika kuhamasisha wananchi kwenye vuguvugu la chungwa(ODM) kuhusu katiba Kenya. Lazima tuwe na viongozi wenye kuona mbali na kujua nini tunastahili kwa raslimali tulizonazo!. Hatuwezi kuwa na chama kinachoona jembe la mkono ndio halali yetu tukipanda kidogo eti tutumie plau na mikokoteni ya kukokotwa na ng’ombe. Tunapaswa tuwe na uwezo wa kufikiri ‘nje ya boksi’.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo wanaosema kwamba suala la kutumia helikopta ni uamuzi binafsi wa Mbowe. Ukweli ni kuwa helikopta ni mkakati wa CHADEMA sio wa Mbowe. Uamuzi wa kutumia helikopta ulifanywa na baraza kuu la chama na kuridhiwa kwa kauli moja na mkutano mkuu wa CHADEMA. Sio uamuzi wa Mbowe ule!. Hata baada ya uchaguzi, baraza kuu lilikaa tena kutathmini na kwa kauli moja walipongeza matumizi ya helikopta na kupitisha azimio la kuendelea kutumia helikopta. Kwa hiyo helikopta ni mkakati na utamaduni wa CHADEMA. Helikopta inatarajiwa kutumika tena kwenye ziara TUMAINI JIPYA. Lakini helikopta ni njia moja tu inayotumiwa na viongozi wa kitaifa kwa kipindi fulani kwa nia fulani ya kisiasa!Kuwafikia wananchi wengi kwa muda mfupi na ujumbe mahususi. Ipo mikakati mingine, mathalani  „CHADEMA ni Msingi“, kama ni jeshi basi huu ni mkakati wa vikosi vya ardhini. Wa chini kwa chini!. Huu unahusisha kutuma vikosi vya makada na viongozi wa kitaifa kufanya mikutano midogo ya hadhara katika kijiji na mitaa na kuingia mikutano ya ndani kutoa mafunzo na kujenga netweki au oganizesheni ya chama nganzi ya chini kabisa!. Huu utaanza mara baada ya helikopta ‚kulipua mabomu’ ngazi ya juu. Hii ni sayansi ya vita vya kisiasa....hii ndiyo vita ya kidemokrasia ya kuhamasisha nguvu ya umma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo waliosema kwamba ‚mtoa ujumbe kwa kutumia helikopta hufika na ujumbe wake na kuondoka na ujumbe wake’. Ukitaka kujua kuwa ujumbe wa helikopta ulileta hamasa angalia jinsi ambavyo wagombea walikuwa wakiweweseka baada ya helikopta kupita maeneo yao. Utakuwa huwatendei haki watu wa Tarime kwa mfano kuwaambia kwamba baada ya Helikopta kupita na Mbowe kumwaga maneno alipoondoka walisahau kila kitu. Ingawa nakubali kuwa kuna baadhi ya maeneo CHADEMA ilisia mbegu katika jangwa na pengine katika magugu. Ni hadithi ya mpanzi! Ndio maana sasa CHADEMA imeamua kujikita katika kusuka vizuri na upya uongozi wa chama ngazi ya chini. Tunaanza uchaguzi kuanzia msingi, tawi na kuendelea mpaka taifa kuanzia uchaguzi wa mwakani. Watanzania wategemee chama kuongeza nguvu. Tunachotaka ni  nguvu na mamlaka ya umma.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ila suala la muda wa kuzungumza naamini linastahili kuzingatiwa. Kwa hiyo katika awamu ya sasa nategemea kwamba mikutano ya helikopta itahusisha  saa si chini ya moja kwa kila mkutano kwa mzungumzaji mkuu kuweza kuzungumza. Kwa maneno mengine sasa badala ya mikutano nane na zaidi kwa siku itapaswa kufanyika mikutano kati ya minne na mitano tu kwa siku. Hakuna kulala mpaka Kieleweke. Watoto wa kijiweni husema, huu utakuwa ni wakati wa makamuzi ya kufa mtu!.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo wanaosema kwamba watu hufika kushangaa helikopta tu! Kuna rafiki yangu mmoja hupenda kujibu hoja hii kwa mzaha kwamba, unaweza kuja kushangaa ndevu za shekhe ama padri lakini kwa dakika tano unazomsilikiliza ukaona TUMAINI JIPYA. Hivi!, tunawafanya watanzania washamba kiasi hiki kiasi kwamba hawajui kuchagua jema na baya.....wapo washangaaji-nakubali, lakini wapo pia ambao yanayozungumzwa huwasukuma kuamua.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wapo viongozi na wagombea wachache wanaojitoa katika upinzani na husema kwamba wanajitoa eti kwa kuwa Mbowe anatumia helikopta badala ya kutoa pesa kwao. Wahenga husema „Mbaazi zikikosa maua husingizia jua’! &lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukweli ubaki pale kwamba helikopta ina wapenzi na washabiki wengi. Inapondwa zaidi na viongozi wa juu hususani wa CCM kama sehemu ya mikakati ya kuichafua CHADEMA na kuchochea migogoro. Hivi majuzi tu wakati wa uzinduzi wa mikakati ya CCM katibu mkuu wa chama hicho alisikika ‚live’ akisema kwamba waachane tu waruke na helikopta wakati sisi tunazindua mikakati. Bila kukumbuka kwamba CHADEMA ilitangulia kuzindua programu yake ya miaka mitano katikati ya mwaka juzi kabla ya CCM kufanya hivyo wiki iliyopita.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Najua wapo pia wachambuzi wachache wanaoponda matumizi ya helikopta lakini najua bi kutokana tu na kutopata siri za upande wa pili wa shilingi kuhusu helikopta. Lila na fila havitangamani asilani.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ukweli ni kwamba helikopta ni chombo tu kinachomwezesha mwanasiasa wa kitaifa katika nchi kubwa na yenye miundo mbinu duni kama ya kwetu kufika katika maeneo mengi na pengine hata yasiyofikika kwa muda mfupi na kwa gharama nafuu. Helikopta ni ubunifu na ishara kwamba CHADEMA ingekuwa madarakani ingetumia ubunifu mwafaka mathalani hata katika kuleta umeme, badala ya kuja na ‚ubunifu wa RICHMOND.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwandishi wa makala hii ni Mkurugenzi wa Vijana wa CHADEMA anayepatikana kupitia &lt;a href="mailto:mnyika@yahoo.com"&gt;mnyika@yahoo.com&lt;/a&gt; , www.chadema.net na 0754 694 553</description><link>http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2008/01/helikopta-ya-chadema-raha-karaha-au.html</link><author>UDI</author></item><item><guid isPermaLink='false'>tag:blogger.com,1999:blog-13876107.post-116983602501184235</guid><pubDate>Fri, 26 Jan 2007 18:20:00 +0000</pubDate><atom:updated>2007-01-26T21:27:05.050+03:00</atom:updated><title></title><description>PROFESA MSOLLA : SULUHISHO LA MIGOMO NI KUTOA HAKI KWA WANAFUNZI&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na John Mnyika&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi karibuni, akiwa mkoani Mbeya katika majumuisho ya ziara yake ya vyuo vikuu. Waziri wa Sayansi teknolojia na elimu ya juu, Mh Prof-Peter Msolla, alinukuliwa na vyombo vya habari akitoa vitisho kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kwa madai kuwa wanafunzi wanaohusika na migomo vyuo vikuu wanajiandalia mikosi na kwamba hawatapata ajira  baada ya masomo yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Prof Msolla ametoa kauli hiyo huku kukiwa na vuguvugu la wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kupinga taratibu za sasa za utoaji mikopo ambapo kwa mujibu wa taratibu za sasa ambazo kimsingi zinakinzana na sheria halisi ya mikopo. Pamoja na mapungufu mengine ya msingi  ni kwamba wanafunzi wanalazimika kuchangia asilimia 40 ya gharama za masomo. Na sasa vuguvugu hili huenda likasambaa zaidi wakati wowote kwani mpaka sasa kuna taarifa kuwa baadhi ya wanafunzi katika baadhi ya vyuo  wanashinikizwa kuchangia pesa hizo ambazo ni kati ya laki 3 na zaidi ya laki 5 ili waruhusiwe kuingia darasani sambamba na kupewa huduma zingine za msingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Aidha, hivi karibuni, vyombo vya habari vimeandika kwamba wanafunzi wa Chuo cha Kilimo Sokoine (SUA) waliendesha mgomo na kuja wizarani kutaka kuonana na waziri kupinga utaratibu wa kuchangia asilimia 40 ya mkopo. Pesa hizi ni takribani laki 5 ambazo walipaswa kuzilipa kabla ya kuanza masomo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Imeelezwa kuwa serikali imewataarifu kuwa wasaini mikataba na kuendelea na masomo. Uamuzi huu unaweza kutafsiriwa kuwa tayari serikali imewasaidia wanafunzi hawa kuendelea na masomo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini ukweli ni kuwa huu ni mtego. Ni wazi kwamba serikali ama inasubiri kipindi cha karibu na mitihani ndipo iwabane wanafunzi kwa kuwataka kulipa hiyo asilimia 40 au inaweza kuwaruhusu wafanye mitihani na pindi watakapokwenda likizo ikatoa maelekezo kuwa wasiolipa wasirejee mpaka watakapopata pesa za kulipa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Huu ni mkakati wa ‘wagawe uwatawale’ (divide and rule) ambao serikali imekuwa ikiutumia mara kwa mara kuvunja mshikamano wa wanafunzi. Na hii inathibitika kutokana na kauli ya Waziri wa Elimu ya Juu, Prof Msolla ambaye amenukuliwa na gazeti la Uhuru la Januari 17 akisema kwamba serikali haina mpango wa kulipa hiyo asilimia 40 kwa kuwa wanafunzi walikwishasaini fomu za mikopo na kwamba sharti hilo lilikuwa sehemu ya mkataba. Waziri anasahau kuwa fomu hizo zilishasainiwa na wanafunzi chini ya shinikizo la serikali pamoja na ahadi mbalimbali kwamba serikali iko mbioni kuandaa utaratibu mzuri zaidi. Tunachotaka ni serikali kutoa tamko kwamba itahakikisha kwamba utaratibu huu unafutwa kwa kutenga pesa katika bajeti ya mwaka huu ikiwemo za kulipia gharama za wanafunzi walioko masomoni hivi sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni katika muktadha huo, tunapaswa kulijadili suala hili ili kuhakikisha serikali inafika mahala inakiri kuwa mikopo sio hisani , ni haki ya kila mtanzania anayepata udahili wa chuo kikuu kwa mujibu wa sheria inayounda bodi ya mikopo. Na kwa mantiki hiyo  tunasisiza msimamo wetu katika misingi ifuatayo;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Migomo na Maandamano ni moja ya njia halali katika kudai haki.&lt;br /&gt;Kauli ya Mh Waziri ni kama vitisho  ambavyo vilikuwepo hata wakati wa serikali ya mkoloni wa kizungu  kuwadhibiti wanafunzi wanao nyanyaswa na serikali yao wasipisisimamie haki yao kwa vigezo kwamba kufanya hivyo ni kujihatarishia mazingira ya ajira punde baada ya kumaliza masomo yao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunapaswa kutambua kuwa nguvu ya umma ni hatua ya mwisho katika kuhakikisha umma unapata haki yake stahiki kutoka kwa serikali isiyojali. Migomo na maandamano   ni hatua ya mwisho inayorejesha wadau katika meza ya majadiliano baada ya hatua za awali za majadiliano kutokuzaa matunda.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Maandamano na mashinikizo ya hali ya juu kutoka kwa wanafunzi wenyewe dhidi ya serikali ni mambo yasiyoepukika kama hatua ya mwisho kwani serikali yetu imekuwa na tabia ya kutowatendea haki wanafunzi kila wanaponyanyaswa mpaka wanapoamua kusitisha masomo kwa migomo na maandamano.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivyo kwa kuwa serikali imejenga tabia ya kutowasikiliza wanafunzi wa elimu ya juu mpaka wagome na kuandamana, Na kwakuwa migomo na maandamano ni njia zinazoruhusiwa kwa mujibu wa mikataba ya kimataifa ya haki za binadamu, katiba ya nchi na sheria za taasisi mbalimbali ikiwemo vyuo vikuu kama moja ya njia ya kushinikiza haki kutendeka. Hivyo si ajabu kwa wanafunzi wa elimu ya juu kufanya kila linalowezekana ikiwa ni hata kugoma na kuandama kwa mujibu wa sheria ili kuhakikisha haki yao inapatikana, inalindwa na kuheshimiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Jumuiya ya wasomi kama vyuo vikuu kuacha haki yao inyongwe kwa hofu ya kitambo,  tena isiyo na ukweli wowote ni mfano mbaya wa namna wasomi wanaotarajiwa kuwa mstari wa mbele kupigania mabadiliko ya msingi ili nchi hii ikombolewe wanavyoweza kudhulumiwa haki yao mbele ya umma unao watazama kama majemedari na wakombozi watarajiwa.! Ni usaliti wa hali ya juu.! Ni usaliti kwa nafsi zao, ni usaliti kwa taifa lao.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndio maana natoa rai kwa Mh Waziri kuacha vitisho, na badala yake ahakikishe wanafunzi wanapata haki yao kama kweli ni msomi mzalendo. Hakuna binadamu anayependa kugomagoma wala kuandamana. Serikali isiwaweke wanafunzi katika mazingira yanayowalazimisha kugoma na kuandamana.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Haiingii akilini kwa mwanafunzi kutishwa kuwa asigome na wala kuandamana kwa madai kuwa kufanya hivyo kunahatarisha ajira yake hapo baadae wakati ukweli ni kwamba  mwanafunzi asipogoma hatopata mkopo, na asipopata mkopo  atafukuzwa chuo, hatomaliza Chuo. Sasa kama  hatopata mkopo na kushindwa kumaliza chuo, ni ajira gani ambayo Msola anasema wanafunzi wanahatarisha ?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mapungufu ya sera na utekelezaji wa sera ya mikopo.&lt;br /&gt;Utaratibu wa sasa wa mikopo una mapungufu  mbalimbali ya kimsingi ambayo yanaleta mkanganyiko wa hali ya juu katika taifa hili, na zaidi unatishia mustakabali wa elimu hiyo kwa wanafunzi wa kitanzania wanao toka familia masikini.&lt;br /&gt;Mosi ; Dhana ya uchangiaji wa gharama za elimu ya juu imegeuzwa kuwa mfumo wa kufanya elimu ya juu nchini kuwa bidhaa inayouzwa  badala ya huduma (service). Dhana nzima ya uchangiaji gharama za masomo ya elimu ya juu imepotoshwa , Kwa mujibu wa sera ya serikali , Mwanafunzi anatakiwa kuchangia asilimia 40 na serikali kumchangia asilimia 60 ya mkopo wote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Lakini kinachotokea ni kwamba, wanafunzi wanapewa mkopo wa asilimia 60 (huu ni mkopo sio mchango kwani watalipa), na baadae mwanafunzi anatakiwa kujilipia mwenyewe asilimi 40 ya gharama zinazobaki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hivi katika muktadha huu, serikali inawezaje kusema kuwa inawachangia wanafunzi kusoma elimu ya juu ? Hii ni cost sharing ya namna gani ? .Kilichopo hapa ni mwanafunzi kujilipia asilimia 100 za gharama za masomo yake (total cost bearing).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili ; Dhana ya kutoa mkopo kwa wanafunzi waliofaulu kwa  daraja la kwanza wavulana, na la kwanza na la pili wasichana ina mapungufu ya msingi. Kwanza inapingana na sheria ya mkopo kuwa kila atakayekidhi vigezo vya mkopo ikiwa na maana ya kupata usajili/udahili wa chuo na kuhakikisha kuwa hana uwezo wa kujisomesha atapatiwa mkopo. Kinachozungumzwa hapa ni  kufikia viwango vya kusajiliwa/kudahiliwa  chuoni na sio utaratibu wa madaraja kama ulivyoelezwa hapo juu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya upinzani kutoa msukumo katika suala hili, serikali ilirudi nyuma kidogo na kuamua kutoa mkopo kwa baadhi ya wanafunzi wa daraja la pili wavulana na la tatu wasichana ambao wengi wao walijiunga na ualimu. Hii ni kwa mujibu wa kauli ya Mh Rais kuwa pamoja na serikali kuwaruhusu baadhi ya wanafunzi wa daraja la pili wavulana, na la tatu wasichana, lakini bado vigezo vilivyowekwa katika fani mbalimbali ni kikwazo kwa wanafunzi hawa kujiunga na vyuo husika.(mathalani katika fani za udaktari na uhandisi).&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Vigezo vilivyowekwa vilizingatia uhaba wa  fursa zilizopo kwa msingi wa ni kiwango gani serikali imepanga kutoa mkopo katika fani fulani. Kwa mantiki hiyo, serikali inapotoa tamko kuwa imewaruhusu wanafunzi wa daraja la pili wavulana na la tatu wasichana katika fani chache, bila kuhakikisha vigezo vinabadilishwa, ni sawa na kutoa haki ambayo haipo. Ni kuwafanyia ‘usanii’ vijana wake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ni vyema Mh Rais atambue hilo, lakini pia atafiti kuhusu ukweli wa kauli yake kuwa serikali inasomesha wanafunzi waliofaulu vizuri kabisa kwa madai kuwa  serikali haiwezi kuwekeza kwa wanafunzi wasio na uwezo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nasema hivyo kwa sababu kuu mbili : Kwa upande mmoja, kuna wanafunzi wengi wanao faulu kwa kiwango cha chini kutokana na mazingira ya shule wanazosomea, mifano dhahiri ni shule za serikali na zile za umoja wa wazazi wa CCM, shule hizi nyingi hazina walimu wala vifaa, mwanafunzi anayepata daraja la tatu au la pili katika shule za aina hii anao uwezo mkubwa wa kujifunza kuliko wanafunzi wengi wanao soma katika shule za kimataifa, seminari na baadhi ya shule za sekondari chache za serikali ambazo zinafaulisha vizuri.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande mwingine, Kauli hii imekuwa ikithibitishwa na maprofesa wanaofundisha vyuo vikuu kwa kubainisha wazi kuwa wanafunzi wengi wanaofanya vibaya vyuo vikuu ni wale wanaotoka shule zenye majina makubwa ambao waliingia kwa alama za juu. Kwa maana hiyo basi, hoja ya Mh. Rais kumchukulia kila mvulana aliyepata daraja la pili na kila msichana aliyepata daraja la tatu hawezi kufanya vizuri sana, ina  mapungufu hayo ya msingi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatu ; Dhana ya kwamba waliopata daraja pili wavulana, na la tatu wasichana kuwa ndio wenye uwezo wa chini kitaaluma, na kwa hiyo wataenda ualimu ni kielelezo kuwa , serikali yetu inaamini Ualimu ndio taaluma isiyohitaji utaalamu sana, na hivyo haihitaji watu wenye uwezo  mkubwa. Kitu ambacho kimewahi kurudisha maendeleo ya taaluma nchini kwa miaka kadhaa sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nne ; Mwisho lakini kubwa zaidi ni kwamba chama tawala CCM katika ahadi zake wakati wa kampeni iliahidi kuhakikisha inawapatia mkopo wanafunzi 30,000 kwa mwaka. Hata hivyo waliofaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza mpaka la tatu ni wanafuzi 21,000 tu. Hivyo kama serikali ingekuwa inatekeleza ahadi zake wanafunzi wote wangepata udhamini wa chuo kikuu. Hata hivyo zaidi ya nusu ya hao , ambao walikidhi vigezo vya mkopo hawakupata mkopo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rai yangu kwa serikali, namuomba tena Mh Rais amshinikize waziri wa elimu ya juu , aufahamishe umma wa Tanzania ni kwa kiwango gani serikali yako imeshindwa kutimiza ahadi uliyoitoa wakati wa kampeni.  Na pia serikali ieleze ni wanafunzi wangapi walistahili mkopo kwa mujibu wa sheria lakini wamekosa na sasa inaandaa utaratibu gani kuhakikisha walikosa mwaka 2006 watapewa haki yao mwaka 2007, na kwamba mwaka 2007 kosa halijirudii na kwamba ahadi ya Mh rais itatekelezwa. Ili serikali iweze kutekeleza ahadi yake inapaswa kutenga si chini ya bilioni 195 kwenye bajeti ya mwaka huu kwa ajili ya mikopo. Hii inawezekana, kwani  kama tunaweza kutenga bilioni 272 katika miradi yenye utata kama mkataba wa RICHMOND, inashindwaje kusikiliza matakwa ya wananchi ya kufanya suala la elimu kuwa kipaumbele ? Kama Mfanyabiashara mmoja wa kitanzania anaweza kutuhumiwa kupata shilingi bilioni 15 ambayo ni sawa na milioni elfu 15 kama ‘hongo ya asilimia 30’ kwenye ununuzi wa RADA tunaweza kweli kusema hatuna pesa za kusomesha wanafunzi elfu 15 wanaohitaji takribani shilingi milioni moja kwa mwaka ?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwelekeo wa elimu ya juu nchini.&lt;br /&gt;Kwa ujumla kadri miaka inavyokwenda, na awamu za  utawala wa CCM zinavyobadilika, ndivyo mwenendo wa elimu ya juu nchini unavyozidi kwenda kombo, na zaidi unaelekea kujenga matabaka ya  masikini wasio na haki ya kupata   elimu dhidi ya matajiri wenye uwezo wa kununua elimu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Itakumbukwa kuwa katika awamu ya kwanza ya serikali ya TANU, na baadae CCM ya wakulima na wafanyakazi chini ya Hayati Baba wa Taifa. Mwl Julius Kambarage kwa mtazamo wa siasa ya ujamaa, wanafunzi wote walisomeshwa bure chuo kikuu. Walipewa mahitaji yote ya msingi kwa mwanafunzi kuweza kusoma. Mwalimu aliweza kuwapatia watoto wa wakulima na wafanya kazi masikini elimu ya bure bila hata ya kuuza migodi, hifadhi za wanyama  makampuni na nyumba za serikali na mali zote za watanzania. Viongozi walioko madarakani hivi sasa wengi wao walisomeshwa na serikali, ni vipi wanashindwa kuweka utaratibu mzuri wa kizazi kipya kupata fursa ya elimu ya juu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali ya awamu ya pili ilijaribu kuwalazimisha wanafunzi wajilipie chuo kikuu, kwa sababu Mwalimu Nyerere alikuwepo, na wanafunzi walikuwa na uwezo mkubwa wa kujipanga na kupigania haki yao, serikali ilishindwa. Hata hivyo kadri Chama Cha Mapinduzi kilivyozidi kujipanga kuhakikisha kinamkandamiza mtoto wa kimasikini, ndivyo kilivyokaribia ushindi, hatimaye katika awamu ya tatu ya CCM kiliweza kushinikiza wanafunzi kujisomesha lakini kwa mkopo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Baada ya serikali ya awamu ya nne kuingia madarakani , tulitarajia mabadiliko ya msingi katika elimu ya juu. Lakini mbaya zaidi kilichotokea ni kwamba ni mwenendo mbaya na wa ukandamizaji zaidi kwa wanafunzi wanaotoka familia masikini.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati serikali ya awamu ya kwanza iliweza kuwasomesha wanafunzi wote bila kulipa hata shilingi wala mkopo, serikali ya awamu ya pili na ya tatu pamoja na kuuza migodi makampuni na mbuga za wanyama ilishindwa kuwasomesha wanafunzi masikini.  Ilifuta utaratibu huo na kuanza kuwasomesha wanafunzi masikini kwa mkopo huku yenyewe ikijivinjari kwa maisha ya anasa katikati ya dimbwi linalotoa harufu ya umasikni.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Serikali ya awamu ya nne iliyoingia madarakani kwa ahadi kemkem na kujifanya yenyewe ndio mkombozi. Ndani ya mwaka mmoja tu, mwenendo na kasi yake mpya, unaelekea kummaliza mkulima na mfanyakazi ambaye ambae pamoja na ukweli kuwa ndio aliyepigania uhuru wa nchi hii ndio masikini wa kutupwa katika nchi hii&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wakati serikali ya awamu ya pili na tatu pamoja na uozo uliofanyika lakini iliweza kutoa mikopo. Serikali ya awamu ya nne kwasababu ya kuendekeza mikataba yenye mazingira ya rushwa na matumizi ya anasa sambamba na kukosa dira madhubuti ya uchumi,   imeshindwa kutoa mikopo kwa wanafunzi masikini ambao ni watoto wa wakulima na wafanyakazi, na sasa inawataka waanze kujilipia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naona hatari kubwa huko tuendako, na bila wanafunzi na asasi za kiraia kushika bango, serikali itaturejesha kwenye utumwa mkongwe wa wageni, maana mali zote zinasombwa na wageni, huku viongozi wetu wakiingia mikataba yenye utata kila kukicha. Bila wanafunzi na asasi hizo kusimama wima kudai haki hii, nchi yetu inaelekea rasmi kuingia kwenye ukoloni mamboleo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hakuna nchi iliyofanya mapinduzi ya kisiasa, kiuchumi na kijamii bila ya kuwekeza zaidi kwenye elimu. Chama  Cha Mapinduzi kinaposhindwa kufanya mapinduzi katika elimu maana yake hakiwezi kufanya mapinduzi katika maendeleo ya watu kama dhana ya mapinduzi ni katika maendeleo ya watu,  labda kama maana yake ni vinginevyo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;RAI YANGU KWA VIJANA&lt;br /&gt;Naomba na kusisitiza kuwa, vijana tusitishwe wala  tusirubuniwe. Tunataarifa kuwa CCM kimeanza kupita vyuoni na mbaya zaidi kinavunja sheria kiliyoipigania chenyewe ya kukataza siasa vyuoni,  lakini sasa kinawatumia viongozi wa vyuo kufanya mkakati wa kuwaingiza vijana CCM,   siwazuii vijana kuingia CCM lakini CCM izingatie sheria za nchi kwa upande mmoja,&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na kwa upande wa pili,  nawaomba vijana mtazame mbele zaidi , na kujiuliza mara mbili mara tatu juu ya  ni nani atasimamia haki zenu ? Je sheria hizi zinamruhusu mdogo wako, ndugu yako, na hata mtoto wa jirani yako aliyeko kijijini kupata elimu ya juu?.Je unaweza kutetea na kuleta mabadiliko kwa mfumo uliopo kazi ambayo ilimshinda hata mwasisi wa CCM yenyewe, Hayati Baba wa Taifa letu, Mwl JK Nyerere ?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Muda wa kustarehe vijana bado !, nchi ipo kwenye lindi la tope la umasikini , tusichelee kudai haki yetu na kuisimamia nchi yetu ikae kwenye mstari mnyoofu kwa hofu potofu ya kunyimwa kazi,   au ahadi za kupewa ukuu wa wilaya, ubunge, ukurugenzi, nk.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tusimame pamoja tudai mabadiliko ya kweli mpaka serikali tuiweke kwenye kona yenye mwanga iweze kuona kuwa kupewa uongozi wa nchi ni kupewa dhamana na wananchi, na haina maana ya kuwa juu ya vichwa vya wananchi.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na nawataka wanafunzi wa vyuo vikuu wasiwe wabinafsi na kusimama kidete kwenye migomo na maandamano wakati wa kudai haki zao za mikopo tu bali watazame maslahi ya umma kwa ujumla ikiwemo masuala ya kupinga mikataba mibovu kama IPTL, RICHMOND, kwenye madini, ununuzi wa RADA na ndege ya rais. Huku kuna mabilioni ambayo yalipaswa kuelekezwa kwenye elimu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Profesa Msolla akumbuke maneno ya Mwanamuziki Bob Marley kwamba unaweza kuwadanganya baadhi ya watu kwa muda mchache lakini huwezi kuwadanganya watu wote kwa muda wote, na kama Mwalimu alivyowahi kusema haki haiwezi kupewa kwenye kisahani cha chai kama zawadi. Haki inatafutwa. Hakuna kulala, Mpaka kieleweke!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwandishi wa makala hii ni mwanaharakati na mwanasiasa kijana anayepatikana kupitia 0754 694 553, mnyika@chadema.net</description><link>http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2007/01/profesa-msolla-suluhisho-la-migomo-ni.html</link><author>UDI</author></item><item><guid isPermaLink='false'>tag:blogger.com,1999:blog-13876107.post-115971242393541807</guid><pubDate>Sun, 01 Oct 2006 14:19:00 +0000</pubDate><atom:updated>2006-10-01T17:20:23.936+03:00</atom:updated><title></title><description>Mungu awalaze mahali pema:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a href="http://www.a-free-guestbook.com/guestbook.php?username=duesville"&gt;http://www.a-free-guestbook.com/guestbook.php?username=duesville&lt;/a&gt;</description><link>http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2006/10/mungu-awalaze-mahali-pema-httpwww.html</link><author>UDI</author></item><item><guid isPermaLink='false'>tag:blogger.com,1999:blog-13876107.post-115971215810705839</guid><pubDate>Sun, 01 Oct 2006 14:14:00 +0000</pubDate><atom:updated>2006-10-01T17:15:58.106+03:00</atom:updated><title></title><description>Tusambaze, tuweke kumbukumbu na kuhamasisha mabadiliko:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a href="http://www.jamboforums.co.tz/showthread.php?t=311"&gt;http://www.jamboforums.co.tz/showthread.php?t=311&lt;/a&gt;</description><link>http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2006/10/tusambaze-tuweke-kumbukumbu-na.html</link><author>UDI</author></item><item><guid isPermaLink='false'>tag:blogger.com,1999:blog-13876107.post-115971202226784377</guid><pubDate>Sun, 01 Oct 2006 14:11:00 +0000</pubDate><atom:updated>2006-10-01T17:13:42.286+03:00</atom:updated><title></title><description>Majibu yangu kuhusu mwelekeo wa CHADEMA:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;a href="http://www.jamboforums.co.tz/showthread.php?t=291&amp;page=3"&gt;http://www.jamboforums.co.tz/showthread.php?t=291&amp;amp;page=3&lt;/a&gt;</description><link>http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2006/10/majibu-yangu-kuhusu-mwelekeo-wa.html</link><author>UDI</author></item><item><guid isPermaLink='false'>tag:blogger.com,1999:blog-13876107.post-115948176438972140</guid><pubDate>Thu, 28 Sep 2006 22:15:00 +0000</pubDate><atom:updated>2006-09-29T01:16:04.416+03:00</atom:updated><title></title><description>&lt;div align="justify"&gt;&lt;br /&gt;DOKEZO KUHUSU UZINDUZI MPYA WA CHADEMA ULIOFANYIKA 13 AGOSTI 2006&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na John John Mnyika&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; “Ukiona kobe ameinama ujue anatunga sheria” na “kimya kirefu kina mshindo mkuu”. Leo ni siku ya kipekee na ya muhimu sana, si tu kwa chama chetu, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), lakini pia kwa wazalendo, wanaharakati, na watanzania wote kwa ujumla. Historia na hali ya chama chetu na vyama vya upinzani kwa ujumla hususani baada ya uchaguzi mkuu uliopita, ndivyo hasa vinavyojenga upekee na umuhimu wa sikuu hii.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mtakumbuka kuwa miaka kumi na tatu iliyopita CHADEMA ilizinduliwa rasmi baada ya kupata usajili wa kudumu tarehe 1 Julai, 1993 chini ya mfumo wa vyama vingi vya siasa. Wakati huo, waasisi wa chama chetu waliweka bayana imani, matumaini na mwelekeo wa CHADEMA. Toka wakati wa Mzee Edwin Mtei na wenzake, ambaye leo tumemzawadia kwa kuthamini mchango wake kama muasisi na mwenyekiti wa kwanza; Kwenda wakati wa Mzee Bob Makani na wenzake, ambaye leo tumemzawadia kama ishara ya kutambua utumishi wake uliotukuka alipokuwa mwenyekiti wa pili wa CHADEMA. Na sasa wakati wangu Freeman Mbowe na wenzake. Leo historia inaandikwa tena kwa kufanya uzinduzi mwingine. Hii ni ishara ya mwendelezo wa imani, matumaini na mwelekeo wa kweli wa CHADEMA chini ya misingi iliyowekwa na waasisi wa chama hiki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nini hatma ya upinzani katika muktadha wa matokeo ya uchaguzi 2005 na utawala wa awamu ya nne?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tumekuwa kimya kidogo tangu  kumalizika kwa uchaguzi mkuu 2005, uchaguzi uliokipa chama tawala ushindi wa asilimia themanini katika nafasi ya uraisi na upinzani kupata idadi ndogo ya wawakilishi wa ubunge na udiwani. Kwa ujumla matokeo yameonesha kuwa upinzani umeporomoka. Bila shaka ni vyema kwanza nikachukua fursa hii kugusia swali ambalo baadhi ya watu wamekuwa wakijiuliza pasipo kuwa na jibu ilhali wengine wakitoa majibu ya kupotosha: Nini hatma ya upinzani Tanzania baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu 2005?. Ama kwa maneno mengine, Upinzani umekufa au unaelekea kufa?. Sina nia ya kujibu swali hili kwa kina kwa kuwa leo si mahali pake. Leo tunafanya uzinduzi wa CHADEMA. Lakini kwa kuwa CHADEMA kinaitwa ‘chama cha upinzani’ naona ni vyema nidokeze hoja kadhaa kuchochea mjadala zaidi kuhusu swali hilo. Hii ni kwa sababu imani, matumaini na mwelekeo  wa CHADEMA unategemea pia mtazamo mwafaka wa watanzania kuhusu swali hilo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nianze kwa kuweka bayana kwamba sipendezwi na jina – ‘vyama vya upinzani’. Sisi wanachadema tunapenda kukiita CHADEMA- ‘chama mbadala’. Vyama hivi vinavyoitwa vya upinzani ni vyama ambavyo kwa malengo ya muda mfupi vinalenga kutoa fikra na sera mbadala. Havijaanzishwa kwa ajili ya kupinga tu!. Hivi ni vyama ambavyo kwa malengo ya muda mrefu vinalenga kuchukua dola na kutekeleza misingi na mipango mbadala. Ni serikali zinazosubiri. Sasa je, vyama mbadala vimekufa au vitakufa? Mimi nasema hapana. Vyama mbadala makini havijafa na haviwezi kufa. Labda “vyama magirini”. Nadokeza sababu kumi na tatu zifuatazo kuthibitisha hilo:&lt;br /&gt;·         Mosi, sababu zilizotufanya tuanzishe mfumo wa vyama vingi,ziwe ni za ndani au za nje bado zipo. Mathalani haja ya kupanua wigo wa demokrasia na kuchochea utawala bora na wenye uwajibikaji bado ipo. Na kwa mantiki hiyo vyama mbadala vitaendelea kuwepo.&lt;br /&gt;·         Vipo vyama mbadala ambavyo mpaka sasa vimeonyesha mchango wao kwa taifa. Ukichambua toka mfumo wa vyama vingi uanze kuna maamuzi ya kisera yamefanyika kutokana na hoja ambazo ziliibuliwa na vyama vinavyoitwa vya upinzani. Hata katika utawala wa awamu ya nne, kuna mambo kadhaa ambayo serikali imeyachukua kutoka upinzani. Hii ni sababu tosha ya raia makini kutaka upinzani uendelee kama vyanzo vya sera mbadala.&lt;br /&gt;·         Pamoja na uchache wa ‘wapinzani’ katika vyombo vya maamuzi mchango wao wa hoja katika kuiwajibisha serikali umeonekana. Imefikia hatua kwamba raia wengi wanatamani wapinzani wengi zaidi wawepo bungeni. Hii ni sababu ya upinzani kuendelea kuungwa mkono na kuhamasishwa kuendelea kuwepo.&lt;br /&gt;·         Matokeo ya uchaguzi yanaonyesha kuwa vipo vyama ambavyo vina uwakilishi katika vyombo vya maamuzi. Vyama hivi vinavyoitwa vya upinzani pia ni vyama tawala baadhi ya maeneo, mathalani CHADEMA inayotawala halmashauri za karatu na kigoma ujiji. Kwa hiyo haviwezi kufa kwa sababu za kawaida.&lt;br /&gt;·         Matatizo ya wananchi bado yapo pamoja na ahadi nyingi. Shida wanazopata wananchi ni sababu tosha ya wao kuwa wapinzani wa mfumo uliopo. Hali hii inaota mizizi zaidi pale wanaposhindwa kuona matokeo yanayoshikika ya uongozi ulioko madarakani.&lt;br /&gt;·         ‘Vyama makini’ vya upinzani vinapata nguvu kadiri ‘vyama magirini’ vinavyozidi kupuputika na wakati huohuo vyama mbadala kushirikiana. Vyama hivi vinazidi kuwa katika nafasi ya kukua na kukomaa kadri mamluki wanavyozidi kugundulika siku hata siku na kurudi walikotoka.&lt;br /&gt;·         Uzoefu kutoka katika nchi nyingine unaonyesha hata katika hali bora ya maisha upinzani unaendelea kushamiri. Hivyo raia wakati wote wanaendeleza upinzani ili kupata kilicho bora zaidi.&lt;br /&gt;·         Vipo vyama vyenye mtandao wa wanachama na wapenzi ambao upinzani uko ndani yao. Upinzani kwao ni suala la kuendelea. It’s a going concern&lt;br /&gt;·         Upo upinzani ndani ya mfumo wenyewe wa utawala, upinzani huu ni chanzo kingine cha upinzani wa nje kuendelea kukua.&lt;br /&gt;·         Jitihada za kuhujumu na kubomoa upinzani zinaishia katika mambo yanayoshikika tu mathalani ‘kununua vijiwe vya wakereketwa’, upinzani kama fikra, mawazo na imani unaendelea kushamiri katika nafsi za watu. Huu haujafa wala hautakufa mpaka fikra, mawazo na imani vitakapo kufa.&lt;br /&gt;·         Vipo vyama vya upinzani ambavyo vimekuwa kisiasa na vinaendelea kujipanga na kujijenga ikiwemo kukabiliana na vikwazo. Hivi vinaonyesha kutokufa na badala yake vinazidi kukua.&lt;br /&gt;·         Wapo watu wanaoingia upinzani kutoka katika mfumo wa utawala kama ambavyo wapo wanaotoka katika upinzani kurudi katika chama tawala. Lakini wachunguzi wa mambo wanafananisha wengine wanaotoka upinzani sawa na wale wanaolezewa kwenye vitabu vitakatifu, waliopata taabu jangwani kisha wakawaomba manabii wawarudishe utumwani walipokuwa karibu na masufuria ya nyama. Kwa maneno mengine, ni wapinzani wa kweli pekee ndio wanaosimama kidete kuifikia nchi ya ahadi&lt;br /&gt;·         Nasisititiza kuwa vyama vinavyoitwa vya upinzani hususani CHADEMA, havijafa na wala havielekei kufa kwa sababu, “Maendeleo ya kweli hayawezi kuletwa na mafisadi walewale wa chama kilekile chenye uoza ule ule wakiendeleza yale yale eti kwa ari mpya, nguvu mpya, na kasi mpya”. Vyama mbadala hasa CHADEMA vitaendelea kupigania maendeleo ya kweli pasipo kuchoka.&lt;br /&gt;Tunaweza kuzijadili vizuri sababu hizi kwa kuchambua historia ya CHADEMA kama mfano wa kutazama ilipotoka, ilipo na inapokwenda baada ya uchaguzi mkuu wa 2005.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nini nafasi ya CHADEMA katika siasa Tanzania chini ya muktadha huo?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pamoja na kushindwa uchaguzi mkuu wa 2005, CHADEMA imeongeza idadi ya wabunge kutoka 5 hadi 11 ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 110 na kuongeza idadi ya kura za ujumla za ubunge kutoka asilimia 4.23 mpaka 8.2. ambayo ni asilimia 100. Ruzuku ya chama imeongezeka kutoka milioni 5.6 kwa mwezi mpaka milioni 35.5 na hivyo kutoa nguvu nyingine ya chama kuweza kujijenga kisiasa. CHADEMA ndicho chama cha upinzani chenye wabunge wengi Tanzania bara. Tulisimamisha mgombea Urais kwa mara ya kwanza na kushika nafasi ya tatu. Jumla ya madiwani imeongezeka kutoka 64 mwaka 2000 mpaka 99 katika uchaguzi 2005. Kwa upande wa Zanzibar chama kimeweza kusimamisha wagombea wengi zaidi kuliko chaguzi zingine na kushika nafasi ya tatu katika kura za ubunge katika majimbo mengi na kujitambulisha kama nguvu ya tatu katika siasa za visiwani. Matokeo haya yamepatikana kwa rasilimali ndogo na kwa maandalizi madogo yaliyofanywa muda mchache kabla ya uchaguzi tena katika mazingira ya ‘rafu za kisiasa’. Vipo vyama ambavyo vimeendelea kupata uwiano ule ule wa kura na vingine vimeporomoka. CHADEMA ndicho chama pekee kikubwa cha upinzani ambacho kimekua na kinaendelea kukua kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mambo gani ya pekee ambayo CHADEMA imeyapata kutokana na uchaguzi 2005?&lt;br /&gt;Uchaguzi wa mwaka 2005 unaonesha kuwa CHADEMA ni chama chenye sura ya utaifa na kitaifa. Tulisema wazi wakati wa kampeni “Tanzania kwanza”. Mwaka  2005 ulishuhudia CHADEMA ikisimamia kidete masuala ya utaifa. Kuanzia haja ya wananchi kumiliki na kunufaika na raslimali na maliasili zetu. Mpaka kwenye mijadala kuhusu uzalendo na alama za taifa mathalani bendera na haja ya kuwaenzi kwa vitendo waasisi wa taifa hili hususani Mwalimu Nyerere. Yote yalitoa mwelekeo wa misimamo yetu kuhusu utaifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CHADEMA ilichukua sura ya kitaifa katika kampeni, ikipendwa kuanzia kusini mwa Tanzania mpaka kaskazini. Kutoka magharibi mpaka mashariki. Matokeo ya uchaguzi yanadhihirisha mwelekeo huu wa kitaifa. Tumepata ushindi katika kona mbalimbali za nchi yetu. Kutoka Karatu huko Arusha mpaka Mpanda Kati mkoani Rukwa. Kutoka Moshi Mjini Mkoani Kilimanjaro mpaka Kigoma Kaskazini huko Kigoma. Tumesambaa zaidi na kushinda hata Tarime mkoani Mara. Tumeendelea kuwa chama tawala katika halmashauri ya Karatu na kutawala kwa mseto katika halmashauri ya Kigoma Ujiji.  Na madiwani wetu 99 nao wamesambaa katika kila pahali nchini. Katika kila mkoa lazima kuna majimbo au jimbo ama walau kata ambapo tuna na nguvu kubwa kisiasa. CHADEMA ni chama cha utaifa na cha kitaifa. Hii ni mbegu ya mwelekeo tuliyoipanda mwaka 2005.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nini chanzo cha uzinduzi mpya wa CHADEMA?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Naam! “Kobe akiinama ujue anatunga sheria” na “kimya kirefu kina mshindo mkuu”. CHADEMA tulikuwa kimya tukijipanga. Baada ya uchaguzi tulikaa kimya na kuibuka kwenye vikao vya kamati kuu na baraza kuu la chama tukitathmini kwa kina uchaguzi na kuandaa mikakati ya hatua za awali. Tulikaa kimya tena na kutuma timu zetu katika wilaya mbalimbali kukusanya maoni kuhusu mabadiliko ya  chama. Leo tumemaliza mkutano mkuu wa chama, na sasa ni wakati wa kazi. Tunaumaliza ukimya wetu kwa kishindo kwa kuizindua upya CHADEMA baada ya zaidi muongo mmoja tangu kuasisiwa kwake.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunafanya hivi  kujenga chama imara na makini zaidi ili kuongeza ufanisi katika ushindani demokrasia ya vyama vingi. Tunazindua mchakato wa kwanza unaohusisha zaidi mabadiliko ya kimuundo na zana kisha tutaanza mchakato wa maboresho ya kisera na uongozi. Tunazindua alama na zana sita za CHADEMA. Ndani ya alama na zana hizi upo ujumbe mahsusi kwa wanaCHADEMA na watanzania. Alama na zana hizi ni ishara tu ya imani, matumaini na mwelekeo wetu kwa mustakabali wa chama na taifa letu.. Tunatazama mbali, tukiwa na imani, matumaini na mwelekeo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uzinduzi wa mpango mkakati wa CHADEMA 2006 na mpaka 2010 ni nini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mosi, tunazindua rasmi utekelezaji wa Mpango Mkakati wa CHADEMA kuanzia 2006 mpaka 2010. Mpango Mkakati ni dhana iliyotoka katika medani ya kivita. CHADEMA tunaitumia dhana hii je tunajipanga kuingia msituni? Naam, tunaingia vitani kwa silaha ya demokrasia ili kupambana na maadui ambao tunao katika ngazi mbili. Ya kwanza ni maadui wanaowakabili wananchi-ujinga, umaskini, maradhi na ufisadi. Ya pili ni mfumo uliowekwa na chama tawala. Hivyo tunajipanga kupambana kwa kutumia siasa na si silaha, ili kutumia uongozi kuleta mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli. Mpango Mkakati ni dhana inayotufanya kutambua nguvu na kuzitumia, kufahamu fursa na kuziendea, kubaini udhaifu na kuuondoa na kugundua vikwazo na kuviepuka ili kupata ushindi. Katika medani ya maendeleo, Mpango Mkakati tunaweza kuulezea  kuwa ni mpangilio unaoelekeza tulipotoka, tulipo, tunapotaka kwenda na namna tutakavyokwenda. Katika Mpango Mkakati huu, yapo mambo ambayo tumedhamiria kuyafanya kwa ajili ya kuleta mabadiliko ya kweli ndani ya chama. Pia yapo mambo ambayo tumedhamiria kuyasimamia kuleta mabadiliko ya kweli nje ya chama,kwa maneno mengine, katika taifa kwa ujumla. Mpango Mkakati huu una mambo mengi, mengine ni siri za ushindi. Kwa mantiki hiyo, nadokeza machache tu:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa ndani tumepanga kujiendesha kama “chama taasisi” na “chama uchaguzi”.  Tumemaliza kampeni ya uchaguzi mkuu. Sasa tunaendesha kampeni ya mabadiliko na maendeleo. Tutaendelea kufanya mabadiliko mbalimbali ndani ya chama pamoja na kuboresha mtandao wa chama ikiwemo vijijini. Baadhi ya mabadiliko ya alama na zana ambayo tumeshayatekeleza tunayazindua leo. Kwa upande mwingine tumejipanga kuwa sauti ya wasio na sauti tukitetea, kuendeleza na kutekeleza mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli. Tumedhamiria kusimamia uwajibikaji wa serikali na kuishinikiza kutekeleza ahadi ilizozitoa. Tutaendelea kuwa wenye mtizamo chanya na wenye kujenga katika kuiwajibisha serikali. Na tutakuwa watu wa fikra, wenye nafsi wazi(open mind) na nishati katika kuibua mawazo na kutengeneza sera tunazohitaji kukabiliana na changamoto hususani za muda mrefu ambazo nchi yetu inakabiliana nazo. CHADEMA kinaendelea kuwa moja ya vyanzo vya imani, matumaini na mwelekeo wa Taifa letu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tulishaanza hatua hizi kwa kutoa sera mbadala. Zipo ambazo serikali imeamua kuzitekeleza. Hatuna tatizo na hilo maana hiyo pia. ndio faida ya kuwa na vyama mbadala kama CHADEMA . Tatizo letu ni kwamba kwa uzoefu wa huko nyuma na dalili zinavyoonyesha sasa serikali inazitekeleza sera hizi nusu nusu na pengine ovyo ovyo. Tunatoa rai kwa serikali kuchota kwa kina utaalamu wa kutekeleza sera hizi toka kwetu. Mkishindwa kutekeleza ushauri huu ni wazi wananchi watakuwa na sababu ya ziada ya kuwapumzisha katika chaguzi zijazo ili tuingie madarakani kutekeleza sera hizo kwa umakini na ufanisi zaidi. Hayo ndiyo mabadiliko ya kweli yanayotakiwa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uzinduzi wa kauli mbiu za ‘Tumanini Jipya’ la “mabadiliko ya kweli, Uhuru wa Kweli”?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pili, Tunazindua kauli mbiu ya mchakato huu. “Tumaini Jipya”. Hii ni kauli mbiu inayobeba dhana nzima ya “imani, matumaini na mwelekeo”. Kauli mbiu hii itakwenda sambamba na uzinduzi  rasmi kauli mbiu ya: “Mabadiliko ya Kweli, Uhuru wa Kweli”. Hii ni kauli mbiu tuliyoitumia wakati wa kampeni za uchaguzi.Tunaizindua tena kama ishara ya kuindeleza na kuitekeleza.Wakati wa kampeni tulisema- “ Maendeleo ya kweli hayawezi kuletwa na mafisadi wale wale wa chama kile kile chenye uoza ule ule wakiendeleza yale yale eti kwa ari mpya, kasi mpya na nguvu mpya. CHADEMA inaamini kwamba kwa falsafa ya Chukua Chako Mapema (CCM), Tanzania yenye neema haitawezekana”, mwisho wa kunukuu. Tuliyasema haya tukitaka mabadiliko ya kweli na hatimaye uhuru wa kweli.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa maneno ya mtaalamu wa siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam(UDSM),  Profesa Mwesiga Baregu aliyoyatoa hivi karibuni,  “Ari, Nguvu na Kasi mpya haiwezi kuwa na maana kama hakuna fikra mpya”. Zaidi ya miezi sita imepita toka utawala wa awamu ya nne ukae madarakani, tumeanza kuona haja ya kuendelea kutetea mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli.Tumesikiliza maneno zaidi ya kuona vitendo. Tumeendelea kupata ahadi lakini nyingine zikiwa na hadaa. Tumewauliza wananchi kadhaa wa kawaida swali moja: Je, umeanza kuona japo matumaini ya maisha bora katika hali yako ya kila siku? Jibu la kijana mmoja ambalo kwa muhtasari linatoa mawazo ya wengine ni - “Tunauziwa mbuzi kwenye gunia”.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa ndipo inapokuja haja ya kuendelea kutetea mabadiliko ya kweli, uhuru wa kweli. Raisi Kikwete na Waziri Mkuu Lowasa walianza kwa hekaheka. Lakini mfumo unaelekea kuwakwaza. Na hii ni wazi kama alivyotoa wosia Mwalimu Nyerere kwenye kitabu cha uongozi wetu na hatma ya Tanzania- nchi yetu imeoza. “Our country is rotten to the core”. Tunahitaji mabadiliko ya kimfumo. Ndio maana tumedhamiria kutetea na kutekeleza mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli. Katika ngao na wimbo wa Taifa ipo ndoto yetu watanzania: “Uhuru na Umoja”. Hii ni ndoto ya pamoja bila kujali itikadi. Ni ndoto tuliyorithi toka kwa waasisi wa Taifa letu. Wakati wa kudai uhuru, viongozi wetu waliweka bayana kwamba tunataka uhuru ili tuondokane na umaskini, ujinga, maradhi na ufisadi ambavyo mkoloni alishindwa kuviondoa. Hatuwezi kusema tuna umoja katika taifa lenye pengo kubwa baina ya maskini na matajiri. Hatuwezi kusema tuna umoja katika ubaguzi. Nia ya kudai uhuru ilikuwa ni kuondoa maadui hawa na matokeo ya uhuru ni taifa lenye elimu, afya, utajiri na uongozi bora. Bado hatujafika. Ndio maana tunasema, ni wakati wa kuendeleza na kutekeleza mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli. Katika hali hii, nawakumbusha tena, “Hakuna Kulala, Mpaka Kieleweke”. Hakuna kulala, tuendeleze mabadiliko ya kweli. Mpaka kieleweke! Kikieleweka tutakuwa na uhuru wa kweli. Huwezi kulala kwa furaha katika ujinga, huwezi kulala kwa raha katika umaskini, utalala kwa karaha katika maradhi, huwezi kulala katika ufisadi. Hivyo hakuna kulala mpaka kieleweke. Mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli ni sehemu ya imani, matumaini na mwelekeo tunaouzindua leo.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uzinduzi wa marekebesho ya katiba ya CHADEMA ni nini?;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tatu, tunazindua marekebisho ya katiba ya CHADEMA. Tumefanya marekebisho ya katiba ya chama hususani katika itikadi, muundo na wajibu. Hii ni alama ya mabadiliko ya kweli. Tunasema kwa maneno na kwa vitendo. Mabadiliko yanawezekana. Tunaamini mabadiliko ya kweli yanaanzia ndani. Wanasosholojia wanasema “Mabadiliko huanzia kwangu”. Huu ndio ujumbe ambao tunamwambia kila mtanzania-‘badilika, tuibadili nchi yetu’.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tumeweka bayana itikadi yetu.Hapo nyuma tulisema CHADEMA inaamini katika falsafa na itikadi ya nguvu na mamlaka ya umma. Sasa tumeamua kuweka bayana falsafa yetu na itikadi yetu. CHADEMA tunaendelea kuwa na falsafa ya nguvu na mamlaka ya umma. Huu ni msimamo wetu wa asili: Kwamba falsafa ya CHADEMA ni kuamini katika “nguvu na Mamlaka ya Umma”(People’s Power) katika kumiliki, kuendesha, kubuni na kuendeleza mawazo, raslimali, uchumi na siasa za nchi. Aidha, falsafa ya nguvu na mamlaka ya umma ndiyo msingi na chimbuko la kuundwa kwa dola ya nchi na kuwa umma ndio wenye madaraka ya mwanzo na mwisho katika kuamua hatma ya nchi na taifa pasipo kuingiliwa, kudanganywa au kughilibiwa na viongozi, watawala au wageni....hivyo basi, falsafa ya “nguvu na mamlaka ya Umma” ndiyo njia ya msingi ya kubadilisha fikra na uongozi unaokandamiza umma, ili kuibua fikra mpya na kuweka uongozi unaoweza kumilikiwa, kuhojiwa, na kuwajibishwa na umma kwa kutumia vyombo vinavyopatikana kwa utashi wa wengi kupitia chaguzi huru na haki. Hii ni falsafa tuliyokuwa nayo ambayo tunaiendeleza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwa upande mwingine tumepitia madhumuni ya kuanzishwa kwa CHADEMA pamoja na sera za chama. Tumejitafakari kiitikadi na kuona tutamke bayana katika katiba yetu tuko wapi. Leo tunatamka kwamba Mkutano mkuu wetu umeamua kwa kauli moja kwamba CHADEMA ni chama cha itikadi ya MRENGO WA KATI(center party). Leo tunazindua kijitabu cha muhtasari wa falsafa na itikadi ya CHADEMA kama sehemu ya kuchochea mjadala kuhusu falsafa na itikadi katika nchi yetu. Kwangu mimi itikadi ni imani. Ni imani inayotuunganisha. Ni imani inayotuongoza. Ni imani inayotuelekeza. Ni imani tunayoielekea. Dhana ya “Mrengo wa kati” pengine itaeleweka vyema kama nitasimulia kisa cha dola moja ya kifalme kama ifuatavyo;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;“Katika ufalme huo palikuwa na baraza ambalo lilikuwa na wajumbe wa makundi matatu. Kundi moja lilikuwa upande wa kulia: Hili lilikuwa ni kundi la watawala, wakati wote lilitetea utawala, nidhamu ya kijamii na maslahi ya watu binafsi. Kundi la pili lilikaa upande wa kushoto: Hili lilikuwa likitetea umuhimu wa dola kuhudumia wananchi ikiwemo umiliki wa pamoja  wa njia zote za uzalishaji mali na kuweka mkazo katika haki za matabaka. Kundi la tatu lilikaa katikati: Hili lilikuwa likitetea umuhimu zaidi wa dola kuwawezesha wananchi, likiweka mkazo katika uhuru na uwezekano wa kuboresha maisha ya mwanadamu na jamii. Kundi hili la tatu ndio asili ya itikadi ya mrengo wa kati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;CHADEMA ni chama cha mrengo wa kati kwa mujibu wa madhumuni yake na sera zake. Mathalani, ukipitia madhumuni ya kiuchumi ya CHADEMA, utabaini kuwa ni chama kinachoamini kukuza na kuimarisha uchumi wa nchi kwa kutumia raslimali za nchi yetu bila kuathiri uhuru wa Taifa, na kuhakikisha kuwa umma kwa ujumla unanufaika na raslimali zao. CHADEMA inaamini katika kujenga na kuimarisha uchumi wa soko huru, utakaoheshimu na kulinda haki na mali za watu, biashara huru na sekta ya watu binafsi bila kupoka mamlaka ya umma katika maeneo nyeti. Tunaamini katika soko huru sio soko holela. CHADEMA inaamini kuhakikisha matumizi bora ya raslimali asilia za nchi ili zichangie kikamilifu katika pato la taifa na hasa kuboresha huduma za kiuchumi zinazotumiwa na wananchi wote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Pia CHADEMA kinayo misingi muhimu katika sera na ajenda zake inayokiweka chama katika Mrengo wa Kati. Tunaamini katika uzalendo na kuthamini mila na desturi zetu zilizo nzuri. Tunaamini katika uhuru chini ya sheria zilizo nzuri. Tunaamini katika siasa ambazo ziko juu ya vyama zenye kusimamia zaidi maslahi ya Taifa. Tunaamini katika umuhimu wa dini katika kujenga maadili ya mwanajamii mmoja mmoja bila kuifanya dini kuwa sehemu ya dola. Tunaamini taifa linaundwa na watu, hivyo uhai wake unawategemea watu, na mabadiliko yake yanatokana na watu. Tunaamini kumiliki raslimali na mali miongoni mwa wananchi kunawapa uhuru zaidi hivyo tunataka kujenga chama na baadaye taifa lenye kutoa fursa, ambapo kila mtu bila kujali asili na hali yake anaweza kutimiza na kufanikiwa kadiri ya vipaji vyake. Hizi ni baadhi tu ya sababu zinazofanya CHADEMA kuwa chama cha mrengo wa kati.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatahivyo, hatuamini kwamba itikadi ni suluhisho pekee la matatizo katika taifa. Tutaendelea na utamaduni wetu wa kuwa na itikadi laini (relaxed ideology) badala ya itikadi iliyojibana (restrictive ideology). Tutaendelea na msimamo wetu wa kutaka mabadiliko kwa vitendo (pragmatism). Hiyo ni imani, matumaini na mwelekeo wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Yapi ya ziada kuhusu marekebisho ya katiba ya CHADEMA?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tumezindua marekebisho ya katiba ya CHADEMA yaliyofanywa na mkutano mkuu maalumu uliomalizika leo. Katika mabadiliko haya tumeboresha pia muundo wa chama na kuweka mkazo wajibu wa wanachama. CHADEMA inauchukulia muundo wa chama kama nyenzo muhimu ya kuwezesha ufanisi kwa kuzingatia malengo ya chama na mazingira ya kisiasa na kiutawala katika jamii. Tumepunguza ukubwa wa baadhi ya vyombo katika ngazi mbalimbali hususani mikoa na kupeleka chama katika ngazi ya chini kabisa ambayo tumeiita “Msingi”. Huu ni muundo ambao utarahisisha mawasiliano katika ngazi mbalimbali za uongozi na kuwezesha ushiriki/ushirikishwaji wa wanachama hasa ngazi za chini  na kumilikisha zaidi chama kwa wanachama kwa ujumla. Muundo wa sasa unaendana na ukubwa wa chama kitaasisi na hivyo utapunguza gharama za uendeshaji.  Muundo wa sasa unapeleka chama zaidi katika vitovu vya mapambano ya kisiasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tumebadili muundo wa chama kutoa nafasi zaidi kwa makundi ya kijamii ya wanawake, wazee na vijana. Katiba ya sasa imetoa mwanya wa kuundwa kwa mabaraza ya wanawake, wazee na vijana. Pia tumeweka katika muundo wetu wa chama nafasi maalumu kwa ajili ya wenye ulemavu na kuwa chama cha kwanza kufanya hivyo katika muundo wake wa kikatiba. Tumeweka bayana mamlaka za kinidhamu pamoja na kuboresha mifumo ya utatuzi wa migogoro. Tumeweka mkazo kwenye wajibu wa mwanachama. Tunasisitiza kwamba chama cha siasa ni mjumuiko wa watu mbalimbali wenye imani inayofanana wenye lengo la kuchukua dola ili kuhakikisha imani hiyo inatekelezwa kwa maslahi ya taifa. Chama ni wanachama na uhai wa chama unategemea wanachama. Hivyo kila mwanachama anawajibu wa kutoa mchango wake wa hali na mali katika kutekeleza malengo ya chama. Mabadiliko haya ya kimuundo na kiwajibu yatakuwa msingi muhimu wakati tutakapoanza kujenga chama kuanzia katika ngazi ya chini kabisa ikiwemo vijijini. Tumeanzisha mabalozi wa kaya kumi na kuingiza mfumo wa ngazi ya majimbo kadiri ya sera yetu ya majimbo. Hii ni sehemu ya imani, matumaini na mwelekeo wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uzinduzi wa bendera mpya ya CHADEMA ni nini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nne, tunazindua na kupandisha bendera mpya ya CHADEMA. Ni alama nyingine ya imani, matumaini na mwelekeo wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kimuundo bendera ya CHADEMA ina rangi nne: Nyeusi, Bluu isiyokoza(light blue), nyeupe na nyekundu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Bendera ya CHADEMA ina nembo ya kiganya cha mkono kilichonyoosha vidole viwili katika mfumo wa V kama ishara ya USHINDI. CHADEMA ni chama kinacholenga kushinda kidemokrasia na hatimaye kuleta ushindi wa maendeleo ya taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rangi ya BLUU ISIYOKOZA iko juu ya rangi NYEKUNDU kama ishara kwamba kama taifa tumevushwa na mashujaa kuelekea katika jamii yenye haki, na wakati wote CHADEMA imevuka hatua kama chama cha siasa na sasa inasimamia haki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rangi nyeupe iko mbele ya rangi zote kama ishara kwamba chama kinatanguliza UKWELI NA UWAZI katika nyanja zote. Pia rangi nyeupi imebeba nembo ya chama kwa kuwa UKWELI NA UWAZI ni misingi muhimu sana kwa chama. Nembo ya chama iko mbele kama kama ishara ya CHADEMA kuwa chama kiongozi katika kuchochea misingi muhimu katika kuleta mabadiliko na maendeleo katika Taifa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Rangi zingine zinatenganishwa na ufito mweusi ambao unaumbo la “T” ikiwasilisha kifupi cha jina la taifa la Tanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;RANGI ZA BENDERA:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;NYEUSI&lt;br /&gt;Rangi hii inawakilisha WATU  WA TANZANIA. Hii ni rangi ya wazawa asili wa nchi yetu. Ni rangi ambayo inabeba pia falsafa ya NGUVU YA UMMA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;BLUU ISIYOKOZA (LIGHT BLUE)&lt;br /&gt;Hii ni rangi ya asili ya CHADEMA. Ni rangi ambayo inawasilisha HAKI. Lakini pia rangi hiyo inawakilisha BAHARI kama ishara ya maliasili/raslimaji na Muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;NYEUPE&lt;br /&gt;Rangi nyeupe inawasilisha UKWELI, UWAZI na AMANI. Huu ni msingi muhimu wa CHADEMA. CHADEMA ni chama ambacho kitasimamia uadilifu kwa njia ya demokrasia.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;NYEKUNDU&lt;br /&gt;Rangi nyekundu inawakilisha MASHUJAA. CHADEMA inathamini historia ya nchi yetu ambayo inawasilisha kumbukumbu ya mashujaa waliotupitisha katika michakato ya mbalimbali ya demokrasia na maendeleo ikiwemo harakati za kuondoa ukoloni. Rangi  ni chimbuko la uzalendo wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uzinduzi wa kadi mpya ya CHADEMA nini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tano, tunazindua kadi mpya za uanachama wa CHADEMA.  Tumeamua kuleta imani, matumaini na mwelekeo zaidi katika uanachama sasa tutaanza kuandikisha wanachama upya. Tumeamua kusitisha utamaduni wa kutoa kadi bure ingawa kadi za CHADEMA bado zitaendelea kuuzwa kwa bei ndogo ili kila mtanzania aweze kugharamia. Lengo ni kuhakikisha kila anayechukua kadi ya chama anachangia kama ishara ya nia yake ya kuunga mkono chama na harakati za ukombozi wa nchi hii. Tunataka tuwe na wanachama hai chini ya mkakati wa “CHADEMA ni msingi”. Tunataka wanachama wamiliki na kukiendesha chama. Michango hii midogo midogo ikiunganishwa pamoja ni nguvu ya pekee katika kuchochea kujitegemea na kuendesha chama kwa nguvu ya wanachama. Kama ambavyo bahari ni muunganiko wa matone madogo madogo ya maji ndivyo ambavyo michango hii inaweza kukijenga chama. Tunataka uanachama uwe chachu ya imani, matumaini na mwelekeo wa CHADEMA.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Uzinduzi wa wimbo wa CHADEMA kitaifa nini?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sita, tunazindua wimbo wa CHADEMA. Huu ni wimbo rasmi wa chama utakaoimbwa kote nchini. Ni sauti ya CHADEMA. Ni njia ya kutumia sanaa kuwasilisha hisia, misimamo, hamasa, matamanio na matarajio yetu kuhusu imani, matumaini na mwelekeo wa CHADEMA na taifa. Ni muhtasari wa yote.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ubeti wa kwanza ni sala. Tunaimba:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;MUNGU TUSAIDIE, MUNGU TUWEZESHE,&lt;br /&gt;TANZANIA INA KILIO,&lt;br /&gt;WANAO TWATESEKA MAOVU YANASHAMIRI;&lt;br /&gt;NCHI YATEKETEA WATAWALA WANEEMEKA&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunakabidhi harakati zetu zote kwa nguvu na mamlaka iliyo asili na juu ya yote. Tunaeleza hali halisi ya Taifa letu. Si kwa kukata tamaa, hapana!. Ni ishara ya kujitambua. Ili kwa nguvu yetu na baraka zake tuweze kutoka tulipo na kuelekea kwenye mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli.Tunaeleza, kwamba tunatambua kuwa hatukuumbwa maskini. Tunathamini utu, maliasili na raslimali ambazo tumepatiwa. Tunajua kuwa tunachokosa ni uongozi bora. Hii ni sehemu ya imani, matumaini na mwelekeo wetu&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ubeti wa pili ni CHADEMA. Tunaimba:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Chama cha Demokrasia na Maendeleo,&lt;br /&gt;Tumaini la ukombozi wa kiuchumi na kisiasa&lt;br /&gt;Chama cha Demokrasia na Maendeleo&lt;br /&gt;Chimbuko la fikra mpya nayo mikakati ya utumishi&lt;br /&gt;Mtetezi wa uhuru, uhuru wa kweli&lt;br /&gt;Maendeleo ya kweli wanayostahili Watanzania&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mlinzi wa uzalendo raslimali za taifa la Tanzania&lt;br /&gt;Jukwaa la harakati kukomesha ufisadi, na uoza wa kimaadili&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa tunatoa suluhisho. Tunaeleza nini ambacho tunatetea. Yapi ambayo tunaendeleza. Na kwa vipi tunatekeleza. Kutoka kudai mabadiliko ya kweli, maendeleo ya kweli mpaka uhuru wa kweli. Tunaweka bayana misingi yetu kama chama. Hii ni sehemu nyingine muhimu ya imani, matumaini na mwelekeo wetu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sehemu ya tatu ni Wito: Tunaimba;&lt;br /&gt;Wazee na akina Baba (twende)&lt;br /&gt;Vijana na akina mama (amka)&lt;br /&gt;Pamoja tuna umaskini (tuna maisha duni)&lt;br /&gt;Pamoja tuna uchungu&lt;br /&gt;Watoto nanyi jiungeni (twende)&lt;br /&gt;Tunaweza acheni acheni woga x 2&lt;br /&gt;KIITIKIO:   WanaCHADEMA tushikamane&lt;br /&gt;                     Demokrasia Yawezekana&lt;br /&gt;                     WanaCHADEMA tushikamane&lt;br /&gt;                     Maendeleo Yawezekana&lt;br /&gt;                     Watanzania tushikamane&lt;br /&gt;                     Mabadiliko Yawezekana&lt;br /&gt;                     Nguvu ya Umma, People’s Power&lt;br /&gt;                     Nguvu ya Umma, People’s Power&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hapa tunamalizia wimbo wetu kwa kuchochea hamasa na kutoa wito kwa wote. Ni wito kwa kila mmoja kujiunga nasi katika kuleta mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli. Ni wito wa kutuunga mkono katika kuchochea demokrasia na maendeleo. Ni mwamko, uamsho na hamasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Sasa nini tufanye?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Wimbo wa CHADEMA umehitimisha kwa kusema kila kitu. Na utuingie katika nafsi zetu. Tusiuimbe kama kasuku, tuuimbe tukiwa na imani, matumaini na mwelekeo. Tuuimbe kwa maneno na kuucheza kwa vitendo. Ndio mchango mwingine ambao tunaweza kutoa kwa CHADEMA, Tanzania na ubinadamu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Na huu ndio ujumbe wangu kwenu:&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ewe mwanaCHADEMA, usihoji CHADEMA inafanya nini. Jiulize wewe umefanya nini kama mwanachama wa CHADEMA. Chama ni cha wanachama, jumla ya maneno na matendo ya wanachama ndio matokeo ya chama.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ewe mtanzania, usiulize mfumo wa vyama vingi uko wapi. Jiulize wewe umechangia nini kufanya vyama vya siasa hususani vyama mbadala kama CHADEMA kuendeleza yale unayoyaamini. Kama Mahatma Ghandi alivyosema, “Kuwa wakala wa mabadiliko unayotaka kuyaona”.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ewe mdau wa maendeleo wa ndani na nje ya nchi, usiulize demokrasia ina hali gani Tanzania. Jiulize, wewe umetoa ushikirikano gani kuwaunga mkono watanzania wenye kutetea, kuendeleza na kutekeleza demokrasia. Michango ya kimaendeleo unayoitoa haitaleta matokeo unayoyataka kama taifa halitakuwa na mifumo ya udhibiti thabiti ikiwemo upinzani makini na wenye nguvu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mabadiliko yanawezekana kama kila mmoja akitimiza wajibu. Na tuanze sasa.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Dokezo hili limeandaliwa kwa ajili ya kuwa rejea kwa yoyote anayetaka kufahamu au kufanya uchambuzi kuhusu uzinduzi mpya wa CHADEMA. Mtayarishaji ni Mkurugenzi wa vijana anayepatikana kupitia &lt;a href="mailto:mnyika@yahoo.com"&gt;mnyika@yahoo.com&lt;/a&gt; na 0744 694 553&lt;br /&gt; &lt;/div&gt;</description><link>http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2006/09/dokezo-kuhusu-uzinduzi-mpya-wa-chadema.html</link><author>UDI</author></item><item><guid isPermaLink='false'>tag:blogger.com,1999:blog-13876107.post-115384872100843421</guid><pubDate>Tue, 25 Jul 2006 17:28:00 +0000</pubDate><atom:updated>2006-07-25T20:32:01.026+03:00</atom:updated><title></title><description>&lt;div align="center"&gt;&lt;br /&gt;&lt;span style="font-size:78%;"&gt;Chambelecho cha  maadhimisho ya Siku ya Mashujaa: Tunu yangu kwa wakina Kinjeketile&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;/span&gt;Na John John Mnyika&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kamaradi Kinjeketile na mashujaa wenzako popote mlipo!Hii ni tunu kwenu. Hidaya kwenu mliomwaga damu wakati mapambano kadhaa na Mreno na Mwarabu. Tuzo kwenu  nyinyi mliopigana na Ujerumani wakati wa utawala na mliomwaga damu katika vita vya dunia. Heko ninyi ambao damu ilisafisha safari ya kumng’oa Nduli Amin. Heri wewe Sethi Benjamini na wote waliopotesha maisha katika hekaheka za kueneza Azimio la Arusha. Kumbukumbu kwenu mliotoa damu katika mikikimikiki ya mfumo wa vyama vingi kutoka Zanzibar mpaka bara. Damu yenu iliyomwagika haizoleki, ukiwa mlioucha hauzoeleki lakini fikra mlizosimamia hazizeeki. Mapambano bado yanaendelea!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Kwako Bushiri bin Salim wa Tanga, suriama wa kiarabu na kiafrika, pamoja na nia yako tenge ya kulinda maslahi katika biashara ya utumwa ulimwaga damu kwa kunyogwa Pangani baada ya kuongoza maasi makali dhidi ya kuingia kwa ukoloni wa Kijeruamani-damu yako ilimwagika pamoja na damu za wapiganaji wa Pwani, Morogoro mpaka uhehe. Ewe Mtemi Meli, uliowashinda wadachi mpaka mwenzio Sina alipokusaliti hatimaye wewe na mashujaa wenzako mkamwaga damu kaskazini mkilinda uhuru.Wewe Chifu Mkwawa, tunakukumbuka uliovyowaunganisha wahehe-toka Kalenga, Tosamaganga mpaka ulipoamua kuimwaga damu yako mwenyewe kuliko uhuru upotee mikononi mwako. Mtemi Isiki wa Tabora uliendesha mashambulizi ya kishujaa, hatimaye ukaamua kumwaga damu yako na ya familia yako kwa kujilipua na baruti ili tu usipate aibu ya uhuru kuchukuliwa mbele ya macho yako. Ewe Mtemi Makongoro wa Musoma, ulipambana kwa ushujaa mpaka ilibidi kikosi cha wanamaji kiletwe kupitia miji ya Mombasa na Kisumu kukumaliza.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nakutunuku Kinjeketile kwa kuongoza vita vya kutisha vya Maji Maji kwa miaka kadhaa vilivyoanzia vilima vya Matumbi karibu na Kilwa. Nyinyi mlitaka kumwondoa mkoloni kwa nguvu na mlikuwa tayari kumwaga damu kuliko kuendelea kuishi bila ya uhuru. Mapambano yenu yalisambaa maeneo mengi ya ardhi yetu. Ninyi mlikuwa mashujaa kweli kweli mliojua umuhimu wa imani na falsafa katika mapambano-mkawapa watu ujasiri kwa dawa ya “Kugeuza risasi, Kuwa maji”. Pamoja na kushindwa vita na wazalendo zaidi ya laki moja kupoteza maisha katika wakati ambao ardhi ilikuwa na watu wachache yapo mapigano ambayo mlishinda. Pamoja na machifu 47 wa Kingoni kunyongwa damu yenu ilileta mabadiliko katika utawala. Kwa vyovyote vile damu nyingi kiasi hiki iliyomwagika kwa sababu ya kudai uhuru haiwezi kupuuzwa. Hivyo waraka huu ni tunu kwenu. Mapambano bado yanaendelea!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nawaandikia waraka huu ninyi wahenga mashujaa muweze kurejea na kurekebisha historia. Najua mnaweza msirudi kimwili, lakini ni vyema kiroho mkandelea kuwa nasi. Fikra zenu za kimapambano hazipaswi kupotea. Kumbukumbu zenu za kishujaa hazistahili kufutika. Taifa lisilo na historia haliishi, linakufa. Kupotosha historia ya mashujaa ni kinyaa. Karibu kila eneo katika nchi yetu yupo shujaa ambaye anaweza kukumbukwa laiti kama historia zenu zingejulikana kizazi hata kizazi na kuwa chimbuko la kujiamini, kujithamini na uzalendo miongoni mwa Watanzania.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Julai 25 ilikuwa siku nyingine ambapo tulifanya maadhimisho ya kinafiki ya siku ya mashujaa. Mtanishangaa kwa kutumia dhana kali- “UNAFIKI”. Namaanisha!. Ni dhana ambayo mnaifahamu na hamkuipenda. Ndio maana hamkutaka kuishi katika unafiki wa kukubaliana ama kutumiwa na watawala. Mkaamua kupambana! Mkamwaga damu mkiukimbia unafiki. Sasa tunawakumbuka!. Lakini nasema tena, tunawakumbuka kwa kufanya maadhimisho ya kinafiki ya siku ya mashujaa. Ndani ya dhana ya unafiki kuna tabia nyingi, mojawapo ni kunena tofauti na matendo na kutenda tofauti na kauli. Na ndiyo tabia tunayoifanya wakati wa maadhimisho ya siku ya mashujaa. Ndio maana nasema, tunafanya maadhimisho ya kinafiki.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Labda ni waambie wakina Kinjeketile, nini tulifanya huku kama ishara ya kuuadhimisha ushujaa wenu. Siku chache zilizopita 25 Julai, tulijumuika chini ya Amiri Jeshi Mkuu, kwa sasa ni Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Yeye mwenyewe hakuwepo, alituma mwakilishi wake. Tulielezwa kwamba Rais yupo kwenye ziara ya kikazi Ujerumani!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Usiku mmoja kabla tuliwasha mwenge wa uhuru pale Mnazi mmoja. Halafu asubuhi yake gwaride lilijipanga kuwapokea wageni wa Kitaifa. Zikatolewa salam za Rais na wimbo wa Taifa ukapigwa kwa heshima yenu. Kikundi cha Buruji kikapiga “last post” na gwaride likaweka silaha begani. Askari sita waliojipanga vyema wakapindua silaha zao chini na baadae mizinga ikapigwa kwa ajili yenu huku watu wote wakiwa kimya. Gwaride likafanya “present arms” na kikundi cha buruji kikapiga “reveilles”. Gwaride likateremsha silaha na kufungua miguu.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Halafu silaha za asili ambazo nyingine nyinyi mashujaa mlizitumia zikawekwa kwenye mnara pamoja na maua. Baadhi ya silaha zilizowekwa ni pamoja na mkuki, ngao, sime, shoka, pinde na mishale. Hizi ni kumbukumbu sanifu za mapambano mliyoyafanya.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hatimaye zikafuata sala na swala kutoka kwa viongozi wa dini wakiwakilishwa na sheikh, mchungaji, padri na maraji wa wahindu. Ingawaje sikumwona kiongozi wa dini ya jadi-ambao najua baadhi yenu nyinyi mashujaa na wahenga mliwaamini. Pengine dini za jadi zilitoweka na damu zenu. Gwaride likatoa tena heshima na wimbo wa taifa kupigwa ukafuatiwa na itifaki za viongozi wa kitaifa kuondoka. Wakabaki polisi kuzilinda silaha za kumbukumbu ya mashujaa mpaka jioni na hatimaye mwenge wa uhuru ukazimwa kama ishara ya mwisho wa maadhimisho ya kumbukumbu yenu ninyi mashujaa. Niwaulize wakina Kinjeketile, haya siyo maadhimisho ya kinafiki ya mashujaa?Pengine mtanijibu hapana!.&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ngoja niwaeleze masuala kadhaa halafu niwaulize tena. Siku hizi kuna kitu kinaitwa Bunge, hiki ni chombo cha juu chenye uwakilishi wa wananchi ambacho kunafanya maamuzi mbalimbali ambayo mengine huwa sheria. Chombo hiki ni kama yale mabaraza ya jadi yaliyokuwepo wakati wenu. Wiki iliyopita bunge lilijadili kuhusu maadhimisho ya vita vya Maji Maji ambavyo nyinyi wakina Kinjeketile mliviongoza. Miaka mia moja imepita toka damu yenu azizi ilipomwagika katika mapambano hayo ya kumwondoa mkoloni.Ungekuwepo najua ungekuwa Mbunge wa Kilwa, ungeshangaa sana-Eti maadhimisho ya vita mlivyovianza Kilwa na mapambano ya mwisho yakawa Songea, yanafanyika kinyume chake!Maadhimisho yameanzia Songea na waziri ameahidi pengine yataishia Kilwa. Chacha Wangwe, mbunge wa CHADEMA(wakati wenu hakukuwa na vyama vya siasa vyenye majina haya) jimbo la Tarime, yeye akahoji-kwanini bendera ya taifa isiwekwe rangi nyekundu kama ishara ya kuwakumbuka nyinyi mashujaa wetu? Naibu waziri wa habari na michezo, Mheshimiwa Emanuel Nchimbi-yeye akajibu, hakukuwa na sababu ya rangi nyekundu kuwekwa kwenye bendera ya Taifa kama ishara ya kuwakumbuka mashujaa. Eti, historia ya uhuru wa nchi yetu inaamuliwa kuanzia mkoloni wa mwisho aliyetutawala ambaye ni Muingereza. Sasa kwa kuwa tulipata uhuru wetu kwa amani bila kumwaga damu chini ya uongozi wa mwalimu Nyerere basi hakukuwa na sababu ya kuweka rangi nyekundu. Enyi mashujaa Kinjeketile na wenzako tunaowakumbuka leo mnakubaliana na jibu hili?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Ndio maana nikasema ni maadhimisho ya kinafiki. Tunanena tofauti na matendo. Nimesema awali, tunaanza maadhimisho ya leo kwa kuwasha mwenge wa uhuru halafu baadae tunaweka silaha za jadi. Kinjeketile na wenzako, iulizeni serikali- kama uhuru wetu tuliupata kwa amani, iulizeni serikali kwanini tunawasha mwenge wa uhuru na baadaye kuweka silaha za jadi? Tunanena tofauti na tunavyotenda? Iulizeni serikali, je harakati za mwisho za uhuru ni kipimo pekee cha historia ya nchi na hivyo kuwa kigezo pekee cha kuamua alama za nchi ikiwemo bendera?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Enyi mashujaa mlioambana kuulinda uhuru wetu dhidi ya wakoloni kuingia kuanzia wakati wa Mreno, Mwarabu na Mjerumani na kumwaga damu, mnakubaliana na majibu haya? Kushindwa kwenu na hatimaye ukoloni kuingia hakuondoi historia kuwa mlimwaga damu kwa ajili ya kulinda uhuru wa ardhi hii tukiyoirithi!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Enyi mashujaa mliopambana kuondoa ukoloni hususani ule wa Ujerumani mkamwaga damu, mnakubaliana na kumbukumbu hii?Kwamba mliyoyafanya si historia kuu kama historia ya uhuru toka kwa Mwingereza?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Enyi mashujaa, waulizeni wataalamu wa historia-baada ya Ujerumani kushindwa na makoloni yake yote kuwekwa chini ya halmashauri ya mataifa na baadaye baraza la udhamini, Tanganyika ikiwekwa chini ya uangalizi wa Uingereza-si kwamba tulikuwa katika hatua za mwisho kabisa za kupewa uhuru ambao tayari tulishaupata kwa damu?Waulizeni pia, hakuna damu yoyote iliyomwagika wakati wa Mwingereza?Je, historia ya nchi yetu iliyojikita katika kipenzi chetu Nyerere imewajumuisha mashujaa wote wa ardhi hii?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Nasema kwa damu-kuanzia ushindi pamoja na kushindwa dhidi Mjerumani ambao ulileta mabadiliko katika mfumo wa utawala sanjari na mashujaa ambao walikuwa mstari wa mbele katika jeshi la Mwingereza na washirika wake katika vita dhidi ya Mjerumani, vile vita vya dunia ambavyo vilipiganwa pia katika ardhi yetu?Wakina nani walimwaga damu zaidi katika kile kinachoitwa ukombozi ulioletwa na majeshi ya mfalme  Afrika(KAR) kama si nyinyi babu zetu?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Hojini serikali, hivi bendera hii ni ya Tanganyika au Tanzania? Jibu la Nchimbi limetolewa katika muktadha wa historia ya Tanganyika, Ingekuwa vipi jibu lingetolewa mintaarafu bendera ya Tanzania ambayo ilipatikana kutokana na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ilihali visiwani kuna historia ya damu kumwagika ama kumwagwa wakati wa mapinduzi? Kama kweli tuna serikali ya mapinduzi Zanzibar na utawala wa Chama cha Mapinduzi(CCM), je ni mapinduzi yasiyo na ‘rangi nyekundu’?&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Tunatenda tofauti na kauli! Tunafanya maadhimisho ya kinafiki. Wakina Kinjeketile tunawakumbuka kwa kuwa mlimwaga damu kupinga ukoloni na unyanyasaji. Mtuulize wajukuu zenu, je tunawaadhisha kwa kuendelea kupiga vita yale mliyoyakataa? Kwa hali ilivyo, wapo wanaotenda yale mliyoyakataa pamoja na kuwa wote kwa kauli tunawaenzi ninyi mashujaa. Tunapaswa sasa kuweka fikra zenu katika vitendo kwa ajili ya ukombozi wa taifa letu. Mwalimu Nyerere alikumbuka fikra zenu akatamka na kutenda kwamba uhuru, si uhuru wa maneno. Ni uhuru dhidi ya ujinga, uhuru dhidi ya maradhi, uhuru dhidi ya umaskini na baadaye akaongezea uhuru dhidi ya rushwa ama ufisadi. Enyi wahenga mashujaa, shukeni katika nyoyo za watoto na wajuu zenu, mtufanye kutokana na maadhimisho ya mwaka huu tuweke dhamira ya kupigana vita kwa zana kisasa kuleta mabadiliko ya kweli na uhuru wa kweli, kuleta haki na maisha bora. Hii ndiyo hidaya kwa damu yenu azizi. Sio siri, kwa sera bila silaha, mapambano bado yanaendelea!&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;Mwandishi wa makala hii ni mwanaharakati na mwanasiasa kijana anayepatikana kupitia &lt;a href="mailto:mnyika@yahoo.com"&gt;mnyika@yahoo.com&lt;/a&gt; na 0744 694 553&lt;br /&gt;&lt;br /&gt;&lt;br /&gt; &lt;/div&gt;</description><link>http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2006/07/chambelecho-cha-maadhimisho-ya-siku-ya_25.html</link><author>UDI</author></item><item><guid isPermaLink='false'>tag:blogger.com,1999:blog-13876107.post-115289724195258500</guid><pubDate>Fri, 14 Jul 2006 17:00:00 +0000</pubDate><atom:updated>2006-07-14T20:14:01.976+03:00</atom:updated><title></title><description>HOTUBA YA NDUGU JOHN J. MNYI