Blogu ya Mkurugenzi wa Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA.

Tuesday, April 22, 2008

Bado nalijaribu jamvi jipya

Monday, March 03, 2008

Kingunge alijivunjia mwenyewe heshima


Hebu nikukumbushe kauli zake kidoooooooooogo---

TAMKO KUHUSU KAULI ZA KINGUNGESisi, viongozi wa vyama vya CHADEMA, CUF, NCCR Mageuzina TLP tuliokutana Equator Hotel tarehe 20 Septemba2007 hapa Arusha tumeitafakari “Orodha yaMafisadi”(List of Shame) na tumejadili kauli za Waziriwa Nchi, Ofisi ya Rais, Siasa na Uhusiano waJamii-Mheshimiwa Kingunge Ngombale-Mwiru alizozitoa 18Septemba 2007 na kunukuliwa na vyombo mbalimbali vyahabari Jumatano 19 Septemba 2007 na kwa pamojatumeazimia kutoa tamko lifuatalo:Kingunge anapotosha umma, apuuzwe; wapinzani wanateteataifaTunaunga mkono uamuzi wa viongozi wetu wa kitaifakuanika wazi kwa umma orodha ya mafisadi; hii ni kwasababu rasilimali zinazofujwa ni za wananchiwatanzania, wanaoathirika kutokana na ufisadi ni ummawa watanzania na wenye uamuzi wa mwisho wakuwawajibisha viongozi mafisadi ni umma wa watanzania.Kwa kuzunguka nchini kueleza yaliyotokea bungeni(hususani kusimamishwa kwa Mbunge Zitto Kabwe nakupigwa danadana kwa hoja ya kashfa ya ufisadi ndaniya Benki Kuu iliyokuwa iwasilishwe na Dr WilbroadSlaa) wakati wa Mkutano wa Bunge la Bajetiuliomalizika hivi karibuni, wabunge wa upinzaniwanatimiza wajibu wao kama wawakilishi wa kweli wawananchi. Kwa kuzunguka nchini kueleza kuhusu ufisadiunaendelea nchini, viongozi wa upinzani wanatekelezawajibu wao wa kisiasa wa kuwazungumzia wananchi wotewa Tanzania wanaoguswa na ufisadi bila kujali itikadiama uanachama; ikumbukwe kuwa vyama vya siasa siovyombo vya uchaguzi tu bali ni taasisi muhimu katikajamii katika kuchochea uwajibikaji na maendeleo. Kwamantiki hiyo basi Waziri Kingunge anaupotosha ummaanaposema kwamba ziara za viongozi wa upinzanizinatokana na ‘hasira ya kushindwa uchaguzi mkuu 2005,kambi ya upinzani kushindwa kumtetea Zitto bungeni,wivu wa kuona CCM inatekeleza ilani yake vizuri, nakwamba wanautumia vibaya mfumo wa vyama vingi’.Tunapenda kusisitiza kuwa Viongozi wa umma wanaokiukana/au kuvunja masharti ya katiba ya Jamhuri yaMuungano na Sheria za Maadili ya Viongozi wa ummalazima waanikwe hadharani na kuwajibishwa na yoyoteanayetoka kauli ya kubeza jitahada hizi ni vyemawatanzania wakampuuza. Kama viongozi wa upinzaniwanavunja sheria kwa kutoa uzushi na kufanya uchochezikama Waziri Kingunge anavyodai kwa nini serikalihaiwakamati na kuwapeleka mahakamani badala ya kutoamatamko ya kulalamika?Kauli za Kingunge ni msimamo wa Serikali?; Ikulu itoetamko!Tumezijadili kauli za Waziri Kingunge na katika hatuaya sasa tusingependa kuamini kama zinawakilishamsimamo wa serikali kwa ujumla wake; hatutaki kuaminikwamba kauli hizo ni msimamo wa pamoja wa Serikalichini ya Rais Jakaya Kikwete ambaye pia ni Mwenyekitiwa Baraza la Mawaziri. Katika hatua ya sasatunazichukulia kauli hizo kuwa ni maoni binafsi yaBwana Kingunge mpaka hapo Ikulu itakapothibitishavinginevyo; hivyo kwa tamko hili tungependa ikulu itoeufafanuzi kuhusu kauli hizo. Lakini tunapenda piakutoa tahadhari kwamba inawezekana kauli hizi za BwanaKingunge amezitoa kwa nia ya kupoteza lengo tuanzekuzijadili kauli zake badala ya kujadili orodha yamafisadi na hatma ya rasilimali za nchi yetu. Hivyotungependa kusisitiza kuwa ikulu ijibu hojazilizotolewa na viongozi wa upinzani ambazo zimemgusamoja kwa moja Rais na serikali.Anayelinda ufisadi ndiye anayekwamisha maendeleo nahuduma za kijamiiTunashangazwa na uamuzi kauli ya Kingunge kwambauamuzi wa Viongozi wa Vyama na Wabunge wa Upinzanikuzunguka nchini ni mkakati wa kisiasa wa kuitoaserikali kwenye mstari wa kushughulikia maji, afya nabarabara. Tunapenda kumbukusha Waziri Kingunge kuwakatika orodha hii ya mafisadi pekee zaidi ya shilingitrilioni 1.3(1,300,000,000,000) ambazo kamazingetumika vizuri ni wazi zingeweza kutumikakuboresha maji, umeme na barabara bila kuendeleakuwakamua zaidi wananchi masikini. Ukweli ni kuwa kwakuendelea kulea ufisadi serikali inajitoa yenyewekwenye mstari wa kutumia vyema kodi za wananchi narasilimali za taifa katika kushughulikia shughuli zamaendeleo na huduma za kijamii ikiwemo maji, afya nabarabara. Ni ukweli pia kwamba kwa kuwawajibishamafisadi viongozi wa upinzani wanatimiza wajibu wao wakuhakikisha rasilimali za taifa zinatumika kwa ustawiwa wananchi walio wengi.Vyombo vya dola tayari vinayo orodha ya mafisadi;vichukue hatuaTunashangazwa na kauli ya Waziri Kingunge ya kuhojisababu za Viongozi wa Upinzani kushindwa kuziwasilishakwenye vyombo vya dola tuhuma walizozitoa dhidi yavigogo hao iwapo kweli wanao ushahidi wakuzithibitisha. Tunashangazwa na kauli hii kwa kuwatunaamini kabisa Waziri Kingunge anafahamu kabisa kuwasehemu kubwa ya tuhuma hizi zipo katika Ripoti zaMkaguzi wa Serikali ikiwemo ile ya mwaka 2005/06 nakwamba vyombo vya dola vinafahamu uwepo wa tuhuma hizilakini kwa zaidi ya miaka miwili vyombo hivyohavijachukua hatua dhidi ya vigogo waliotajwa.Tunaamini kwamba viongozi wa upinzani walichofanya nikuamua kushtaki kwa wenye mali walioibiwa ambao niwananchi wote wa Tanzania ili kwa pamoja tuwezekuvitaka vyombo vya dola viweze kuchukua hatua.Tunashangazwa na kauli hii ya Waziri Kingunge ya‘kuwahukumu’ viongozi wa upinzani kwa kushindwakupeleka ushahidi kwa kuwa kauli hii inapingana nakauli zingine ambazo zimewahi kutolewa na viongozi waserikali kuhusu tuhuma hizo hizo. Tunapendakumkumbusha Waziri Kingunge kwamba tayari Spika WaBunge-Samuel Sitta alishasema kwamba anavipelekapolisi vielelezo vyote vya ushahidi alivyotoa Dr Slaaili vichunguzwe. Pengine Kingunge angetoa hukumu hiyokwa Spika kwa kushindwa kupeleka vielelezo. Piaikumbukwe kwamba ni serikali hiyo hiyo iliyowahi kutoataarifa kwa umma kwamba tuhuma za ufisadi ikiwemo zaBOT zinachunguzwa na TAKUKURU. Kadhalika WaziriMkuu-Edward Lowasa alitoa kauli baadaye kwambaSerikali iliyafahamu madai ya Kashfa ya ufisadi BenkiKuu(BOT) kabla ya upinzani. Kwa upande mwingine, madaiya kutaka kushughulikia rushwa kubwa kubwa ikiwemo zakwenye mikataba yalianza kutolewa na Rais Kikwetewakati akifungua Mkutano wa Kwanza kabisa wa Bungemwaka 2005. Lakini baadaye ni Rais Kikwete alinukuliwana vyombo vya habari akisema kwamba anawafahamu walarushwa na anawapa muda wajirekebishe; tulitarajiaWaziri Kingunge kama mshauri wa Rais wa masuala yasiasa angemshauri apeleke ushahidi katika vyombo vyadola na si kuwahukumu viongozi wa upinzani ambaowametoa orodha ya mafisadi na ushahidi kutoka kwenyetaasisi za serikali yenyewe!. Na ni jukumu la vyombovya dola kuchukua hatua za kufuatilia baada ya orodhaya mafisadi kuwekwa hadharani.TAKUKURU inajipotezea imani yenyewe!Tumeshangazwa pia na kauli ya Waziri Kingunge yakuwalaumu viongozi wa upinzani kwa kutokuwa na imanina TAKUKURU. Kwa misingi ya kauli zao ambazo wamezitoakatika nyakati mbalimbali, viongozi wa upinzaniwamekuwa wakikisisitiza kuwa TAKUKURU inajipotezeayenyewe imani kwa wananchi kutokana na taarifa zake nakwamba wamekuwa wakiipa changamoto TAKUKURU kuchukuahatua. Mathalani TAKURU kuisafisha kampuni yaRICHMOND. “….hakuna ushahidi wowote uliopatikanakuthibitisha vitendo vya rushwa, uzembe na upokeaji wakamisheni watendaji wa serikali….uchunguzi huoumethibitisha udhaifu wa kawaida katika utendaji naambao haukuhusisha rushwa au manufaa ya aina yoyoteile kwa upande wa watendaji na hakuna hasarailiyosababishwa na udhaifu huo”(Mwananchi 12/5/2007).“….baada ya kuona hivyo, Richmond ilionekana kufahamumwenendo wa mambo serikalini…”(Tanzania Daima12/5/2007). Maswali yaliyobaki mpaka hivi sasa ambayosi TAKURU wala TAKUKURU ya sasa hawajayajibu ni pamojana: Ni kwanini Kamati ya Waziri Mkuu iliipa tendaRichmond baada ya Bodi ya Wakurugenzi ya Tanescokuitaka bodi yake ya sabuni kutangaza upya zabuni hiyokwa kutimia zabuni za kimataifa? Richmond kuwezakufahamu mwenendo wa mambo ya ndani serikalini sioishara ya rushwa ya kimadaraka? Ni kweli kama hakunahasara iliyosababishwa na uamuzi huu wakati ambapowatanzania wamekaa bila umeme kwa miezi mingi bilakupata umeme wa dharura waliotarajia wakati wadharura, Rais amekiri kwamba umeme ulichangia kushukakwa kasi ya ukuaji wa uchumi na hata kuongeza mfumukowa bei na mpaka leo bado megawatts 100 hazijatimizwana Richmond/Dowans? Tunapenda kumkumbusha WaziriKingunge kwamba Mkataba wa Richmond/Dowans pekeeumeligharimu taifa zaidi ya Bilioni 200 mpaka sasaambazo zingeweza kuelekezwa kwenye elimu, afya nabarabara. Viongozi wa upinzani wanapohoji utendaji waTAKUKURU wanataka ichukue hatua za harakakushughulikia mafisadi na kuendelea kuwa Taasisi yaKuzuia na Kudhibiti Rushwa na si Taasisi ya Kulinda,Kusafisha ama Kutetea Rushwa !Wasomi na asasi za kijamii wako sahihi; Kingungeamelewa madarakaTumefadhaishwa na kauli ya Waziri Kingunge kwambawasomi nchini wametathimini uamuzi wa Bunge wakumsimamisha Mbunge Zitto Kabwe kwa kutanguliza jazbabadala ya busara na kutilia wasiwasi uelewa wa makundiya kijamii kuhusu mantiki ya uzalendo. Hatutakikuamini katika hatua ya sasa kwamba huu ni msimamo waserikali kwamba wasomi na makundi ya kijamiiwametanguliza jazba na kukosa busara na uelewa katikakuijadili adhabu aliyopewa Mbunge Zitto Kabwe na hojayake ya kutetea Rasilimali za nchi yetu hususanimadini. Tunaamini kwamba kauli hii ni maoni binafsi yaBwana Kingunge ambayo ni ishara ya kulewa madarakakutokana kung’ang’ania serikalini toka wakati nchi hiiinapata uhuru kwani hii si mara ya kwanza kutoa kauliza kubeza-aliwahi kuibeza CHADEMA kwa kumtaja Nyererekwenye kampeni 2005 na hivi karibuni Julai 3, 2007aliripotiwa na vyombo vya habari akitetea msimamo waRais Kikwete wa kutumia nafasi yake kama raiskudhoofisha upinzani kwa kufanya kampeni za CCM katikamikutano ya kiserikali. Tunapenda kumbukusha WaziriKingunge maneno ya Shaban Robert kwamba “ elimuilipokuwa bado kujulikana mvi zilihesabika kuwa alamaya hekima lakini fikra hizo wakati wake umeshapitahaupo na wala hauji tena. Kisichobadilika ni kwambamtu mzima bado anastahili heshima kutoka kwa mdogo” .Ni vyema Waziri Kingunge akafahamu kwamba wasomi kamaProfesa Issa Shivji na makundi ya Kijamii mathalaniMtandano wa Jinsia(TGNP), Chama cha Wanasheria waMazingira(LEAT), Kituo cha Sheria na Haki zaBinadamu(LHRC) walifanya tathmini yao kwa lengo lakulinda maslahi ya taifa bila kujali itikadi.Mafisadi zaidi waendelee kutajwa; serikali ijibu hojaHivyo tunapongeza na tutaendelea kuunga mkono jitahadazote za vyama vya siasa, asasi za kijamii na hata watubinafsi waliowataja na watakaoendelea kuwatajaviongozi na/au maafisa wa umma na/au mawakala na/auwashirika wao katika sekta binafsi ambao kwa namnambali mbali wameshiriki katika kupora utajiri na/aufedha za umma na hivyo kulisababishia taifa na umma waWatanzania ufukara na/au umaskini mkubwa. Kadhalikatunaunga mkono na kutoa mwito kwa vyama vya siasa,asasi za kijamii na hata watu binafsi kuendeleakuwawajibisha viongozi wa umma ambao kwa kutumianyadhifa na/au vyeo vyao katika utumishi wa ummawamefanya maamuzi ambayo yamesababisha taifalimepoteza mapato na/au utajiri na rasilmali zake nakuwaneemesha raia na/au taasisi za kiuchumi na/au zakibiashara za kigeni. Kwa mfano, viongozi wa ummawalioshiriki katika kusaini mikataba mibovu katikasekta za madini na/au nishati na/au maeneo mengineyenye umuhimu mkubwa kwa maisha ya taifa na jamii yaWatanzania. Na katika haya tunataka serikali ijibuhoja na si kupuuzia na kutoa kauli za kejeli kama "haoni wapinzani hawana jingine la kufanya", "wana haki yakutoa maoni yao na huo ndio uzuri wa demokrasia" .Waziri Kingunge na serikali kumbukeni kuwa watuwachache wanaweza kudanganyika katika muda mchachelakini watu wote hawewezi kudanganywa wakati wote.Watanzania wa leo na kesho si watanzania wa jana najuzi.John MnyikaMkurugenzi wa Vijana Taifa (CHADEMA)Na Mwenyekiti wa KikaoGodbless LemaKatibu Mwenezi Mkoa-Arusha(TLP)Na Msemaji wa Ushirikiano wa Vyama vya Upinzani-ArushaMohamed MaabadMwenyekiti wa Wilaya-Arusha Mjini(CUF)Na Mwenyekiti wa Ushirikiano wa Vyama vyaUpinzani-ArushaEned MuroMwakilishi-Arusha(NCCR-Mageuzi)Amos KibandaKatibu Mkoa-Arusha(CHADEMA)Calist LazaroMwenyekiti wa wilaya-Arusha Mjini (TLP)

Wednesday, February 20, 2008

Kwa niaba ya Baraza la Vijana wa CHADEMA(BAVICHA), vijana wa CHADEMA tunaungana na wapenda uhuru, haki na ukweli kote nchini kulaani uamuzi wa Jeshi la Polisi kuwakamata na kuwaweka ndani vijana wa wawili wa kitanzania Maxence Melo na Mike Mushi kwa sababu ya masuala ya mtandao wa Jambo Forum(www.jamboforums.com).

Uamuzi wa kuwakamata na kuwaweka ndani kwa takribani saa 24 na kuwahoji kwa zaidi ya saa 14(usiku na mchana) tunaona ni kinyume cha sheria ambayo inaeleza bayana mtuhumiwa anapaswa kuhojiwa si zaidi ya masaa manne kwa mfululizo na kwa ujumla ni uvunjaji wa haki za binadamu na haki za kikatiba za kupata na kutoa taarifa/habari. Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali katika Jeshi la Polisi, vijana hawa wamekamatwa kwa kutuhumiwa kuendesha mtandao wa Jambo Forum ambao unadaiwa kuwachafua watu mbalimbali ambao vyanzo hivyo vya polisi mpaka sasa havijawataja.

Vyanzo mbambali vya polisi vimeeleza kuwa uamuzi wa kuwakamata vijana hawa umetokana na jeshi la polisi kupata mashtaka toka kwa watu wasiotajwa kwamba mtandao huo umekuwa ukiwachafua watu mbalimbali hususani viongozi wa serikali; suala hili nao linakwenda kinyume cha misingi ya kikatiba na kisheria. Sisi tunaamini kwamba kama kuna mtanzania yoyote ambaye anadhani amekashifiwa na mtandao huo ana haki ya kukanusha ama kuchukua hatua za kisheria kwa kwenda mahakamani. Mikakati hii ya kuzuia uhuru wa habari iliwahi kujitokeza siku za usoni pale upinzani ulipotoa ‘orodha ya mafisadi’ na baadhi ya vyombo vya habari kuchapa majina hayo vilipewa vitisho mbalimbali na watuhumiwa hao wa ufisadi ambao walisema wamechafuliwa.

Serikali na vyombo vya dola ni vyema vikafahamu kwamba uhuru wa maoni kupitia katika mitandao unafaida zake na hasara zake, hivyo kuundoa uhuru wote kwa sababu za malalamiko ya watu wachache, masuala binafsi au migogoro ya familia Fulani ni kuukosesha umma faida ambazo zinatokana na mitandao kama Jambo Forum. Pia serikali ifahamu kwamba sheria nyingi za Tanzania zinasimamia masuala ya habari ziko kimya kuhusu masuala ya habari katika mitandao hivyo, mitandao kama Jambo Forum inalindwa kwa kanuni na mikataba ya kimataifa ambapo imesajiliwa.

Tunarudia tena kukumbusha kuwa mwanahabari ni mjumbe tu wakufikisha ujumbe katika jamii; ambaye anapaswa kulindwa na kuheshimiwa. Tabia inayoanza kuchipua ya kuwanyanyasa wajumbe au chombo kilichofikisha ujumbe tena kwa njia ambazo ni kinyume cha sheria na haki binadamu badala ya kuushughulikia ujumbe wenyewe; ikiachwa ikashamiri inaweza ikatishia ufanisi wa sekta ya habari ambayo inapaswa kudumishwa kama mhimili wa nne wa dola.

Aidha vijana wa CHADEMA tumesikitishwa na kutoweka hewani kwa mtandao wa Jambo Forum ambako kutokana na vyanzo mbalimbali inaelezwa kwamba waratibu wa mtandao huo wameshinikizwa kuufunga kutokana na shinikizo la ‘kigogo’ mmoja wa jeshi la polisi kwa maelekezo toka serikalini.

Jambo Forum Wanahabari imekuwa mstari wa mbele kwa uwazi bila woga katika mapambano dhidi ya ufisadi na kutetea rasilimali za taifa, na kuwa sehemu ya jukwaa la sauti umma kusikika na habari kusambaa ndani na nje ya Tanzania kutia teknolojia ya habari na mawasiliano(TEKNOHAMA). Jambo Forum imekuwa mstari mbele katika kuandika tuhuma za ufisadi na/au matumizi mabaya ya madaraka zinazowakabili viongozi kadhaa wa serikali, makampuni na taasisi mbalimbali.

Mtandao wa Jambo Forums ni moja katika ya vyombo vya habari na majukwaa ya umma yaliyohusika kwa kiasi kikubwa kwa kulifunua na kuliweka wazi sakata la Richmond hasa baada ya kuweka hadharani mkataba wa Richmond na kuchambua mambo mbalimbali yanayohusiana na mkataba huo. Kashfa ya Richmond ndiyo iliyosababisha kujiuzulu kwa Waziri Mkuu Mhe. Edward Lowassa na baadaye kuvunjwa kwa baraza la Mawaziri. Jambo Forum imewezesha ‘siri’ za ufisadi zinazofichwa na baadhi ya vigogo ikiwemo serikalini kuwekwa wazi kwa umma na watumishi mbalimbali wa serikali na taasisi mbalimbali bila majina yao kujulikana.

Mtandao wa Jambo Forum umekuwa ni changamoto kwa mitandao mingine ya serikali ikiwemo kitengo cha mawasiliano cha Ikulu kuboresha ufanisi wao katika kutumia TEKNOHAMA katika kuwasiliana kwa umma. Mtandao huo umekuwa ni ukumbi pia wa vyombo vya ulinzi na usalama ikiwemo polisi kupata mawazo mbalimbali ya umma kuhusu masuala ya uhalifu yanayopaswa kufuatiliwa.

“Inashangaza badala ya serikali kutoa ushirikiano kwa mitandao kama hii inakuwa mstari wa mbele kuona kwamba inafungwa. Huku ni kukinzana na dhamira ya Rais Kikwete ya kuongeza uhuru wa habari na haki ya Taarifa hapa nchini. Sisi tulitegemea vipaji vya vijana wanaotengeneza mitandao mbalimbali vikuzwe kwa maslahi ya Taifa badala ya kukamatwa”.

Vijana wa CHADEMA tunatoa rai kwa umma kutochukulia suala hili kuwa ni tukio dogo linalowahusu vijana wawili waliokamatwa bali litazamwe kama tukio linalohusu maslahi ya taifa, uhuru wa vyombo vya habari na haki za kikatiba za kupata na kutoa taarifa/mawazo.

Hivyo tunaitaka serikali kutoa tamko la kina lenye kueleza ni kwa sababu zipi zilizopelekea kukamatwa na vijana hawa na walalamikaji ni wakina nani. Pia serikali itoe tamko rasmi kama imeufungia mtandao wa Jambo Forum au la na tunawataka watanzania wanaoratibu mtandao huo kwa mapenzi mema ya nchi yao waurudishe mtandao huo hewani mapema iwezakanavyo wakati tamko la serikali linasubiriwa. Kadhalika tunatoa rai kwa yoyote ambae anadhani hajatendewa haki ama amechafuliwa na Jambo Forum ajitokeze kukanusha au kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mtandao huo badala ya kulitumia jeshi la polisi ama baadhi ya watu kuhujumu haki ya umma ya kupata na kutoa taarifa.

Katika mataifa mbalimbali duniani, mitandao kama Jambo Forum inachukuliwa kama sehemu ya vyombo vya habari na mahali pa umma kukutana kujadili masuala mbalimbali. Hivyo uamuzi wa kufungia Jambo Forum, ni sawa na uamuzi wa kufungia chombo kingine cha habari kama redio, televisheni na magazeti. Kadhalika, uamuzi wa kufungia Jambo Forum ambapo umma wa watanzania kwa maelfu umekuwa ukikutana kujadili masuala mbalimbali ni sawa na kupiga marufuku kukusanyika huko ambapo ni kinyume cha katiba ya nchi na mikataba ya kimataifa ya haki za binadamu. Mwisho, tunaitaka serikali na vyombo vya dola visidhani Jambo Forum ni Maxence Melo ama Mike Mushi bali mihimili ya Jambo Forums kwani ni umma wa wachangiaji na wasomaji waliosambaa hapa nchini na nchi mbalimbali ambao baadhi yao wanaweza kukamatwa, majukwaa yao kuweza kushambuliwa, lakini mawazo yao ya mabadiliko yataishi milele hata pale ndoto ya maendeleo, uhuru na umoja itakapotimia katika taifa letu.


Imetolewa tarehe 20 Februari 2008 na:


John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana
0754694553

Labels:

Thursday, January 17, 2008

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


WAZIRI MAGUFULI INGILIA KATI HATMA YA WAKAZI KIBAMBA
UTEKELEZAJI WA MRADI WA MIUNDO MBINU YA NGAZI YA WILAYA ENEO LA LUGURUNI NA KIBAMBA HOSPITALI KUKIUKA SHERIA ZA ARDHI ZA TANZANIA NA HAKI ZA MAKAZI
MAOFISA WANAOTUHIMIWA KUJIHUSISHA NA RUSHWA NA KUVUNJA HAKI ZA BINADAMU KATIKA UTEKELEZAJI WA MRADI WACHUKULIWE HATUA.
MCHAKATO WA MRADI UWEKWE WAZI KWA UMMA


Kwa tamko hili naungana na wakazi wenzangu wa Jimbo La Ubungo wanaokaa katika Kata ya Kibamba kupinga kitendo cha kutaka kuwahamisha Kimabavu kutoka katika ardhi na makazi yao ambavyo wamemiliki kihalali kwa mujibu wa sheria za nchi ya Tanzania kwa kushirikisha ngazi zote za Serikali ya Muungano wa Tanzania zikiwemo Serikali za Vijiji, Mitaa, Kata, Manispaa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi. Kuwahamisha Kimabavu ni ukiukwaji mkubwa wa Sheria za Ardhi pamoja na Haki za Makazi kama zilivyoainishwa katika Tamko la Kimataifa ya Haki za Binadamu, ambayo Tanzania imesaini.

Kwa hakika, vitendo vya watumishi wa Wizara yako, Halmashauri ya Jiji na Manispaa ya Kinondoni waliokabidhiwa jukumu la kutekeleza mradi huu vimepelekea utekelezaji wa mradi huu kuchukua sura ya kuhamisha watu kimabavu kutokana na kukiuka kabisa mwongozo wa uhamishaji watu kama ulivyoainishwa katika Sheria ya Kimataifa ya Haki za Binadamu na Haki za Makazi; mikataba ambayo Tanzania imeridhia. Na baada ya kuridhia Serikali ya Tanzania iliwajibika kuuingiza mwongozo huo katika Sheria za Ardhi zinazoongoza watu kuhamishwa kutoka katika Ardhi na Makazi yao.


Hivyo basi namuomba Mhe John Magufuli- Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi kuingilia kati suala la wananchi wa Jimbo la Ubungo Kata ya Kibamba kuhamishwa kimabavu katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundo mbinu eneo la Luguruni na Kibamba Hospitali na kufanya yafuatayo:-

1) Wizara yako isitishe notisi ya siku 30 iliyotolewa kwa waathrika kuwa wamehama.

2) Wizara yako isitishe vitendo vya kuvunja mkataba kati yake na wananchi wa Luguruni na Kibamba Hospitali uliofikiwa mwezi Febrauari 2007 kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa miundo mbinu ngazi ya wilaya eneo la Luguruni na Kibamba Hospitali kwa kutumia ardhi ya wananchi waliopo.

3) Wizara yako ifanyie uchunguzi wa kina malalamiko ya ukiukwaji taratibu zilizomo ndani ya Sheria ya Ardhi na Sheria ya Kimataifa ya Haki za Binadamu na Haki za Makazi.

4) Wizara yako isitishe zoezi zima la utekelezaji wa mradi huu hadi hapo tathmini itakayo washirikisha waathrika kuhusu kuepukika au kutoepukika kwa uhamishwaji watu katika utekelezaji wa mradi huu. Mchakato wa mradi mzima uwekwe wazi kwa umma ikiwemo bajeti ya mradi na mchakato wa utekelezaji. Kama Serikali (Wizara ya Ardhi, Nyumba na Makazi, JIJI na Manispaa ya Kinondoni) hazitaki kuwashirikisha waathrika katika kupendekeza mbinu mbadala badala ya watu kuhamishwa, ziwajibike kuhakikisha inapata ridhaa wote itakaowahamisha badala ya kufanya hivyo kwa mabavu.

5) Endapo baada ya tathmini shirikishi, baadhi ya kaya zitalazimika kuhamishwa, mpango kabambe ambao utakaokuwa shirikishi uandaliwe kuhusu hatma ya kaya zitakazolazimika kuhamishwa. Mpango huo uandae kwa uwazi raslimali za kutosha kuwalipa fidia itakazowezesha kaya husika kurejea katika kiwango cha maisha walioyokuwa nayo kabla ya kuhamishwa.

6) Endapo baada ya tathmini shirikishi, baadhi ya kaya zitalazimika kuhamishwa tathmini ya thamani ya mali ifanyike upya ikiwashirikisha independent valuers kwa nia ya kuepuka vitendo vya wananchi kudaiwa rushwa.

7) Wizara yako isimamie majadiliano ya pamoja kati ya watekelezaji wa mradi na waathrika kutathmini endapo zipo mbinu zinzoweza kutumika kuepuka watu wasihamishwe kutoka katika ardhi na makazi yao k.m waathrika wakaelekezwa kuwekeza katika miradi mchanganyiko na makzi kama inavyofanyika eneo la Kariakoo.

8) Wizara yako, JIJI na Manispaa ya Kinondoni viyafanyie uchunguzi wa kina madai yote ya rushwa, ufisadi na ukiukwaji wa haki za binadamu vinavyodaiwa kutendwa na maafisa waliopewa jukumu la kutekeleza mradi huu kwa nia ya kuwabaini watumishi wasio waaminifu ili waondolewe wasiiendelee kuipaka Serkali matope mbele ya wananchi. (kama ilivyoelezewa katika barua ya wazi ya wananchi kwa mamlaka zinazohusika ya tarehe 03 Januari 2008 ambayo nimeiambatanisha)


Imetolewa 16 Januari 2008 na:


John Mnyika
Mkurugenzi wa Vijana Taifa(CHADEMA) na Mkazi wa Jimbo la Ubungo
0754694553

Monday, January 14, 2008

Majibu kuhusu Utamaduni wa Amani

Prosper,

Nakubaliana na maoni yako, ndugu zetu wa Kenya hususani na Kibaki na Raila wanapaswa kuweka utaifa wao mbele na kutafuta suluhu ya mgogoro unaoendelea kufukuta huko. Na ni funzo kwetu wa Tanzania kwamba tufanye mabadiliko sasa kuhakikisha mifumo yetu ya uchaguzi na kisiasa inakuwa huru na inasimama mstari wa mbele katika kulinda haki na amani.

Huu ujumbe ameandika kaka Mwakatobe mwenyewe kwa mkono wake? Sitaki kuamini!Kila uhuru ana haki ya mawazo na fikra, lakini binadamu anapotoa mawazo tofauti na imani yake ambayo imezoeleka na wengi kuna haja ya kujiuliza maswali mengi sana. Nitaendelea kujiuliza. Ukipata wasaa wa kuonana naye naomba umwulize ana kwa ana kama ujumbe huu ameuandika yeye.

Sidhani kama mwakatobe ambaye tulikuwa naye NYF miaka mingi nyuma kabla ya kuingia kwenye siasa- wakati huo tukiwa kwenye harakati tu za kawaida za kuhamasisha mabadiliko ya kiraia nchini, sidhani kama alikuwa na mawazo kama haya. Na kwa kweli binafsi nimepata nafasi ya kubadilishana naye mawazo kirafiki kabisa maeneo mbalimbali hapa dsm na hata nje ya mkoa- kuanzia nyumbani kwake mpaka kwenye vikao vya ndani. Ukimweleza hivi najua atakumbuka mengi sana! Kama ujumbe umeandikwa mwenyewe- basi binadamu ni kiumbe cha pekee sana! Nitajaribu kuingia katika kumbukumbu zangu kuona kama nipata maandiko yake ya wakati huo, ikiwemo ile itikadi/falsafa aliyokuwa akiitetea. Je, ni wakati huo ndio alikuwa akiandika alichokuwa akiamini au ni sasa ndicho anachokiamini, Je, ataendelea kuamini hivyo? Nini asili ya uongofu huu? Kwa kweli, nikianza kuandika kwa undani kumbukumbu hizo za zamani, tukio hata tukio, hatua hata hatua- kwa kweli nitajikuta naandika mambo mengine binafsi kabisa! Sitafanya hivyo. Na wala si nia yangu kuandika makala ya gazetini, sitafanya hivyo pia. Kwa kuwa siamini kama makala haya uliyonitumia ni fikra huru za kaka Gwandumi Mwakatobe!

Nakubaliana na maandiko haya kwamba AMANI ni tunu ya muhimu sana, na inafaa kulindwa kwa gharama zozote. Nakubaliana pia kwamba Tanzania ina UTAMADUNI WA AMANI. Ila mwandishi alipaswa kujiuliza- Utamaduni nini? Je, utamaduni huweza kuzaliwa na kufa? Nini asili ya utamaduni wa amani katika Tanzania? Na yapi yanaweza kufanya utamaduni huo kutoweka?

Msimamo wa Kaka Gwandumi huko nyuma umekuwa ni kuwa Tanzania pamoja na kuwa tuna amani lakini kuna watanzania wengi hawana amani- na hali hii ya kukosa kwao amani inachangiwa pia na kukosa kwao haki, na wengine ni kutokana na hali mbaya ya maisha iliyozidi mipaka. Katika mazingira hayo msimamo wake wakati wote umekuwa kama ule wa Mwalimu Nyerere ambao pia ni msimamo ulioko kwenye Biblia ambayo Kaka Gwandumi amekuwa akiitumia kwa muda mrefu kwenye maandiko yake. Kwamba AMANI ni TUNDA la HAKI. Ndio maana sitaki kuamini kama msimamo huu mpya ni wa Kaka Gwandumi.

Nakubaliana na mwandishi katika utangulizi kwake kwamba njia za amani ndizo ambazo ni za kwanza kabisa, na za kistaarabu katika kufikia malengo ya kisiasa. Ila sikubaliani naye kwamba njia zingine ni njia ambazo madhara yake hayawezi kufutika milele. Naandika ujumbe huu leo Januari 12 ambapo Wazanzibar wameadhimisha mapinduzi ya umma yaliyomwaga damu kumng’oa sultani; Je, anataka kusema kwamba mapinduzi yale- yeye kama mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi, anayatangaza kuwa ni haramu na njia mbaya zaidi iliyowahi kutumika katika historia ya Taifa letu ambayo itasababisha visiwa vile visiwe na Amani milele? Afrika Kusini ilitumia muda mwingi mijadala na kujenga hoja huku makuburu wakitumia risasi za moto, ANC baadaye ikaazisha Umkotwo we Sizwe, jeshi lake hili ambalo lilifanya uharamia kwa serikali ya makuburu ikilenga miundo mbinu yao- ni harakati hizi ziliwarudisha makaburu kwenye meza ya majadiliano. Sisemi hivi kuhalalisha mapinduzi ya kijeshi; njia ambayo katika siasa za sasa za ustaraabu ni njia ya mbali kabisa. Nasema hivi kufuta hoja ya mwandishi, na mifano kwa kweli iko mingi sana duniani. Hawa wastaarabu wa demokrasia wa magharibi tunaowazungumzia leo, karibu kila taifa lao limepitia katika ushenzi usiomithilika kufikia katika ustawi walio nao sasa! Sisemi hivi kuhalalisha kwamba sasa tuwe washenzi, nasema hivi ili mwandishi wa makala haya ajaribu kutafakari kidogo- “Hivi kwa nini binadamu wanafikia hatua ya kuwa washenzi?”.

Mwandishi amejaribu kujenga hoja kwamba AMANI ndiyo kipeo cha yote. Na amani hiyo ndiyo ameiita URITHI MKUU WA UTAMADUNI WETU WA KISIASA. Kama nilivyosema, utamaduni huzaliwa, hukua na huweza hata kufa? Mwandishi ajiulize, ni mambo gani yanatishia kuua huu utamaduni? Niliwahi kuandika hapa baadhi ya mambo ambayo yanaweza kutishia kufa kwa utamaduni wetu wa amani, mambo ambayo baadhi hata Nyerere mwenyewe alishawahi kuyatabiri- bonyeza hapa kusoma andiko langu hilo:Jambo moja utabaini;
http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_15.html HAKI( kwa maana ya JUSTICE ambayo ni zaidi ya RIGHT); ni roho ya AMANI. Bila haki amani iko shakani. Haki ikitoweka, amani haiwezi kuishi hata kwa kuandika makala elfu na maelfu za propaganda kuhusu umuhimu wa amani katika nchi yetu. Namna ya kuendeleza uhai wa amani hiyo ni kuchambua, kukemea na kuondoa mizizi inayotishia haki za wengi. Mwandishi amesema AMANI ni urithi mkuu; lakini mwandishi anajua kuwa urithi ni jambo jema lakini si kila mrithi anauwezo wa kutunza urithi kama mwenye mali mwenye ambaye aliichuma kwa tabu hatua kwa hatua. Kauli ya kwamba huu ni urithi pekee haiwezi kulinda urithi huo.

Ukiona viongozi wa serikali wanazomewa hadharani. Ukioana wananchi wanaanza kujichukulia sheria mikononi wenyewe. Huku viongozi na makada wakiendelea kuiamba AMANI,AMANI, AMANI! Wananchi wakiendelea kuimba HAKI, HAKI, HAKI!. Hizo ni alama za nyakati. Ni wakati wa viongozi na wananchi kukaa na kutafakari na kuzungumza lugha moja. Si wakati wa viongozi na kikundi cha watu wachache kuwahubiria kile wasioamini. Tembelea maeneo ya migodi, pata hisia za wananchi. Jaribu kaa vijiweni, sikiliza wananchi wanazungumza nini kuhusu ufisadi na watawala wao. Mambo haya yatahitaji mchambuzi kama huyu, aliyeandika kurasa zote hizi kuyafanyia kazi kwa manufaa ya taifa letu. Na ni kwa kuchukua hatua ndipo tutakuwa kweli walinzi wa AMANI. Ni kwa kuamka, na kukemea aina zote za UBAGUZI, zinazoanza kujitokeza katika nchi yetu, ndipo tutadumisha Taifa lenye AMANI.

Umemkweza lakini wakati huo huo umemtweza Kinjeketile; niliwahi kuandika, tunu ya yangu kwa shujaa huyu:
http://www.chadema.net/makala/mnyika/mnyika_13.html mwandishi wa uchambuzi huu kama naamini anajua historia ya nchi yetu pamoja na upotofu wote wa kihistoria uliofanyika. Anajua kwamba Kinjekitile ni mtu ambaye anapaswa kujengewa Minara kama ambavyo wakina Nyerere wanabigiwa baragumu! Wajerumani wametumia muda mrefu katika nchi yao mwaka jana kukumbuka vita vya Maji Maji, wanajua ni mapambano ya namna gani yalifanyika. Na mara baada ya Vita hivi utawala wa Kijerumani haukuwa tena katika hali ya awali hapa nchini. Falsafa ya maji, ilikuwa ni falsafa ya mapambano tu; lakini mbele yake waliokuwepo machifu na viongozi wengine wa kiafrika na wapambanaji wao waliokamata silaha. Mataifa ya wenzetu, chimbuko la uzalendo wao- ni harakati za watu kama hao. Lakini sisi tunawabeza! Uzalendo utatoka wapi? Uzalendo huchachushwa kwa moyo za hisia za kutazama mambo makubwa yaliyofanyika katika Taifa!

Mwandishi anajua kwamba Wajerumani ndio walikokuwa wakoloni halisi, huku waingereza ambao Mwalimu aliwakimbiza kwa Harakati za Ndani na Zile hotuba za umoja wa Mataifa kwa kuwa walikuwa na wadhamini tu. Najua mwandishi anayajua haya yote! Mwandishi anajua kwamba kama waingereza wangekuwa walowezi Tanganyika kama ilivyokuwa kwa Kenya ni wazi baada ya Maji Maji ingezaliwa Mau Mau nyingine hapa kwetu. Mwandishi anajua haya! Anajua kwanini tulipeleka vikosi vyetu vijana wetu wakapoteza damu kuleta ukombozi kusini mwa Afrika- Msumbiji, Angola, Afrika Kusini nk! Anajua haya. Hata Nyerere aliyajua haya, ndio maana hakupeleka njia za Amani na Maelewano huko(Non Violence Method); Nyerere aliyekuwa kiongozi aliyejua falsafa ya mapambano. Alijua adui anayetumia mbinu gani akabiliwe kwa mbinu gani!. Ndio maana hakutaka kukaa meza moja ya majadiliano na maelewano na Iddi Amini Dada! Unadhani Nyerere hakuwa anajua “urithi mkuu na utamaduni wetu wa kisiasa” za AMANI?

Mwandishi ametumia muda mrefu kujenga hoja kwamba WAPINZANI wanachochea vurugu, uhasama, ugomvi, matusi, kejeli nk na kwamba ndio wanaoelekea kuvunja AMANI nchini. Lakini mwandishi ameshindwa kutaja mifano ya kauli au matukio hayo na yalihusu wapinzani gani! Ujumbe huu, ukisomwa juu juu, waweza kuaminika na kuviza imani ya watanzania kwa watanzania wenzao walioko kwenye upinzani. Lakini tukumbuke, Mandela alipopinga ubaguzi aliitwa mpinzani mwenye kuvunja amani. Nyerere aliitwa na serikali ya mkoloni, mpinzani mwenye kuvunja amani na akashtakiwa kwa uchochezi. Mchambuzi mahiri kama huyu, angetumia muda kuvitaka vyombo vya dola kuchukua hatua kwa wapinzani hao kama kweli wanavunja amani ya nchi!. Mwandishi akumbuke kwamba, kwa mpinzani Dr Slaa alipojitokeza hadharani kusema ufisadi wa Benki Kuu(BOT) aliitwa majina yote ambayo mwandishi huyu ametumia kueleza tabia ya upinzani. Leo hii baada ya Rais Kikwete kuona ukweli wa mambo tena katika sehemu ndogo tu ya ukaguzi wa EPA; wale wote waliosema maneno hayo sijui kama wanajisikia AMANI mioyoni mwao! Ndio maana sitaki kuamini kama ameandika Kaka Mwakatobe ujumbe huu, kwa kuwa najua yeye anajua , na huwa anapenda sana kutumia biblia- na ndani ya kitabu hicho kuna simulizi ya Yesu ambaye naye aliitwa majina kama hayo na watawala wa wakati huo. Lakini leo wakristu wote kote duniani wanamuita jina tofauti kabisa!

Siasa za kistaraabu za kujenga hoja naziunga mkono! Siasa safi, za sera na hoja. Na ndio ambazo upinzani umekuwa ukifanya. Dr Slaa alianzia bungeni, akajaribu kutoa hoja ya awali ikapuuzwa. Akaongeza ukali zaidi wa maneno, hakueleweka. Akaongeza uzito zaidi kwa kuandaa hoja binafsi, akaletewa mizegwe. Na hapo ndipo alipotumia lugha kali zaidi, kwamba ‘hawa ni wezi na mafisadi’. Leo mpaka Kikwete naye ameanza kutumia lugha kali! Lugha ambayo miezi michache nyuma, mawaziri waliikebehi kama ambayo makala hii inakebehi upinzani!. Wote kati yetu, mtu akichukua mali- tutazungumza kwa ‘urithi wa utadamuni wetu wa kisiasa’, “Naomba nirudishie”; asiporudisha lugha gani hufuata?

Mwandishi ameendelea mbele kuonyesha nia ya maandiko yake pale alianza kujenga hoja kwamba Nyerere alisema ‘kiongozi bora lazima atoke CCM”; mwandishi anasahau ni Mwalimu huyu huyu alisema “CCM sio Mama yangu”. Mwandishi akasome maandiko ya mwisho mwisho ya Mwalimu Nyerere kwenye “Uongozi wetu na hatma ya Tanzania”; hakika hii kansa ya uongozi Nyerere alishaitabiri, na unaweza kubashiri kama angekuweo sasa na ufisadi angefanyaje! Kama kweli Nyerere aliamini kwamba “Kiongozi bora lazima atoke CCM”; Mwandishi anaweza kutuelezaje yaliyotokea kule Musoma baada ya mfumo wa vyama Vingi kuanza ambapo Baba wa taifa alimnadi wazi mgombea wa Upinzani Balozi Ndobho kwa ubora wake na kumuacha wa chama chake CCM? Watanzania tunapaswa kuwa na siasa zilizo juu ya vyama, zinazotazama zaidi maslahi ya Taifa.

Mwandishi anajenga hoja kwamba dosari kuu ya upinzani ni kutaka wananchi wakichukie Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake! Mwandishi anajua kabisa kwamba wema ni sumu ya uovu. Kama CCM na serikali yake wanatenda mema, unadhani wananchi wanaweza kuchukia hata wapinzani wangesambaza chuki? Lakini kwa kuwa kuna UOVU unajaribu kufichwa ni wazi kwamba yoyote anayesema UKWELI, ataonekana ni mchonganishi na mchochea chuki. Wakina Dr Slaa, Zitto wote wanaitwa waongo, huku wakina Mbowe na wengine wakiitwa wachochezi, Wakina Kubenea wakimwagiwa Tindikali na wakina Ndimara Wakikatwa mapanga. Hiyo ndiyo AMANI! Bahati nzuri, watanzania wanaelewa, na ipo siku KITAELEWEKA!

Eti, kero ya wapinzani ni kuona CCM inazidi kuimarika na kukubalika! Ndio maana siamini kabisa kuwa haya ni maneno ya Kaka Mwakatobe. Mwandishi anasema watanzania hawafanyi utafiti kubaini ukweli huu, anasahau kuwa ni watanzania hawa hawa ndio wametoa maoni yao kwenye tafiti mbalimbali kwamba umaarufu wa CCM umeporomoka. Sio sababu ya chuki ya upinzani, ni kwa chama hicho kushindwa kutekeleza ahadi lukuki ilizotoa. Huu ni ukweli ambao mwanaCCM yoyote makini anaufahamu.

Mchambuzi huyu anarudia kauli ya mara kwa mara ya kwamba wapinzani hawana DIRA- lakini mchambuzi huyu huyu anajua hazina ya sera ambazo CCM imekuwa ikichota kutoka upinzani kuanzia enzi za kufuta kodi za manyanyaso mpaka kipindi hiki cha kupitia mikataba ya madini. Mchambuzi huyu anajua kuwa “Maisha Bora kwa Kila Mtanzania” ni lengo tu la MKUKUTA ambao umeandaliwa na wananchi wote bila kujali itikadi na kuchukuliwa tu kwenye ilani ya Chama tawala. Mchambuzi amesahau kabisa kwa CCM imeshatelekeza falsafa na itikadi yake, na hata Mwalimu Nyerere amekiri hili kwenye kitabu cha Uongozi Wetu na Hatma ya Tanzania. Mwandishi angetueleza- DIRA YA CCM ni ipi? Mchambuzi mahiri kama huyu alipaswa awe anafahamu kabisa Dira na mwelekeo wa vyama vingine nchini. CHADEMA mathalani, mambo haya yamefafanuliwa Kwa CHADEMA falsafa na itikadi yake inapatikana hapa:
http://www.chadema.net/maoni/kijue.php na ilani yake ambayo utangulizi wake ni dira ya “Tanzania tunayoitaka” inapatikana hapa: http://www.chadema.net/ilani/tanzania.php na popular manifesto 2005 inapatikana hapa http://www.chadema.net/maoni/ilani.php . Lakini Ndio maana sitaki kabisa kuamini kwamba aliyeandika ni Kaka Mwakatobe, kwa kuwa najua kabisa yeye alikuwa kwenye jopo la wataalamu waliofanya mapitio ya Sera na Katiba ya CHADEMA mwaka 2003/04. Wakati huo, mimi hata sikuwa mwachama wa CHADEMA. Kwa maneno mingine, najua Kaka Mwakatobe anafahamu vizuri asili ya Falfafa ya “Nguvu ya Umma”. Hivyo, sifikiri kabisa kwamba anaweza kusema upinzania hauna dira! Yeye anafahamu kwamba hata Mwalimu Nyerere aliwahi kusifia Sera za CHADEMA.

Bahati nzuri nilikuwepo CHADEMA mwaka 2005, na nilikuwa mgombea Ubunge wa Ubungo wakati huo; najua undani wa mambo. Mwandishi amezusha kwamba mwaka 2005 CHADEMA iliponzwa kwa kujipendekeza kwa wafadhili; wafadhili gani, kujipendekeza gani? Hapa mwandishi anataka kusheheneza hisia kwamba CHADEMA ilipewa mapesa kutoka nje na kuyatumia kwenye helikopta na kuwatelekeza wagombea wa ngazi nyingine. Bahati nzuri, ni CHADEMA pekee iliyotangaza wazi matumizi yake ya fedha katika kampeni. Rejea Tamko la Baraza Kuu la CHADEMA hapa:
http://www.chadema.net/uchaguzi/ripoti1.php CCM mbona mpaka leo haijatangaza? Hapa imeelezwa wazi kiasi gani tulitumia, kiasi gani zilitumika kwenye helikopta. Lakini tulikwenda mbele zaidi kutangaza ni kiasi gani zilipatikana toka nje. Tuliweka wazi, kampeni zetu hajikuchangiwa kwa fedha toka nje- zimegharamiwa kwa ruzuku ya chama ni michango ya wanachama mbalimbali. Kitu pekee tulichopata toka kwa rafiki zetu wa nje ni ruzuku kidogo ya kuendesha warsha ya mafunzo kwa wagombea ubunge, na michango hii ya kiufundi haikutolewa kwa CHADEMA tu katika kipindi cha kuelekea uchaguzi. Mchambuzi huyu, angepaswa aandike uchambuzi wa kutaka CCM itangaze mapato na matumizi yake ya uchaguzi-na angeuliza vile vile, zile tuhuma za fedha za uchaguzi wa CCM kutoka nje ya nchi ambazo walisema wangelishitiki gazeti la nje lililofichua suala hilo zimefikia wapi? Kama mchambuzi huyu hafahamu tuhuma hizo- asome humu atazipata: http://www.chadema.net/habari/misc/misc_10.html .Baada ya kuchambua hapa, atajua ni chama kipi cha siasa ‘kinajipendekeza’ kwa wafadhili wake wa wakati wa uchaguzi!

Inasikitisha kwamba mchambuzi kama huyu, anadiriki kudanganya kuwa CHADEMA ilikuwa ikitumia milioni 10 kwa siku kwa ajili ya helikopta! Huu ni uzushi kabisa. CHADEMA haijawahi kutumia milioni 10 kwa siku kwa ajili ya kukodi helikopta. Niliwahi kuchambua gharama za matumizi ya helikopta katika makala yangu iliyotoka katika vyombo vya habari vya nyumbani- makala hiyo inapatikana pia hapa:
http://www.chadema.net/blogu/mnyika/2008/01/helikopta-ya-chadema-raha-karaha-au.html .Ni vyema akajiridhisha na kusema ukweli.

Mchambuzi huyu, anataka kujenga picha kwamba upinzani unapokea mabilioni mengi ambayo ingeweza kabisa kujenga zahanati, shule, hospitali nk ili kuonyesha kwa vitendo. Mchambuzi anataka kujenga picha kwamba vyama vya upinzani vinatapanya fedha! Mwandishi anashindwa kujua kwamba ruzuku ya vyama inatolewa kwa kazi maalumu za kisiasa ambazo sheria ya vyama vya siasa imeelekeza. Mwandishi anashindwa kujua kwamba michango mahususi inayotolewa inatolewa kwa kazi mahususi. Mchambuzi anashindwa kujua kabisa kwamba huwezi kupewa mchango wa kuendesha mafunzo wa viongozi ukapeleka kwenye kujenga zahanati pamoja na umuhimu wake. Kubwa kuliko yote, mwandishi anaashindwa kuelewa kazi ya vyama vya siasa- anashindwa kujua kwamba vyama vya siasa vinatoa sera na viongozi ili watumie vizuri rasilimali kuleta barabara, zahanati nk. Mwandishi anashindwa kujua kwamba michango ya wafadhili mbalimbali inapitia serikalini kutoa huduma za kijamii na kutekeleza miradi ya kimaendeleo- kazi ya upinzani ni kuiwajibisha serikali iliyoko madarakani na kutoa mwelekeo mbadala! Mwandishi anashindwa kujiuliza mbona CCM inapokea ruzuku ya takribani bilioni mbili(milioni 2000) kila mwezi kutokana na fedha za walipa kodi, wakati CHADEMA inapokea milioni 56 tu kwa mwezi lakini CCM haijengi barabara, zahanati kutokana na ruzuku hiyo? Badala yake madarasa, zahanati nk zinajengwa kwa kodi za wananchi kupitia bajeti ya nchi, michango ya wananchi na fedha toka kwa wadau wa maendeleo? Ni kutokujua au kupotosha?

Hili la kusaidia miradi ya kuthibiti umaskikini: Linahitaji mjadala zaidi, tujiulize- duniani kote, kazi ya vyama vya siasa ni nini? Imani yangu ni kuwa CHADEMA tumeweza kufanya vizuri katika miradi mbalimbali katika halmashauri ambazo tumeongoza Kigoma Ujiji, Hai na Karatu; na tuendelea katika halmashauri ambazo tumeanza kuongoza baada ya 2005, sasa tunaoongoza pia Halmashauri mpya moja ya Tarime. Sidhani kama upinzani unatakiwa kugawa fedha za miradi ya kuondoa umasikin- kufanya hivyo, kuna vikwazo vifuatavyo: Mosi, tutakuwa tunatoa takrima ya maendeleo kwa wananchi toka mifukoni mwa chama ambayo kimsingi ni rushwa, Pili, tutatoa fursa kwa mafisadi nao kuanza kutoa michango hiyo kupitia vyama vyao- sasa mwenye kisu kikali ndio atakula nyama. Tatu, tutakuwa tumetoka katika malengo ya msingi ya chama cha siasa. Kwa maoni yangu, chama cha siasa ni muunganiko wa watu wenye mawazo yanayoshabihiana kwa lengo la kuchukua dola ili kutekeleza mawazo hayo, na kabla ya kuchukua dola kuiwajibisha dola iliyoko madarakani kwa misingi ya mawazo hayo! Kwa hiyo bidhaa za vyama vya siasa ni 'uongozi', 'sera' na 'oganizesheni'. Kwa hiyo, tunaondoa umasikini kwa kutoa viongozi bora, sera bora na oganizesheni bora. Kwa sasa pamoja na kuwa upinzani tumewatoa wakina Dr Slaa, Zitto nk ambao wanaiwajibisha serikali kwa sera zinazopinga ufisadi na kutetetea rasilimali za taifa, kwa kweli matokeo ya harakati zao ni fedha zetu za kodi kutumika vizuri zaidi katika miradi ya kuondoa umaskini. Naamini kabisa, serikali ya sasa(pamoja na ufisadi unaoendelea) kwa staili hii ya Orodha ya mafisadi kila mmoja yuko tumbo joto- hivyo, sidhani kama watakuwa na ari, nguvu na kasi mpya ya kufuja fedha za miradi ya kuondoa umaskini kama ilivyokuwa wakati wa Mkapa- sasa kama hali ikiwa nzuri kiasi nani atanufaika kama sio mwananchi? Nani amesababisha manufaa hayo kama si upinzani? Na ikifika 2009 na 2010 changamoto kwetu ni kuwafanya watu waelewe kwamba wakituchagua sisi tutaingia wenyewe kutekeleza sera hizo vizuri zaidi tofauti na CCM inayofanya mambo machache tena baada ya shinikizo. Kama ni kutokujua, niliwahi kuandika hapa kazi chama cha siasa- na ni kwa vipi upinzani unasaidia maendeleo nchini: “Huduma za Kijamii zinazotolewa na Vyama Vya Siasa vya Upinzani. Akitaka naweza kumtumia hilo andiko. .Leo upinzani ukiwezesha bilioni 133 zilizofujwa BOT zikapatikana unajua ni madarasa, barabara na zahanati ngapi? Kati ya chama kutumia milioni 56 kufanya harakati za kisiasa za kupambana na ufisadi na kuokoa bilioni 133 na chama kutumia milioni 56 kujenga matundu ya choo nyumbani kwa wananchi wachache kipi bora?

Ndio maana siamini kama ujumbe huu umeandikwa na kaka Mwakatobe; najua anaujue Ukweli huu, na anajua kuwa UKWELI ni UHURU. Na anajua kwamba utumwa wowote unaosababishwa na jitihada ya kulinda maslahi binafsi na ni suala baya. Lakini anajua zaidi, kujaribu kuambikiza utumwa huo kwa kizazi cha baadaye cha Taifa hili ni DHAMBI. Na Ole wake yule ayakayesababisha mmoja wapo wa watoto hawa kutenda dhambi...................


JJ

Ps: Unaweza kuutuma ujumbe huu kwa Kaka Mwakatobe na marafiki zetu wengine, lakini usiupeleke kama makala ya kwenye gazeti kwa kweli. Sijafanya uhariri wowote wala kuweka mpangilio, nimeandika mawazo kwa kadiri yalivyokuwa yakitiririka. Heri ya Mwaka Mpya na wasalimie Kigoma.




Saturday, January 12, 2008

‘HELIKOPTA YA CHADEMA’: RAHA, KARAHA AU ‘SILAHA’?

Na John Mnyika

Wakati wa uchaguzi mkuu 2005 “Helikopta ya CHADEMA” ilizua hamasa na mjadala mkubwa. Wako walioponda na wapo waliosifia. Mapema mwaka huu baraza kuu la CHADEMA lilitangaza kwamba chama kitaendelea kutumia helikopta kama moja ya vitendea kazi wakati wa utekelezaji wa mpango mkakati wa miaka mitano ya chama hiki. Wiki chache zilizopita vyombo kadhaa vya habari viliripoti kwamba CHADEMA inatarajia kutumia helikopta katika ziara yake ya kuwashukuru wananchi na kutekeleza baadhi ya mikakati ya chama huku chombo kimoja cha habari kikisema kwamba “Helikopta hiyo itakodiwa kwa dola 1200 kwa saa hivyo kwa saa 24 itakuwa dola za kimarekani 28,800 kwa siku. Hii ni sawa zaidi ya milioni 35 kwa siku”. Eti, CHADEMA itakodi helikopta kwa shilingi za kitanzania 35,000,000 kwa siku!. Hoja na maswali mbalimbali yametolewa kuhusu helikopta. Lengo la makala hii ni kujibu baadhi ya maswali na kupanua mjadala kuhusu matumizi ya helikopta. Wakati serikali ilipoamua kutumia magari ghali maarufu kama mashangingi, palikuwa na mjadala mkali. Wakati serikali iliponunua ndege ya raisi kwa takribani bilioni 40 mjadala ulikuwa kitu cha muhimu. Wakati serikali iliponunua rada ya kijeshi kwa gharama kubwa hutukuweza kuepuka kujadili kama walipa kodi. Kadhalika CHADEMA kama chama cha siasa kinaposemwa kinataka kutumia milioni 35 kwa siku kukodi chombo cha usafiri tunapaswa kwa kweli kukijadili. Tunawajibu huo kwa kuwa vyama vya siasa ni asasi za wanachama. Lakini pia ni asasi za umma kwa kuwa zinaendeshwa kwa pesa za walipa kodi kwa kiasi fulani. Hii ni kwa sababu ruzuku inayotolewa na serikali kwa vyama vya siasa vyenye wabunge na vilivyofikisha asilimia inayotakiwa ya kura inatokana na kodi za wananchi.

Si kweli kwamba gharama za kukodi helikopta ni shilingi milioni 35 kwa siku. Na kwa mtazamo wangu ni kwamba katika kufanya ziara mfulululizo za kisiasa katika nchi kubwa kama Tanzania helikopta ni nafuu kuliko magari na ndege. Najua wengi mtashangaa!. Huu ndio ukweli. Helikopta nyingi duniani zinakodishwa kati ya dola 1000 na dola 2000 kutegemea aina, mwendo kasi, msimu nk. Uchaguzi 2005 CHADEMA ilikodi helikopta ya dola 1200 kwa saa. Kwa kampeni zote zilizoratibiwa na makao makuu ya chama, CHADEMA ilitumia jumla ya Tsh milioni 750 na ushee. Kati ya hizo ni sh milioni 223 tu zilitumika kwenye helikopta. Na si bilioni 3 kama baadhi wanavyosema, na pesa hizi zilitoka wanachama na wapenzi wa chama humu humu nchini. Na kwa kweli CHADEMA inapaswa kupongezwa kwa kuwa wazi kusema imetumia shilingi ngapi na kuvitaka vyama vingine navyo viseme. CHADEMA iliviambia vyama vingine navyo viseme toka Mei sasa ni Disemba. Kimya!!!Bado wanaandaa mahesabu toka Disemba mwaka jana uchaguzi ulipokwisha!.

Nirejee kwenye mjadala wa helikopta!. Wasichojua watu ni kuwa helikopta, tofauti na vyombo vingi vya usafiri gharama zake za kukodi zinahesabiwa kwa muda ambao helikopta inakuwa hewani. Helikopta ikiwa chini hailipiwi gharama za kukodi. Wanachofanya tu ni kukupa kiwango cha chini kabisa cha kuruka kwa siku ambacho mara nyingi ni saa moja na kiwango cha chini kabisa cha siku za kukodi ambacho kwa mashirika mengi ni wiki moja. CHADEMA katika uchaguzi uliopita ilikuwa inatumia kati ya saa moja hadi mawili kwa siku!.

Sasa tuchukue kadirio la juu- masaa mawili kwa siku, hii inafanya gharama kuwa dola 2,400 kwa siku. Mafuta ya ndege ni kati ya tsh 900 na 1200 kwa lita. Ila kwa uzoefu wanngu mafuta ya masaa mawili ni takribani asilimia 10 ya gharama za kukodi kwa hiyo ni dola 240. Jumla kwa siku ni takribani dola 2640, tufanye 2700 ili tuweze kufanya mahesabu kwa urahisi. Tukigeuza kwenda fedha za kitanzania hii ni sawa na takribani 2,970,000 kama dola moja ikiwa shilingi 1100 .

Kwa hiyo gharama ya CHADEMA kukodi helikopta kwa siku ni shilingi hata tukimbandisha kupindukia milioni 3 tu. Ukifanya mikutano 8 kama ambavyo Mbowe alikuwa akifanya kwenye uchaguzi 2005 kwa siku hii ni sawa na wastani wa kadirio la juu wa shilingi laki nne kwa mkutano mmoja. Laki nne kwa mkutano mmoja wa mgombea urais. Hizi ni pesa kidogo. Mkutano uliofura watu ambao wamekuja wenyewe bila kubebwa na FUSO wala mabasi wala kuletwa kulipwa posho wala kuja kwa kupewa fulana na kofia. Wanakuja kwa ridhaa yao. Hii ni kuwa very cost effective(umakini katika gharama)! Iliwahi kusemwa kwamba Naambiwa mkutano mmoja wa kikwete wa Jangwani uligharimu tsh milioni 20. Hii ni sawa na mikutano mingapi ya helikopta? Gharama za kukodi ‘shangingi’ moja kwa siku ni dola 200. Hii ni sawa na 1/6 ya kukodi helikopta kwa gari moja tu!. Kikwete alikuwa na msafara wa mashangingi mangapi katika msafara wake wa kampeni? (watasema aliyanunua- sawa sasa tuyahesabu katika rate ya kukodishwa!). Haishangazi katika maeneo walikuwa wakitumia mashangingi ya serikali. Msafara wa magari mengi unahitaji watendaji kiasi gani? Kama kila mmoja akilipwa posho ya kati ya 20 na 30 jumla ya gharama kwa siku ni kiasi gani? Kikwete na Shein walikuwa wavuki kwa magari pekee mkoa hadi mkoa. Walikuwa wakitumia ndege ya serikali. Eti walikuwa wanaikodi. Ndege ya serikali kukodi ni bei gani kwa safari? Inatofauti gani na helikopta? Lakini je, ndege inaweza kutua kijijini na kufanya mikutano kama nilivyosema? Haya ndiyo mambo yanayohitaji mjadala!

Wapo wanaotoa hoja kwamba helikopta inafika maeneo machache tu. Ukweli ni kuwa helikopta inafika maeneo mengi hata yale yasiyofikika kirahisi. Katika uchaguzi uliopita CHADEMA ilitumia magari katika awamu ya kwanza ya kampeni. Tukapata uzoefu wa kutumia magari katika kampeni za urais. Kumbuka hii ilikuwa ni mara ya kwanza kusimamisha mgombea urais. Katika awamu ya pili na kuendelea CHADEMA ilitumia helikopta. Mosi, Baada ya kuanza kutumia helikopta CHADEMA ilikuwa na uwezo wa kufanya wastani wa mikutano 8 kwa siku. Hii ilifanya Mbowe awe mgombea aliyefanya mikutano mingi kuliko mgombea mwingine yoyote tena katika maeneo yenye utofauti mkubwa wa umbali. Pili, CCM ni wajanja, siku za kampeni(kabla ya muda kuongezwa ni around 70) wakati ambapo nchi ina wilaya zaidi ya 130 na majimbo zaidi ya 230. Mgombea urais anayetumia magari kufanya mkutano mmoja kila wilaya kwa siku hawezi kumaliza nchi nzima katika kipindi hiki kifupi cha kampeni. CCM inatumia ‘faida’ ya kuwa na wakuu wa wilaya, wakuu wa mikoa nakadhalika kuziba mapengo na kuwa na ‘nguvu ya ziada ya kushindana’(competitive edge). Njia moja ya kuwazidi kete ni kutumia helikopta kwenda maeneo tofauti kwa haraka. Tatu, CCM imeshindwa katika miaka zaidi ya 45 ya utawala wake imeshindwa kuweka mtandao mzuri wa barabara mpaka vijijini kabisa. Hiki ni kikwazo cha wagombea wa uraisi kufika kila mahali. Yapo maeneo ambayo mpaka sasa wanadhani Nyerere bado ni rais. Hapafikiki kirahisi. Helikopta ilikuwa na makawa na jenerata ndogo. Ipo mikutano ambayo ilifanyika vijijini kabisa ambapo ingekuwa ngumu kufika kwa magari katika wakati mwafaka. Huku ni kuwafikishia ujumbe wa mabadiliko wananchi waliopembezoni kabisa!. Sasa itatumika tena kuchambua mwaka mmoja serikali imefanya nini na imeshindwa kufanya nini na kuwahamasisha uwajibikaji na kusambaza ‘TUMAINI JIPYA’. Hii ni kwa manufaa kwa Taifa zaidi ya vyama..

Wapo waliotoa hoja kwamba helikopta imekuwa ikimbeba Mbowe pekee na kwamba inawakosesha fursa viongozi wengine kuhutubia mikutano. Si kweli kwamba helikopta ilimbeba Mbowe pekee. Helikopta inategemea ukubwa. Ile ambayo CHADEMA ilikodi katika uchaguzi 2005 ilikuwa na uwezo wa kubeba abiria 3 na rubani. Kwa hiyo kupanga ni kuchagua, unaamua tu kuchagua ni viongozi wangapi wapande. Kwa hiyo alikuwa akipanda Mbowe, mratibu wa ziara ya helikopta ambaye humsaidia pia rubani kutambua maeneo na nafasi ya kiongozi mmoja. Hapa ilitegemea mahali. Yapo maeneo ambayo alipanda mgombea mwenza, yapo maeneo ambayo mgombea wa eneo husika wa ubunge alipanda na yapo maeneo ambayo kiongozi wa chama wa eneo husika alipanda. Kwa hiyo ilifanyika kutokana na hali na mahali. Binafsi nilipanda helikopta ilipokuja Ubungo- tulitua Kimara, Mbezi, Mabibo, Urafiki na kadhalika. Nilipanda kama mgombea ubunge wa jimbo la Ubungo katika mwaka 2005. Kwa hiyo wagombea wanaosema helikopta ni ya Mbowe pekee ni wazushi. Tatizo ni kuwa ilikuwa ukitaka kupanda helikopta lazima uache jimbo lako uende kuipandia katika jimbo ambalo mkutano wa mwisho unafanyika kabla ya kufika kwako. Kwa hiyo wapo waliamua kubaki jimboni kwao waisubiri ije wampokee mgombea urais. Ilikuwa ni suala la kuchagua tu. Lakini kupanda helikopta ni nini mpaka watu wagombanie? Kiongozi wa chama wa eneo husika anapaswa kuwa uwanjani akimsubiri mgombea wake wa urais au kiongozi wa kitaifa afike ampokee, hizo ndizo itifaki.

Wapo wanaotoa hoja kwamba hizo pesa zilizotumika kwa ajili ya helikopta zingepelekwa katika matumizi mengine. Nyerere aliwahi kusema, kupanga ni kuchagua. Hizo milioni 200 na ushee zilizopelekwa katika helikopta zingepelekwa katika matumizi mengine zisingeleta kishindo kama ambayo imeletwa na helikopta. Kupanga ni kuchagua. Lakini, kama ni kupelekwa maeneo mengine shilingi milioni 500 zilipelekwa katika maeneo mengine mathalani mabango, vipeperushi, vyombo vya habari, kusaidia wagombea ubunge katika maeneo ambayo chama kilikuwa na uwezekano mkubwa wa kushinda kwa mujibu wa tathmini ya vikao vya huu vya chama.

Wapo wanaosema helikopta ni ‘raha mustarehe’ hivyo ni ishara ya Mbowe na CHADEMA kupenda anasa. Ukweli ni kuwa helikopta ni suluba, helikopta ni kazi. Kwa yoyote aliyewahi kupanda helikopta ya polisi ambayo inashabihiana na ile iliyotumiwa na CHADEMA anajua kuwa kupanda helikopta ni kuweka roho rehani kama sio hewani. Helikopta inaleta suluba ya kuongeza idadi ya mikutano, binafsi nampa pole Freeman kwa kuhutubia mikutano mingi namna hiyo kwa siku. Huyu jamaa angekuwa ‘kimeo’ angeanguka siku nyingi sana! Lakini jamaa alikuwa wima siku zote za kampeni. Sijasikia ameanguka jukwaani. Helikopta ni chombo cha kazi. Helikopta tunayotumia haina kiyoyozi kama mashangingi, haina viti vinavyofanana na masofa kama mashangingi. Haina raha kama ndege ya serikali wala haina anasa kama ndege ya rais. Hakuna wahudumu ndani wala ratiba ya kupewa juisi na keki. Karaha ya helikopta ni harufu ya moshi na vumbi la upepo mkali unaposhuka. Ni ishara ya mapambano na harakati!. Ni ‘silaha’ ya vita vya kidemokrasia dhidi ya mfumo mbovu wa utawala unaopenda anasa!

Wapo wanaojenga hoja kwamba Tanzania bado haijafikia ngazi na hadhi ya viongozi wake wa vyama vya siasa kutumia helikopta.Lol, salaale! Huku ni kujidharau. Wakenya jirani zetu hapo wanatumia helikopta mpaka kukagua mashamba. Ile helikopta ambayo CHADEMA ilikodi pamoja na kurudi kufanyiwa matengenezo ilitumiwa pia na watu wa mashindano ya magari. Ni helikopta ilitumika kuhamasisha wananchi kwenye vuguvugu la chungwa(ODM) kuhusu katiba Kenya. Lazima tuwe na viongozi wenye kuona mbali na kujua nini tunastahili kwa raslimali tulizonazo!. Hatuwezi kuwa na chama kinachoona jembe la mkono ndio halali yetu tukipanda kidogo eti tutumie plau na mikokoteni ya kukokotwa na ng’ombe. Tunapaswa tuwe na uwezo wa kufikiri ‘nje ya boksi’.

Wapo wanaosema kwamba suala la kutumia helikopta ni uamuzi binafsi wa Mbowe. Ukweli ni kuwa helikopta ni mkakati wa CHADEMA sio wa Mbowe. Uamuzi wa kutumia helikopta ulifanywa na baraza kuu la chama na kuridhiwa kwa kauli moja na mkutano mkuu wa CHADEMA. Sio uamuzi wa Mbowe ule!. Hata baada ya uchaguzi, baraza kuu lilikaa tena kutathmini na kwa kauli moja walipongeza matumizi ya helikopta na kupitisha azimio la kuendelea kutumia helikopta. Kwa hiyo helikopta ni mkakati na utamaduni wa CHADEMA. Helikopta inatarajiwa kutumika tena kwenye ziara TUMAINI JIPYA. Lakini helikopta ni njia moja tu inayotumiwa na viongozi wa kitaifa kwa kipindi fulani kwa nia fulani ya kisiasa!Kuwafikia wananchi wengi kwa muda mfupi na ujumbe mahususi. Ipo mikakati mingine, mathalani „CHADEMA ni Msingi“, kama ni jeshi basi huu ni mkakati wa vikosi vya ardhini. Wa chini kwa chini!. Huu unahusisha kutuma vikosi vya makada na viongozi wa kitaifa kufanya mikutano midogo ya hadhara katika kijiji na mitaa na kuingia mikutano ya ndani kutoa mafunzo na kujenga netweki au oganizesheni ya chama nganzi ya chini kabisa!. Huu utaanza mara baada ya helikopta ‚kulipua mabomu’ ngazi ya juu. Hii ni sayansi ya vita vya kisiasa....hii ndiyo vita ya kidemokrasia ya kuhamasisha nguvu ya umma.

Wapo waliosema kwamba ‚mtoa ujumbe kwa kutumia helikopta hufika na ujumbe wake na kuondoka na ujumbe wake’. Ukitaka kujua kuwa ujumbe wa helikopta ulileta hamasa angalia jinsi ambavyo wagombea walikuwa wakiweweseka baada ya helikopta kupita maeneo yao. Utakuwa huwatendei haki watu wa Tarime kwa mfano kuwaambia kwamba baada ya Helikopta kupita na Mbowe kumwaga maneno alipoondoka walisahau kila kitu. Ingawa nakubali kuwa kuna baadhi ya maeneo CHADEMA ilisia mbegu katika jangwa na pengine katika magugu. Ni hadithi ya mpanzi! Ndio maana sasa CHADEMA imeamua kujikita katika kusuka vizuri na upya uongozi wa chama ngazi ya chini. Tunaanza uchaguzi kuanzia msingi, tawi na kuendelea mpaka taifa kuanzia uchaguzi wa mwakani. Watanzania wategemee chama kuongeza nguvu. Tunachotaka ni nguvu na mamlaka ya umma.

Ila suala la muda wa kuzungumza naamini linastahili kuzingatiwa. Kwa hiyo katika awamu ya sasa nategemea kwamba mikutano ya helikopta itahusisha saa si chini ya moja kwa kila mkutano kwa mzungumzaji mkuu kuweza kuzungumza. Kwa maneno mengine sasa badala ya mikutano nane na zaidi kwa siku itapaswa kufanyika mikutano kati ya minne na mitano tu kwa siku. Hakuna kulala mpaka Kieleweke. Watoto wa kijiweni husema, huu utakuwa ni wakati wa makamuzi ya kufa mtu!.

Wapo wanaosema kwamba watu hufika kushangaa helikopta tu! Kuna rafiki yangu mmoja hupenda kujibu hoja hii kwa mzaha kwamba, unaweza kuja kushangaa ndevu za shekhe ama padri lakini kwa dakika tano unazomsilikiliza ukaona TUMAINI JIPYA. Hivi!, tunawafanya watanzania washamba kiasi hiki kiasi kwamba hawajui kuchagua jema na baya.....wapo washangaaji-nakubali, lakini wapo pia ambao yanayozungumzwa huwasukuma kuamua.

Wapo viongozi na wagombea wachache wanaojitoa katika upinzani na husema kwamba wanajitoa eti kwa kuwa Mbowe anatumia helikopta badala ya kutoa pesa kwao. Wahenga husema „Mbaazi zikikosa maua husingizia jua’!

Ukweli ubaki pale kwamba helikopta ina wapenzi na washabiki wengi. Inapondwa zaidi na viongozi wa juu hususani wa CCM kama sehemu ya mikakati ya kuichafua CHADEMA na kuchochea migogoro. Hivi majuzi tu wakati wa uzinduzi wa mikakati ya CCM katibu mkuu wa chama hicho alisikika ‚live’ akisema kwamba waachane tu waruke na helikopta wakati sisi tunazindua mikakati. Bila kukumbuka kwamba CHADEMA ilitangulia kuzindua programu yake ya miaka mitano katikati ya mwaka juzi kabla ya CCM kufanya hivyo wiki iliyopita.

Najua wapo pia wachambuzi wachache wanaoponda matumizi ya helikopta lakini najua bi kutokana tu na kutopata siri za upande wa pili wa shilingi kuhusu helikopta. Lila na fila havitangamani asilani.

Ukweli ni kwamba helikopta ni chombo tu kinachomwezesha mwanasiasa wa kitaifa katika nchi kubwa na yenye miundo mbinu duni kama ya kwetu kufika katika maeneo mengi na pengine hata yasiyofikika kwa muda mfupi na kwa gharama nafuu. Helikopta ni ubunifu na ishara kwamba CHADEMA ingekuwa madarakani ingetumia ubunifu mwafaka mathalani hata katika kuleta umeme, badala ya kuja na ‚ubunifu wa RICHMOND.

Mwandishi wa makala hii ni Mkurugenzi wa Vijana wa CHADEMA anayepatikana kupitia mnyika@yahoo.com , www.chadema.net na 0754 694 553

Friday, January 26, 2007

PROFESA MSOLLA : SULUHISHO LA MIGOMO NI KUTOA HAKI KWA WANAFUNZI

Na John Mnyika

Hivi karibuni, akiwa mkoani Mbeya katika majumuisho ya ziara yake ya vyuo vikuu. Waziri wa Sayansi teknolojia na elimu ya juu, Mh Prof-Peter Msolla, alinukuliwa na vyombo vya habari akitoa vitisho kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kwa madai kuwa wanafunzi wanaohusika na migomo vyuo vikuu wanajiandalia mikosi na kwamba hawatapata ajira baada ya masomo yao.

Prof Msolla ametoa kauli hiyo huku kukiwa na vuguvugu la wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kupinga taratibu za sasa za utoaji mikopo ambapo kwa mujibu wa taratibu za sasa ambazo kimsingi zinakinzana na sheria halisi ya mikopo. Pamoja na mapungufu mengine ya msingi ni kwamba wanafunzi wanalazimika kuchangia asilimia 40 ya gharama za masomo. Na sasa vuguvugu hili huenda likasambaa zaidi wakati wowote kwani mpaka sasa kuna taarifa kuwa baadhi ya wanafunzi katika baadhi ya vyuo wanashinikizwa kuchangia pesa hizo ambazo ni kati ya laki 3 na zaidi ya laki 5 ili waruhusiwe kuingia darasani sambamba na kupewa huduma zingine za msingi.

Aidha, hivi karibuni, vyombo vya habari vimeandika kwamba wanafunzi wa Chuo cha Kilimo Sokoine (SUA) waliendesha mgomo na kuja wizarani kutaka kuonana na waziri kupinga utaratibu wa kuchangia asilimia 40 ya mkopo. Pesa hizi ni takribani laki 5 ambazo walipaswa kuzilipa kabla ya kuanza masomo.

Imeelezwa kuwa serikali imewataarifu kuwa wasaini mikataba na kuendelea na masomo. Uamuzi huu unaweza kutafsiriwa kuwa tayari serikali imewasaidia wanafunzi hawa kuendelea na masomo.

Lakini ukweli ni kuwa huu ni mtego. Ni wazi kwamba serikali ama inasubiri kipindi cha karibu na mitihani ndipo iwabane wanafunzi kwa kuwataka kulipa hiyo asilimia 40 au inaweza kuwaruhusu wafanye mitihani na pindi watakapokwenda likizo ikatoa maelekezo kuwa wasiolipa wasirejee mpaka watakapopata pesa za kulipa.

Huu ni mkakati wa ‘wagawe uwatawale’ (divide and rule) ambao serikali imekuwa ikiutumia mara kwa mara kuvunja mshikamano wa wanafunzi. Na hii inathibitika kutokana na kauli ya Waziri wa Elimu ya Juu, Prof Msolla ambaye amenukuliwa na gazeti la Uhuru la Januari 17 akisema kwamba serikali haina mpango wa kulipa hiyo asilimia 40 kwa kuwa wanafunzi walikwishasaini fomu za mikopo na kwamba sharti hilo lilikuwa sehemu ya mkataba. Waziri anasahau kuwa fomu hizo zilishasainiwa na wanafunzi chini ya shinikizo la serikali pamoja na ahadi mbalimbali kwamba serikali iko mbioni kuandaa utaratibu mzuri zaidi. Tunachotaka ni serikali kutoa tamko kwamba itahakikisha kwamba utaratibu huu unafutwa kwa kutenga pesa katika bajeti ya mwaka huu ikiwemo za kulipia gharama za wanafunzi walioko masomoni hivi sasa.


Ni katika muktadha huo, tunapaswa kulijadili suala hili ili kuhakikisha serikali inafika mahala inakiri kuwa mikopo sio hisani , ni haki ya kila mtanzania anayepata udahili wa chuo kikuu kwa mujibu wa sheria inayounda bodi ya mikopo. Na kwa mantiki hiyo tunasisiza msimamo wetu katika misingi ifuatayo;

Migomo na Maandamano ni moja ya njia halali katika kudai haki.
Kauli ya Mh Waziri ni kama vitisho ambavyo vilikuwepo hata wakati wa serikali ya mkoloni wa kizungu kuwadhibiti wanafunzi wanao nyanyaswa na serikali yao wasipisisimamie haki yao kwa vigezo kwamba kufanya hivyo ni kujihatarishia mazingira ya ajira punde baada ya kumaliza masomo yao.

Tunapaswa kutambua kuwa nguvu ya umma ni hatua ya mwisho katika kuhakikisha umma unapata haki yake stahiki kutoka kwa serikali isiyojali. Migomo na maandamano ni hatua ya mwisho inayorejesha wadau katika meza ya majadiliano baada ya hatua za awali za majadiliano kutokuzaa matunda.

Maandamano na mashinikizo ya hali ya juu kutoka kwa wanafunzi wenyewe dhidi ya serikali ni mambo yasiyoepukika kama hatua ya mwisho kwani serikali yetu imekuwa na tabia ya kutowatendea haki wanafunzi kila wanaponyanyaswa mpaka wanapoamua kusitisha masomo kwa migomo na maandamano.

Hivyo kwa kuwa serikali imejenga tabia ya kutowasikiliza wanafunzi wa elimu ya juu mpaka wagome na kuandamana, Na kwakuwa migomo na maandamano ni njia zinazoruhusiwa kwa mujibu wa mikataba ya kimataifa ya haki za binadamu, katiba ya nchi na sheria za taasisi mbalimbali ikiwemo vyuo vikuu kama moja ya njia ya kushinikiza haki kutendeka. Hivyo si ajabu kwa wanafunzi wa elimu ya juu kufanya kila linalowezekana ikiwa ni hata kugoma na kuandama kwa mujibu wa sheria ili kuhakikisha haki yao inapatikana, inalindwa na kuheshimiwa.

Jumuiya ya wasomi kama vyuo vikuu kuacha haki yao inyongwe kwa hofu ya kitambo, tena isiyo na ukweli wowote ni mfano mbaya wa namna wasomi wanaotarajiwa kuwa mstari wa mbele kupigania mabadiliko ya msingi ili nchi hii ikombolewe wanavyoweza kudhulumiwa haki yao mbele ya umma unao watazama kama majemedari na wakombozi watarajiwa.! Ni usaliti wa hali ya juu.! Ni usaliti kwa nafsi zao, ni usaliti kwa taifa lao.

Ndio maana natoa rai kwa Mh Waziri kuacha vitisho, na badala yake ahakikishe wanafunzi wanapata haki yao kama kweli ni msomi mzalendo. Hakuna binadamu anayependa kugomagoma wala kuandamana. Serikali isiwaweke wanafunzi katika mazingira yanayowalazimisha kugoma na kuandamana.

Haiingii akilini kwa mwanafunzi kutishwa kuwa asigome na wala kuandamana kwa madai kuwa kufanya hivyo kunahatarisha ajira yake hapo baadae wakati ukweli ni kwamba mwanafunzi asipogoma hatopata mkopo, na asipopata mkopo atafukuzwa chuo, hatomaliza Chuo. Sasa kama hatopata mkopo na kushindwa kumaliza chuo, ni ajira gani ambayo Msola anasema wanafunzi wanahatarisha ?

Mapungufu ya sera na utekelezaji wa sera ya mikopo.
Utaratibu wa sasa wa mikopo una mapungufu mbalimbali ya kimsingi ambayo yanaleta mkanganyiko wa hali ya juu katika taifa hili, na zaidi unatishia mustakabali wa elimu hiyo kwa wanafunzi wa kitanzania wanao toka familia masikini.
Mosi ; Dhana ya uchangiaji wa gharama za elimu ya juu imegeuzwa kuwa mfumo wa kufanya elimu ya juu nchini kuwa bidhaa inayouzwa badala ya huduma (service). Dhana nzima ya uchangiaji gharama za masomo ya elimu ya juu imepotoshwa , Kwa mujibu wa sera ya serikali , Mwanafunzi anatakiwa kuchangia asilimia 40 na serikali kumchangia asilimia 60 ya mkopo wote.

Lakini kinachotokea ni kwamba, wanafunzi wanapewa mkopo wa asilimia 60 (huu ni mkopo sio mchango kwani watalipa), na baadae mwanafunzi anatakiwa kujilipia mwenyewe asilimi 40 ya gharama zinazobaki.

Hivi katika muktadha huu, serikali inawezaje kusema kuwa inawachangia wanafunzi kusoma elimu ya juu ? Hii ni cost sharing ya namna gani ? .Kilichopo hapa ni mwanafunzi kujilipia asilimia 100 za gharama za masomo yake (total cost bearing).

Pili ; Dhana ya kutoa mkopo kwa wanafunzi waliofaulu kwa daraja la kwanza wavulana, na la kwanza na la pili wasichana ina mapungufu ya msingi. Kwanza inapingana na sheria ya mkopo kuwa kila atakayekidhi vigezo vya mkopo ikiwa na maana ya kupata usajili/udahili wa chuo na kuhakikisha kuwa hana uwezo wa kujisomesha atapatiwa mkopo. Kinachozungumzwa hapa ni kufikia viwango vya kusajiliwa/kudahiliwa chuoni na sio utaratibu wa madaraja kama ulivyoelezwa hapo juu.

Baada ya upinzani kutoa msukumo katika suala hili, serikali ilirudi nyuma kidogo na kuamua kutoa mkopo kwa baadhi ya wanafunzi wa daraja la pili wavulana na la tatu wasichana ambao wengi wao walijiunga na ualimu. Hii ni kwa mujibu wa kauli ya Mh Rais kuwa pamoja na serikali kuwaruhusu baadhi ya wanafunzi wa daraja la pili wavulana, na la tatu wasichana, lakini bado vigezo vilivyowekwa katika fani mbalimbali ni kikwazo kwa wanafunzi hawa kujiunga na vyuo husika.(mathalani katika fani za udaktari na uhandisi).

Vigezo vilivyowekwa vilizingatia uhaba wa fursa zilizopo kwa msingi wa ni kiwango gani serikali imepanga kutoa mkopo katika fani fulani. Kwa mantiki hiyo, serikali inapotoa tamko kuwa imewaruhusu wanafunzi wa daraja la pili wavulana na la tatu wasichana katika fani chache, bila kuhakikisha vigezo vinabadilishwa, ni sawa na kutoa haki ambayo haipo. Ni kuwafanyia ‘usanii’ vijana wake.

Ni vyema Mh Rais atambue hilo, lakini pia atafiti kuhusu ukweli wa kauli yake kuwa serikali inasomesha wanafunzi waliofaulu vizuri kabisa kwa madai kuwa serikali haiwezi kuwekeza kwa wanafunzi wasio na uwezo.

Nasema hivyo kwa sababu kuu mbili : Kwa upande mmoja, kuna wanafunzi wengi wanao faulu kwa kiwango cha chini kutokana na mazingira ya shule wanazosomea, mifano dhahiri ni shule za serikali na zile za umoja wa wazazi wa CCM, shule hizi nyingi hazina walimu wala vifaa, mwanafunzi anayepata daraja la tatu au la pili katika shule za aina hii anao uwezo mkubwa wa kujifunza kuliko wanafunzi wengi wanao soma katika shule za kimataifa, seminari na baadhi ya shule za sekondari chache za serikali ambazo zinafaulisha vizuri.

Kwa upande mwingine, Kauli hii imekuwa ikithibitishwa na maprofesa wanaofundisha vyuo vikuu kwa kubainisha wazi kuwa wanafunzi wengi wanaofanya vibaya vyuo vikuu ni wale wanaotoka shule zenye majina makubwa ambao waliingia kwa alama za juu. Kwa maana hiyo basi, hoja ya Mh. Rais kumchukulia kila mvulana aliyepata daraja la pili na kila msichana aliyepata daraja la tatu hawezi kufanya vizuri sana, ina mapungufu hayo ya msingi.

Tatu ; Dhana ya kwamba waliopata daraja pili wavulana, na la tatu wasichana kuwa ndio wenye uwezo wa chini kitaaluma, na kwa hiyo wataenda ualimu ni kielelezo kuwa , serikali yetu inaamini Ualimu ndio taaluma isiyohitaji utaalamu sana, na hivyo haihitaji watu wenye uwezo mkubwa. Kitu ambacho kimewahi kurudisha maendeleo ya taaluma nchini kwa miaka kadhaa sasa.

Nne ; Mwisho lakini kubwa zaidi ni kwamba chama tawala CCM katika ahadi zake wakati wa kampeni iliahidi kuhakikisha inawapatia mkopo wanafunzi 30,000 kwa mwaka. Hata hivyo waliofaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza mpaka la tatu ni wanafuzi 21,000 tu. Hivyo kama serikali ingekuwa inatekeleza ahadi zake wanafunzi wote wangepata udhamini wa chuo kikuu. Hata hivyo zaidi ya nusu ya hao , ambao walikidhi vigezo vya mkopo hawakupata mkopo.

Rai yangu kwa serikali, namuomba tena Mh Rais amshinikize waziri wa elimu ya juu , aufahamishe umma wa Tanzania ni kwa kiwango gani serikali yako imeshindwa kutimiza ahadi uliyoitoa wakati wa kampeni. Na pia serikali ieleze ni wanafunzi wangapi walistahili mkopo kwa mujibu wa sheria lakini wamekosa na sasa inaandaa utaratibu gani kuhakikisha walikosa mwaka 2006 watapewa haki yao mwaka 2007, na kwamba mwaka 2007 kosa halijirudii na kwamba ahadi ya Mh rais itatekelezwa. Ili serikali iweze kutekeleza ahadi yake inapaswa kutenga si chini ya bilioni 195 kwenye bajeti ya mwaka huu kwa ajili ya mikopo. Hii inawezekana, kwani kama tunaweza kutenga bilioni 272 katika miradi yenye utata kama mkataba wa RICHMOND, inashindwaje kusikiliza matakwa ya wananchi ya kufanya suala la elimu kuwa kipaumbele ? Kama Mfanyabiashara mmoja wa kitanzania anaweza kutuhumiwa kupata shilingi bilioni 15 ambayo ni sawa na milioni elfu 15 kama ‘hongo ya asilimia 30’ kwenye ununuzi wa RADA tunaweza kweli kusema hatuna pesa za kusomesha wanafunzi elfu 15 wanaohitaji takribani shilingi milioni moja kwa mwaka ?

Mwelekeo wa elimu ya juu nchini.
Kwa ujumla kadri miaka inavyokwenda, na awamu za utawala wa CCM zinavyobadilika, ndivyo mwenendo wa elimu ya juu nchini unavyozidi kwenda kombo, na zaidi unaelekea kujenga matabaka ya masikini wasio na haki ya kupata elimu dhidi ya matajiri wenye uwezo wa kununua elimu.

Itakumbukwa kuwa katika awamu ya kwanza ya serikali ya TANU, na baadae CCM ya wakulima na wafanyakazi chini ya Hayati Baba wa Taifa. Mwl Julius Kambarage kwa mtazamo wa siasa ya ujamaa, wanafunzi wote walisomeshwa bure chuo kikuu. Walipewa mahitaji yote ya msingi kwa mwanafunzi kuweza kusoma. Mwalimu aliweza kuwapatia watoto wa wakulima na wafanya kazi masikini elimu ya bure bila hata ya kuuza migodi, hifadhi za wanyama makampuni na nyumba za serikali na mali zote za watanzania. Viongozi walioko madarakani hivi sasa wengi wao walisomeshwa na serikali, ni vipi wanashindwa kuweka utaratibu mzuri wa kizazi kipya kupata fursa ya elimu ya juu?

Serikali ya awamu ya pili ilijaribu kuwalazimisha wanafunzi wajilipie chuo kikuu, kwa sababu Mwalimu Nyerere alikuwepo, na wanafunzi walikuwa na uwezo mkubwa wa kujipanga na kupigania haki yao, serikali ilishindwa. Hata hivyo kadri Chama Cha Mapinduzi kilivyozidi kujipanga kuhakikisha kinamkandamiza mtoto wa kimasikini, ndivyo kilivyokaribia ushindi, hatimaye katika awamu ya tatu ya CCM kiliweza kushinikiza wanafunzi kujisomesha lakini kwa mkopo.

Baada ya serikali ya awamu ya nne kuingia madarakani , tulitarajia mabadiliko ya msingi katika elimu ya juu. Lakini mbaya zaidi kilichotokea ni kwamba ni mwenendo mbaya na wa ukandamizaji zaidi kwa wanafunzi wanaotoka familia masikini.

Wakati serikali ya awamu ya kwanza iliweza kuwasomesha wanafunzi wote bila kulipa hata shilingi wala mkopo, serikali ya awamu ya pili na ya tatu pamoja na kuuza migodi makampuni na mbuga za wanyama ilishindwa kuwasomesha wanafunzi masikini. Ilifuta utaratibu huo na kuanza kuwasomesha wanafunzi masikini kwa mkopo huku yenyewe ikijivinjari kwa maisha ya anasa katikati ya dimbwi linalotoa harufu ya umasikni.

Serikali ya awamu ya nne iliyoingia madarakani kwa ahadi kemkem na kujifanya yenyewe ndio mkombozi. Ndani ya mwaka mmoja tu, mwenendo na kasi yake mpya, unaelekea kummaliza mkulima na mfanyakazi ambaye ambae pamoja na ukweli kuwa ndio aliyepigania uhuru wa nchi hii ndio masikini wa kutupwa katika nchi hii

Wakati serikali ya awamu ya pili na tatu pamoja na uozo uliofanyika lakini iliweza kutoa mikopo. Serikali ya awamu ya nne kwasababu ya kuendekeza mikataba yenye mazingira ya rushwa na matumizi ya anasa sambamba na kukosa dira madhubuti ya uchumi, imeshindwa kutoa mikopo kwa wanafunzi masikini ambao ni watoto wa wakulima na wafanyakazi, na sasa inawataka waanze kujilipia.

Naona hatari kubwa huko tuendako, na bila wanafunzi na asasi za kiraia kushika bango, serikali itaturejesha kwenye utumwa mkongwe wa wageni, maana mali zote zinasombwa na wageni, huku viongozi wetu wakiingia mikataba yenye utata kila kukicha. Bila wanafunzi na asasi hizo kusimama wima kudai haki hii, nchi yetu inaelekea rasmi kuingia kwenye ukoloni mamboleo.

Hakuna nchi iliyofanya mapinduzi ya kisiasa, kiuchumi na kijamii bila ya kuwekeza zaidi kwenye elimu. Chama Cha Mapinduzi kinaposhindwa kufanya mapinduzi katika elimu maana yake hakiwezi kufanya mapinduzi katika maendeleo ya watu kama dhana ya mapinduzi ni katika maendeleo ya watu, labda kama maana yake ni vinginevyo.

RAI YANGU KWA VIJANA
Naomba na kusisitiza kuwa, vijana tusitishwe wala tusirubuniwe. Tunataarifa kuwa CCM kimeanza kupita vyuoni na mbaya zaidi kinavunja sheria kiliyoipigania chenyewe ya kukataza siasa vyuoni, lakini sasa kinawatumia viongozi wa vyuo kufanya mkakati wa kuwaingiza vijana CCM, siwazuii vijana kuingia CCM lakini CCM izingatie sheria za nchi kwa upande mmoja,

Na kwa upande wa pili, nawaomba vijana mtazame mbele zaidi , na kujiuliza mara mbili mara tatu juu ya ni nani atasimamia haki zenu ? Je sheria hizi zinamruhusu mdogo wako, ndugu yako, na hata mtoto wa jirani yako aliyeko kijijini kupata elimu ya juu?.Je unaweza kutetea na kuleta mabadiliko kwa mfumo uliopo kazi ambayo ilimshinda hata mwasisi wa CCM yenyewe, Hayati Baba wa Taifa letu, Mwl JK Nyerere ?

Muda wa kustarehe vijana bado !, nchi ipo kwenye lindi la tope la umasikini , tusichelee kudai haki yetu na kuisimamia nchi yetu ikae kwenye mstari mnyoofu kwa hofu potofu ya kunyimwa kazi, au ahadi za kupewa ukuu wa wilaya, ubunge, ukurugenzi, nk.

Tusimame pamoja tudai mabadiliko ya kweli mpaka serikali tuiweke kwenye kona yenye mwanga iweze kuona kuwa kupewa uongozi wa nchi ni kupewa dhamana na wananchi, na haina maana ya kuwa juu ya vichwa vya wananchi.

Na nawataka wanafunzi wa vyuo vikuu wasiwe wabinafsi na kusimama kidete kwenye migomo na maandamano wakati wa kudai haki zao za mikopo tu bali watazame maslahi ya umma kwa ujumla ikiwemo masuala ya kupinga mikataba mibovu kama IPTL, RICHMOND, kwenye madini, ununuzi wa RADA na ndege ya rais. Huku kuna mabilioni ambayo yalipaswa kuelekezwa kwenye elimu.

Profesa Msolla akumbuke maneno ya Mwanamuziki Bob Marley kwamba unaweza kuwadanganya baadhi ya watu kwa muda mchache lakini huwezi kuwadanganya watu wote kwa muda wote, na kama Mwalimu alivyowahi kusema haki haiwezi kupewa kwenye kisahani cha chai kama zawadi. Haki inatafutwa. Hakuna kulala, Mpaka kieleweke!

Mwandishi wa makala hii ni mwanaharakati na mwanasiasa kijana anayepatikana kupitia 0754 694 553, mnyika@chadema.net